M
MegaPyne
Guest
NI KUTOKA DODOMA NA MORO
JK AWAKABIDHI KADI AWAAHIDI AJIRA
Wanafunzi wa vyuo vikuu vilivyoko katika mikoa ya Morogoro na Dodoma wameipongeza Serikali ya Chama Cha Mapinduzi kwa uamuzi wake wa kuwapatia mikopo wanafunzi wa vyuo va elimu juu .
Wameeleza kuwa utaratibu huo wa Serikali ya CCM chini ya uongozi wa Rais Jakaya Kkikwete umewawezesha hata watoto wanaotoka katika familia za daraja la ‘tatu' nao kupata elimu ya juu.
Pongezi hizo zimetolewa na wanafunzi hao, muda mfupi kabla ya Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi, Rais Jakaya Kikwete kuwakabidhi kadi za uanachama wa CCM, baada ya wanafunzi hao zaidi ya 1000 kuamua kujiunga na chama hicho. Hafla hiyo ilifanyika jana jioni Jumatatu katika Makao Makuu ya CCM, Dodoma .
Wanafunzi hao ambao kwa kila chuo waliwakilishwa na wenzao wapatao 20 ni kutoka vyo vikuu vya Dodoma, Mtakatifu John, vyuo vya Mipango na Madini,(544), na SUA, Mzumbe na chuo kikuu cha Kiislamu vyote vya Morogoro (566))
"Mhe Rais na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi, kwanza tunapenda tukupongeze kwa ushindi mnono ulioupata katika uchaguzi uliomalizika leo (Jumatatu), ushindi huu unaonyesha ni kwa namna gani wajumbe wa mkutano mkuu walivyo na imani nawe" akasema mwakilishi wa wanafunzi kutoka vyuo vya mkoa wa Dodoma.
Akaongeza " lakini pia tunapenda kutoa shukrani zetu kwa Serikali ya Chama Cha Mapinduzi kwa kuwa na mipango mizuri ya kuwapatia wanafunzi wa vyuo vikuu mikopo, asante kwa mikopo hii ambayo imewawezesha watoto kutoka familia za daraja la tatu kupata elimu"
Hata hivyo wamesema wanafunzi hao kuwa pamoja na utaratibu huo mzuri, wanamwomba Rais kuangalia uwezekano wa kuongeza kiwango cha mikopo, kuharakisha upatikanaji wake na pia kuwasaidia wale ambao hawajapata hadi sasa.
"Mhe. Rais kuchelewa kwa mikopo hii kunatufanya wengine tuuze vocha za simu ili tujikimu, lakini pia kuna wenzetu ambao hadi sasa hawajafanikiwa kupata mikopo tunaomba hili uliangalie" akasema mwakilishi wa wanafunzi kutoka Dodoma, kauli iliyoshangiliwa na wanafunzi hao
Wanafunzi hao walimweleza Rais kwamba wamehamasika na kuamua kujiunga na CCM, na kuahidi kuwa watakilinda na wanamuunga mkono Rais katika juhudi zake za kuwatumikia Watanzania ili waweze kuwa na maisha bora.
Aidha wanafunzi hao kwa ujumla wao wamempongeza Rais Jakaya Kikwete kwa ushindi mnono alioupata katika Uchaguzi Mkuu wa CCM, na kwamba ushindi wake huo ni kielelezo cha namna gani anavyokubalika mbele ya wajumbe wa Mkutano Mkuu na kubwa zaidi ni kwamba wana imani naye.
Wamemwomba Rais apange ratiba ya kuvitembelea vyuo vikuu na kuzungumza na wanafunzi ili nao wapate wasaa mzuri wa kumpongeza. Wamemhakikishia kwamba wataendelea kuwahimiza wanafunzi wa elimu ya juu kujiunga na CCM, na kwamba zile fikra kwamba kuna upinzani dhidi ya CCM katika vyuo vikuu si sahihi.
Akizungumza na wanafunzi hao baada ya kuwakabidhi kadi zao, Rais alisema amefurahishwa sana na idadi kubwa ya wanafunzi wa vyuo vikuu kutoka Dodoma na Morogoro ambao wameamua kwa hiari yao kujiunga na Chama Cha Mapinduzi.
Akawaeleza kuwa Chama kina mkakati maalum kwa kuwavutia wasomi wengi kujiunga na CCM na kwamba hiyo ni njia bora na sahihi ya kuwaandaa viongozi katika ngazi mbalimbali za serikalini na katika Chama.
"Nimefurahi sana kwa kweli, kwa sababu chama lazima kipate wasomi, na nchi haiwezi kuendelea bila ya wasomi, na duniani hakuna nchi ambayo imeendelea kwa kuwa na watu mbumbumbu. Na ndio maana tulipoingia serikalini tulitoa umuhimu wa pekee katika elimu" akasema Kikwete.
Amewahakikishia wanafunzi hao kwamba, Serikali ya Chama Cha Mapinduzi imejiwekea mkakati maalum wa kuwaajiri wanafunzi waliohitimu chuo kikuu kuanzia ngazi ya tarafa.
Akawaeleza kuwa wasisite kwenda kufanya kazi katika tarafa kwani huko ndio kunakowafungulia uzoefu na fursa ya kupanda katika safu za uongozi ziwe za ukatibu tawala, ukuu wa wilaya, ukuu wa mikoa na nafasi nyingine nyingi.
"Tunamkakati maalum wa kuwaajiri wanafunzi, na mwaka huu tunaanza na wanafunzi wapatao 500 kutoka SUA, na ninapenda niwahakikishie kwamba vijana wasomo ambao tumewaajiri katika nafasi ya ukuu wa wilaya 12 kati yao wanafanya vizuri sana, hii inaonyesha umuhimu wa kuwaajiri wasomi" akasisitiza Rais.
Akizungumzia kuhusu suala la mikopo ya wanafunzi, Rais amewaahidi wanafunzi hao, kwamba kabla ya kuondoka mkoani Dodoma atahakikisha anakutana na Waziri wa Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu na Mwenyekiti wa Bodi ya Mikopo na kuangalia matatizo yaliyojitokeza ili kuyapatia ufumbuzi.
"Nataka niwahakikishie kwamba kabla sijaondoka hapa Dodoma nitakutana na Waziri na Mwenyekiti wa Bodi na kuangalia wapi pana tatizo na kulitafutia ufumbuzi, maana suala hili la mikopo limeingiliwa na watu wengi wakiwamo wanasiasa, lakini hatima yake anayeathirika ni mwanafunzi" akasema Rais na kushangiliwa na wanfunzi hao.
Amewaeleza kuwa Serikali inaandaa utaratibu wa kuboresha njia za mawasiliano kati ya Bodi ya Mikopo na wanafunzi wa vyuo vikuu.
Rais Kikwete pia alitumia fursa hiyo kuwaeleza wanafunzi hao juhudi na mikakati mbalimbali inayofanywa na Serikali katika uboreshaji na upanuzi wa elimu nchini kuanzia elimu ya awali hadi chuo kikuu na kwamba imejipanga vema kukabiliana na changamoto mbalimbali.
Kuhusu ombi la kutembelea vyuo vikuu, Rais ameahidi kupanga utaratibu na kwa kuanzia atakitembelea chuo kikuu cha Dodoma kabla hajaondoka.
Awali Katibu Mkuu wa CCM Yusufu Makamba aliwataka wanachama hao wapya kila mmoja wao kushawishi wanachama wapya watano kujiunga na Chama Cha Mapinduzi.
Source: Subirini Magazeti ya Kesho.
JK AWAKABIDHI KADI AWAAHIDI AJIRA
Wanafunzi wa vyuo vikuu vilivyoko katika mikoa ya Morogoro na Dodoma wameipongeza Serikali ya Chama Cha Mapinduzi kwa uamuzi wake wa kuwapatia mikopo wanafunzi wa vyuo va elimu juu .
Wameeleza kuwa utaratibu huo wa Serikali ya CCM chini ya uongozi wa Rais Jakaya Kkikwete umewawezesha hata watoto wanaotoka katika familia za daraja la ‘tatu' nao kupata elimu ya juu.
Pongezi hizo zimetolewa na wanafunzi hao, muda mfupi kabla ya Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi, Rais Jakaya Kikwete kuwakabidhi kadi za uanachama wa CCM, baada ya wanafunzi hao zaidi ya 1000 kuamua kujiunga na chama hicho. Hafla hiyo ilifanyika jana jioni Jumatatu katika Makao Makuu ya CCM, Dodoma .
Wanafunzi hao ambao kwa kila chuo waliwakilishwa na wenzao wapatao 20 ni kutoka vyo vikuu vya Dodoma, Mtakatifu John, vyuo vya Mipango na Madini,(544), na SUA, Mzumbe na chuo kikuu cha Kiislamu vyote vya Morogoro (566))
"Mhe Rais na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi, kwanza tunapenda tukupongeze kwa ushindi mnono ulioupata katika uchaguzi uliomalizika leo (Jumatatu), ushindi huu unaonyesha ni kwa namna gani wajumbe wa mkutano mkuu walivyo na imani nawe" akasema mwakilishi wa wanafunzi kutoka vyuo vya mkoa wa Dodoma.
Akaongeza " lakini pia tunapenda kutoa shukrani zetu kwa Serikali ya Chama Cha Mapinduzi kwa kuwa na mipango mizuri ya kuwapatia wanafunzi wa vyuo vikuu mikopo, asante kwa mikopo hii ambayo imewawezesha watoto kutoka familia za daraja la tatu kupata elimu"
Hata hivyo wamesema wanafunzi hao kuwa pamoja na utaratibu huo mzuri, wanamwomba Rais kuangalia uwezekano wa kuongeza kiwango cha mikopo, kuharakisha upatikanaji wake na pia kuwasaidia wale ambao hawajapata hadi sasa.
"Mhe. Rais kuchelewa kwa mikopo hii kunatufanya wengine tuuze vocha za simu ili tujikimu, lakini pia kuna wenzetu ambao hadi sasa hawajafanikiwa kupata mikopo tunaomba hili uliangalie" akasema mwakilishi wa wanafunzi kutoka Dodoma, kauli iliyoshangiliwa na wanafunzi hao
Wanafunzi hao walimweleza Rais kwamba wamehamasika na kuamua kujiunga na CCM, na kuahidi kuwa watakilinda na wanamuunga mkono Rais katika juhudi zake za kuwatumikia Watanzania ili waweze kuwa na maisha bora.
Aidha wanafunzi hao kwa ujumla wao wamempongeza Rais Jakaya Kikwete kwa ushindi mnono alioupata katika Uchaguzi Mkuu wa CCM, na kwamba ushindi wake huo ni kielelezo cha namna gani anavyokubalika mbele ya wajumbe wa Mkutano Mkuu na kubwa zaidi ni kwamba wana imani naye.
Wamemwomba Rais apange ratiba ya kuvitembelea vyuo vikuu na kuzungumza na wanafunzi ili nao wapate wasaa mzuri wa kumpongeza. Wamemhakikishia kwamba wataendelea kuwahimiza wanafunzi wa elimu ya juu kujiunga na CCM, na kwamba zile fikra kwamba kuna upinzani dhidi ya CCM katika vyuo vikuu si sahihi.
Akizungumza na wanafunzi hao baada ya kuwakabidhi kadi zao, Rais alisema amefurahishwa sana na idadi kubwa ya wanafunzi wa vyuo vikuu kutoka Dodoma na Morogoro ambao wameamua kwa hiari yao kujiunga na Chama Cha Mapinduzi.
Akawaeleza kuwa Chama kina mkakati maalum kwa kuwavutia wasomi wengi kujiunga na CCM na kwamba hiyo ni njia bora na sahihi ya kuwaandaa viongozi katika ngazi mbalimbali za serikalini na katika Chama.
"Nimefurahi sana kwa kweli, kwa sababu chama lazima kipate wasomi, na nchi haiwezi kuendelea bila ya wasomi, na duniani hakuna nchi ambayo imeendelea kwa kuwa na watu mbumbumbu. Na ndio maana tulipoingia serikalini tulitoa umuhimu wa pekee katika elimu" akasema Kikwete.
Amewahakikishia wanafunzi hao kwamba, Serikali ya Chama Cha Mapinduzi imejiwekea mkakati maalum wa kuwaajiri wanafunzi waliohitimu chuo kikuu kuanzia ngazi ya tarafa.
Akawaeleza kuwa wasisite kwenda kufanya kazi katika tarafa kwani huko ndio kunakowafungulia uzoefu na fursa ya kupanda katika safu za uongozi ziwe za ukatibu tawala, ukuu wa wilaya, ukuu wa mikoa na nafasi nyingine nyingi.
"Tunamkakati maalum wa kuwaajiri wanafunzi, na mwaka huu tunaanza na wanafunzi wapatao 500 kutoka SUA, na ninapenda niwahakikishie kwamba vijana wasomo ambao tumewaajiri katika nafasi ya ukuu wa wilaya 12 kati yao wanafanya vizuri sana, hii inaonyesha umuhimu wa kuwaajiri wasomi" akasisitiza Rais.
Akizungumzia kuhusu suala la mikopo ya wanafunzi, Rais amewaahidi wanafunzi hao, kwamba kabla ya kuondoka mkoani Dodoma atahakikisha anakutana na Waziri wa Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu na Mwenyekiti wa Bodi ya Mikopo na kuangalia matatizo yaliyojitokeza ili kuyapatia ufumbuzi.
"Nataka niwahakikishie kwamba kabla sijaondoka hapa Dodoma nitakutana na Waziri na Mwenyekiti wa Bodi na kuangalia wapi pana tatizo na kulitafutia ufumbuzi, maana suala hili la mikopo limeingiliwa na watu wengi wakiwamo wanasiasa, lakini hatima yake anayeathirika ni mwanafunzi" akasema Rais na kushangiliwa na wanfunzi hao.
Amewaeleza kuwa Serikali inaandaa utaratibu wa kuboresha njia za mawasiliano kati ya Bodi ya Mikopo na wanafunzi wa vyuo vikuu.
Rais Kikwete pia alitumia fursa hiyo kuwaeleza wanafunzi hao juhudi na mikakati mbalimbali inayofanywa na Serikali katika uboreshaji na upanuzi wa elimu nchini kuanzia elimu ya awali hadi chuo kikuu na kwamba imejipanga vema kukabiliana na changamoto mbalimbali.
Kuhusu ombi la kutembelea vyuo vikuu, Rais ameahidi kupanga utaratibu na kwa kuanzia atakitembelea chuo kikuu cha Dodoma kabla hajaondoka.
Awali Katibu Mkuu wa CCM Yusufu Makamba aliwataka wanachama hao wapya kila mmoja wao kushawishi wanachama wapya watano kujiunga na Chama Cha Mapinduzi.
Source: Subirini Magazeti ya Kesho.