Elections 2010 Wanafunzi wa vyuo vikuu mtaji kwa chadema.

kinepi_nepi

JF-Expert Member
Aug 16, 2007
869
235
Baada ya serikali ya CCM kufikiri kutowarudisha vyuoni wanafunzi wa vyuo vikuu inawakomoa wogombea wa vyama vya upinzani, imejikuta kwenye wakati mgumu baada ya kutawanya wapiga debe wa mageuzi Tanzania nzima bila kujijua.

Ilikuwa ni vigumu sana kumfikia kila mtu kule kijijini, ila baada ya serikali kuwanyima haki ya msingi wanafunzi hawa moja na muhimu ni ya masomo yao, na ya pili ni ile ya kura. Wanafunzi walio zaidi ya 60000 waliotawanyika Tanzania nzima hasa vijijini wanatoa elimu ya urai na kuonyesha ubaya wa serikali ya CCM na kuhamasisha base zote za wapenda demokrasia na mageuzi ya kiutawala.

Vyama vya upinzani sasa vinatakiwa kuwatumia wanafunzi hawa Kulinda na kusimamia kura, Kuwa Mawakala wa vyama vya upinzani. Kwa hali ilivyo sasa wanafunzi wengi wanaweza kuwa waaminifu, wakiwa ni taifa la sasa la wasomi wanaelewa wazi elfu 20 ya rushwa ili kusaini uongo haiwezi kumpa ajira wala kumsomesha.

Wanafunzi mlio mitaana tumieni elimu yenu kwa faida yenu na kizazi chetu kijacho. Kumbuka mizwengwe ya vyuo imeanza tokea enzi za kale, matokeo yake ni kuzalisha vilaza, wanaoshindwa kupambana na dunia ya sasa.

Shule zikifunguliwa utasikia CRUSH Program ili tuweze kumaliza kwa sababu ya muda. Kazini hakuna Crush Program, kampuni za uzalishaji za ukweli zinataka matokeo swala la kwamba mtaala haukufuatwa kwa sababu ya serikali hakuna atakayesikia wala kujua. Tulinde vizazi vyetu vijavyo viepuke hii adha.
 
Kama ulikuwapo kichwani mwangu. Leo nilikuwa vijiji vya Sumve kuhamasisha. Nimewakuta ccm na watu sijui wa wapi wale. Imekula kwao mwaka huu.
 
wanafunzi 60,000; katika kila kata hapakosekani mwnfnz mmoja, naamini kwa mazingira ya sasa kila mwnfnz hakosi kilongalonga (simu), inabidi ku'design msg na isambazwe kwa kila mwnfnz ili asifadhaike kwa kutopiga kura, akumbushwe ili ajue wajibu wake ktk kuielimisha jamii kuhusu uchaguzi ujao, afaham kuwa nafasi yake huko alipo ni muhimu zaidi kuliko kura yake moja. Huu ni mwaka wa ukombozi coz for the first time uchaguzi unafanyika wanachuo wakiwa nyumbani.
 
kwa hesabu za fasta fasta kati ya wanfnz 60,000 lazima 40,000 au 50,000 ni wanaopenda mabadiliko, nimetoa hao 20,000 au 10,000 ambao huenda wanafaidika na mfumo wa kifisadi au ........ hao 40 au 50 waliobaki kila mmoja akishawishi wapiga kura 50 wachague CHADEMA nina uhakika katika hao 50 walioshawishiwa nao kila mmoja atashawishi wakwake. USHINDI UPO CHADEMA.
 
Mimi nahamasisha sana huku Tabora, machinga wengi nimewashawishi na kuwapa elimu hadi wameamua kuandaa kadi zao tayari tayari. Mwaka huu mwisho wa mafisadi.
 
Hata wawakilishi wa kusimamia uhesabuji wa kura sasa wamepatikana kiurahisi. Mahesabu yao yamekwama
 
Back
Top Bottom