Wanafunzi wa vyuo hulipwa kulingana na siku za masomo na si vinginevyo!

Konseli Mkuu Andrew

JF-Expert Member
May 10, 2013
740
855
Mimi pia ni mnufaika wa mkopo wa Elimu ya juu unaotolewa na serikali.Nimeona kumekuwa na minong'ono mingi na kuna kipande cha video kikitembea kikionesha baadhi ya wanafunzi wakiandamana kuhusu kukatwa pesa ya kujikimu kutoka Laki tano na ushirini 520000/= mpaka laki tatu na tisini na moja 391000/=.

Kinachonishangaza minong'ono imekuwa mingi tena ya chini chini kuliko vitendo.Tujikumbushe mkataba tuliosaini na bodi ya mikopo Kuna kipengele kinasema 'Utalipwa kutokana na idadi ya siku utakazo kaa chuo" ambapo mwanafunzi wa chuo kikuu kwa siku anapata 8500/=.

Sasa jiulize hii semester unakaa siku ngap mpaka kuelekea kwenye UE? alafu piga mahesabu ukiona hiyo laki tatu inaendana na siku utakazo kuwa chuo basi kaa chini tulia na ukiona haindani basi tafuta mamlaka husika na wakufafanulie Ila ukijifanya mzee wa maandamano utapoteza chuo na Kama unavyojua wengi tunatoka familia duni Sana hivyo kufukuzwa chuo kutaenda kuwaumiza wazazi wetu.
 
Mkuu Hakuna kipengele kinamhusu mnufaika kulipwa kulingana na idadi ya siku alizokaa chuo. Labda umejichanganya kwenye sharti la kipengele Cha 2.3 Kinachosema

"... bodi itaendelea kutoa mkopo kwa muda wa kawaida wa masomo (normal course duration) Hadi mwanafunzi atakapomaliza masomo yake... "

Hapo inamaa kwamba Kama kozi unayosoma ni ya miaka minne, maana yake mkopo utapokea kwa miaka 4, hivyo ukifeli baadhi ya modules ukalazimika kuzirudia mwaka wa 5, bodi haitahusika kukulipia kwa sababu normal course duration yako Ni miaka 4
 
Mkuu Hakuna kipengele kinamhusu mnufaika kulipwa kulingana na idadi ya siku alizokaa chuo. Labda umejichanganya kwenye sharti la kipengele Cha 2.3 Kinachosema

"... bodi itaendelea kutoa mkopo kwa muda wa kawaida wa masomo (normal course duration) Hadi mwanafunzi atakapomaliza masomo yake... "

Hapo inamaa kwamba Kama kozi unayosoma ni ya miaka minne, maana yake mkopo utapokea kwa miaka 4, hivyo ukifeli baadhi ya modules ukalazimika kuzirudia mwaka wa 5, bodi haitahusika kukulipia kwa sababu normal course duration yako Ni miaka 4



Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
Ila mkuu navyofahamu ni kuwa kila course Ina mwaka mmoja mbele.Nina jamaa yangu alirudia mwaka Ila akaendelea kupata mkopo,course yake ilikuwa ni 3years Ila akalipwa miaka minne na ule mwaka wa kurudia.


Pia kuhusu kulipa kutokana na siku utakazo kaa chuo ngoja nipitie mkataba alafu nije na majibu Mkuu.
 
Back
Top Bottom