Wanafunzi wa Sekondari kuchujwa kwa mtihani kabla ya kupanda kidato

Hahaaaa hii nchi bwana, kila anayeingia anakuja na tamko lake la nitoke vipi..... Mara hakuna "average" mara ipo.......
 
Mkakati wowote ambao unaweza kupata angalau nafasi ya kufanikiwa, lazima uanze na walimu. maslahi yao, makazi yao, mafao yao. hilo la kwanza. vyoo bora, madawati na vyumba vya madarasa vifuatie, maktaba na maabara pia. lakini kwanza mwalimu. maana hata chini ya mti, mwalimu aliyehamasika atapiga kazi na atafanikisha kwa kiwango kikubwa tu. lakini hata uweke kila mwanafunzi awe na laptop, kama mwalimu hana morali ni kazi bure tu. Ni "kujilisha upepo". hayo maagizo hayana maana yoyote. Ni UMAGUFULI na UMAKONDA katika ubora wake.
Mindi ulichoongea ni cha ukweli, maslahi yanamfanya mtu afanye kazi kwa bidii na kujitoa lakini si kama hali ilivyo sasa na sio kwa walimu tuu hata kwa wafanyakazi wa sector nyingine hakuna mwenye hari ya kujitoa kufanya kazi wakati nyumbani hakueleweki!!
Hakuna mwenye hamu ya kufanya kazi wakati anajua hakuna chochote mpaka mwisho mwezi ambapo hata huo mwisho wa mwezi ana kamshahara kanakatwa kwenye mkopo.
Hata waliokuwa wanajitolea kufanya kazi Jmosi sasa hakuna anayetaka anaona bora apambane na hali yake kwenye vitu vingine vitakavyomuingizia hela.
Kwahyo wanapotoa matamko yao wafikirie na hao walimu au wafanyakazi kuwaongezea au kuboresha maslahi yao la sivyo itakuwa mambo ya Passive Resistance ya kugeuza miche au kuchemsha mbegu zisiote na mwisho wa siku hakuna kinachoendelea.
 
Naona lengo kubwa hapa si kuboresha elimu Bali ni kushindana na shule za binafsi! Kwa mkakati huo ataonekana ameshinda! Maana divisheni 1 zote ambazo zingepatikana Minaki na Pugu zinahamishiwa Kibaha sekondari! Na divisheni 2, 3, na 4 ambazo zingeonekana kibaha sekondari zinahamishiwa kilangalanga! Kwa maana hiyo matokeo yataonyesha wanafunzi wote wa kibaha wamepata divisheni 1, hali kadhalika Mzumbe, Ilboru, Tabora boys & girls, Kilakala na Msalato!
Sasa kwa utaratibu huo ndo tutakuwa tumeboresha elimu au? Idadi ya divisheni 1 itabaki ile ile isipokuwa zitaonekana kwenye special school tu! Idadi ya divisheni 4 na 0 siyo kwamba itapungua ila itaonekana kwa shule za kata tu! What a mess!
Ni sawa na MTU aliyekuwa na noti 4 za msimbazi (10,000/=), na noti 8 za jero jero (500/=). Mwanzoni mfuko wake wa kulia ulikuwa na noti 3 za msimbazi na 2 za jero, wakati mfuko wake wa kulia ulikuwa na noti 1 ya msimbazi na 6 za jero. Sasa akaamua kuhamishia misimbazi yote kwenye mfuko wa kulia na jero jero zote mfuko wa kushoto! Kwa hiyo akitoa pesa zake za mfuko wa kulia ni misimbazi mtupu! Je hapo ameongeza kipato? Je hapo anastahili pongezi? Hicho ndicho kilichopangwa kufanyika! Nitashangaa sana kama tamko lake halitatenguliwa kama lile la mheshimiwa fulani aliyetaka ili usajili ndoa ni lazima uwe na cheti cha kuzaliwa! Yetu macho!
 
Mindi ulichoongea ni cha ukweli, maslahi yanamfanya mtu afanye kazi kwa bidii na kujitoa lakini si kama hali ilivyo sasa na sio kwa walimu tuu hata kwa wafanyakazi wa sector nyingine hakuna mwenye hari ya kujitoa kufanya kazi wakati nyumbani hakueleweki!!
Hakuna mwenye hamu ya kufanya kazi wakati anajua hakuna chochote mpaka mwisho mwezi ambapo hata huo mwisho wa mwezi ana kamshahara kanakatwa kwenye mkopo.
Hata waliokuwa wanajitolea kufanya kazi Jmosi sasa hakuna anayetaka anaona bora apambane na hali yake kwenye vitu vingine vitakavyomuingizia hela.
Kwahyo wanapotoa matamko yao wafikirie na hao walimu au wafanyakazi kuwaongezea au kuboresha maslahi yao la sivyo itakuwa mambo ya Passive Resistance ya kugeuza miche au kuchemsha mbegu zisiote na mwisho wa siku hakuna kinachoendelea.
Kweli kabisa Shyshii, niliongelea walimu kwa sababu naona Magu amekomaa na "elimu bure" na "madawati" akahesabu kwamba ameshamalizana na sekta ya elimu. kumbe kuna mambo kibao, na pia vipaumbele vyake siyo sahihi. Madawati yamemwagwa kama njugu, matokeo yake hakuna hata vyumba vya kuyawekea. hapo unajiuliza kama si bora wangeanza na vyumba kwanza? maana mkakati wa Maji walianza kuboresha mabomba ili maji yakiongezeka yawe na mahali pa kupita!!

kwa ujumla suala la "Manpower development and maintenance" ni kitu ambacho kwenye akili ya Magu hakipo kabisaaaa. yeye anawaza kuboma majumba na kujenga barabara tu. anachofanya kwa wafanyakazi ni udhibiti, upelelezi uliopitiliza mpaka unaweza kusema ni kupiga chabo, kuwapekua pekua wafanyakazi kutafuta vyeti feki, na sasa umri feki. sawa, hayo ni muhimu, lakini si uboreshaji ungeenda sambamba? matokeo kama unavyosema, kuna very high demoralisation kila sehemu. na sasa anatoa tamko "sipandishi mishahara" watu wakianza kujadili hoja, anakuja juu watu wamemnukuu vibaya, ebo!!!
 
Ndalichako alipiga marufuku sekondari za private kufanya hiyo michujo!!!!! This Government!!
 
Back
Top Bottom