Influenza
JF-Expert Member
- Jul 1, 2018
- 1,445
- 3,403
Mkutano wa 20 wa wakuu wa nchi za Afrika Mashariki umeanza leo asubuhi Ijumaa Februari Mosi, 2019 kujadili masuala mbalimbali.
Viongozi wakuu waliopo katika mkutano huo unaofanyika jijini Arusha, Tanzania ni Rais wa Tanzania, John Magufuli; Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta; Yoweri Museveni wa Uganda na Paul Kagame wa Rwanda.
Katika mkutano huo Rais wa Burundi, Pierre Nkurunzinza anawakilishwa na makamu wa kwanza wa Rais, Gaston Sindimwo huku Rais wa Sudan Kusini akiwakilishwa na Waziri wa Biashara, Paul Mayon.
Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika ya Mashariki imeeleza kikao wakuu hao wameanza na kikao cha ndani na saa 8 mchana watafanya mkutano mkuu.
Kwa mujibu wa ratiba hiyo miongoni mwa ajenda za mkutano huo ni kuidhinisha Kenya kugombea uanachama wa baraza la usalama la Umoja wa Mataifa katika kipindi cha mwaka 2021-2022.
Ajenda nyingine ni kupata taarifa ya mchakato wa Somalia kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki na kupata taarifa ya itifaki ya masuala ya umoja wa forodha.
Wakuu hao wa nchi pia wanatarajia kujadiliana juu ya mchakato wa shirikisho la kisiasa la Afrika ya Mashariki na taarifa mbalimbali za fedha na utendaji wa Sekretarieti.
UPDATES
Jaji Sauda Mjasiri ameapishwa leo Februari 01 2019 katika Mkutano wa 20 wa Wakuu wa Nchi Jumuiya ya Afrika Mashariki
Jaji Msafiri anakuwa Mwanamke wa pili kuteuliwa katika nafasi hiyo na atatumikia nafasi hiyo kwa miaka mitano akichukua nafasi ya Jaji Fakihi Jundu
Aidha, Wanafunzi wawili kutoka Tanzania wamefanya vizuri katika Shindano la uandishi wa insha katika ngazi ya kanda ya Afrika Mashariki
Michael Nyaruga kutoka Kibaha sekondari ameibuka kidedea kwa mwaka 2017 huku Innocent Shirima kutoka Moshi sekondari akiibuka kidedea kwa mwaka 2018
Sent using Jamii Forums mobile app
Viongozi wakuu waliopo katika mkutano huo unaofanyika jijini Arusha, Tanzania ni Rais wa Tanzania, John Magufuli; Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta; Yoweri Museveni wa Uganda na Paul Kagame wa Rwanda.
Katika mkutano huo Rais wa Burundi, Pierre Nkurunzinza anawakilishwa na makamu wa kwanza wa Rais, Gaston Sindimwo huku Rais wa Sudan Kusini akiwakilishwa na Waziri wa Biashara, Paul Mayon.
Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika ya Mashariki imeeleza kikao wakuu hao wameanza na kikao cha ndani na saa 8 mchana watafanya mkutano mkuu.
Kwa mujibu wa ratiba hiyo miongoni mwa ajenda za mkutano huo ni kuidhinisha Kenya kugombea uanachama wa baraza la usalama la Umoja wa Mataifa katika kipindi cha mwaka 2021-2022.
Ajenda nyingine ni kupata taarifa ya mchakato wa Somalia kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki na kupata taarifa ya itifaki ya masuala ya umoja wa forodha.
Wakuu hao wa nchi pia wanatarajia kujadiliana juu ya mchakato wa shirikisho la kisiasa la Afrika ya Mashariki na taarifa mbalimbali za fedha na utendaji wa Sekretarieti.
UPDATES
Jaji Sauda Mjasiri ameapishwa leo Februari 01 2019 katika Mkutano wa 20 wa Wakuu wa Nchi Jumuiya ya Afrika Mashariki
Jaji Msafiri anakuwa Mwanamke wa pili kuteuliwa katika nafasi hiyo na atatumikia nafasi hiyo kwa miaka mitano akichukua nafasi ya Jaji Fakihi Jundu
Aidha, Wanafunzi wawili kutoka Tanzania wamefanya vizuri katika Shindano la uandishi wa insha katika ngazi ya kanda ya Afrika Mashariki
Michael Nyaruga kutoka Kibaha sekondari ameibuka kidedea kwa mwaka 2017 huku Innocent Shirima kutoka Moshi sekondari akiibuka kidedea kwa mwaka 2018
Sent using Jamii Forums mobile app