Wanafunzi wa kitanzania wapitao Urusi kutokea Sumy, Ukraine

Hili ni tatizo halikupaswa kutokea hata kidogo, ni uzembe tu wa nchi za Afrika.

Nchi za Magharibi ikiwemo USA, Australia, Canada zilitoa angalizo kwa Raia kuondoka wiki kadhaa kufuatia taarifa za kiintelejensia. Marekani ilitaarifa kila hatua kiasi kwamba viongozi wa Ukraine walitilia mashaka, leo imedhihirika ni kweli.

Tanzania haikufanya juhudi za kuondoa Raia mapema bali kuwataka watulie na wafuatae maagizo ya maeneo wanayoishi, maeneo tarajiwa ya vita.
Hili lilikuwa jambo la kusikitisha na kuhuzunisha

Yametoke yaliyotokea, tunaposikia hakuna escort, kama ni kweli, kuna maswali ya kujiuliza

Kama Taifa tubadilike, intelejensia za kubaini vibaka na Wapinzani na mabango hazitusaidii katika dunia ya leo inayokwenda kasi.

Tunatumia akili nyingi kwa mambo yasiyo na maana, yanapotokea ya kutumia akili, ima hatuwezi au tumechoka.

Kwa hili, uongozi wa utakwepaje lawama?

JokaKuu Pascal Mayalla
Huu sio muda wake,zaidi yakulalamika hujashauri chochote ni kwa namna gani wanafunzi watarudi nyumbani salama.Haya malalamiko hayana msaada wowote kwa sasa
 
Huu sio muda wake,zaidi yakulalamika hujashauri chochote ni kwa namna gani wanafunzi watarudi nyumbani salama.Haya malalamiko hayana msaada wowote kwa sasa
Ile ni traumatic situation. Muhimu tu wawe na equanimity.
Equanimity maana yake wasiwe na woga pia wasiwe na confidence.
 
Mnakumbuka moja ya njia ambayo tulikuwa tukiishauri Serikali ya Tanzania juu ya wanafunzi wa Tanzania waliokwama nchini Ukraine katika mji wa Sumy, ni Serikali kupitia Balozi zetu kufanya mazungumzo na Serikali ya Urusi ili kuruhusu wanafunzi wapitie nchi ya Urusi kutokea Sumy, Ukraine.

Kwasababu Mji wa Sumy,Ukraine upo mbali sana hadi kufika Mpakani Poland, Romania na Hungari ambapo watu wengi hukimbilia huko kupata hifadhi. Mji wa Sumy umepakana kabisa na nchi ya Urusi hivyo mapendekezo yalikuwa wanafunzi wa Sumy, hasa Sumy State University-Ukraine wapitie Urusi kwani ndio karibu kuliko kwenda Poland,Hungari na Romania ambapo ni mbali na njia si salama kutokea Sumy.

Serikali ya Tanzania kupitia Balozi zetu nchini Urusi(Moscow) na Stockholm (Sweden) zikafanya mazungumzo na Serikali ya Urusi, hivyo Serikali ya Urusi ikakubali kutengeneza njia salama yaani Safe Passage/Safe Corridor kwa ajili ya wanafunzi wanaotokea Sumy. Hivyo wanafunzi wameombwa kuondoka kuanzia leo tar 5/Machi/2022 wakiwa na Bendera za Tanzania kuelekea eneo la Urusi liitwalo Sudzha (Sudja) na watakapofika hapo watapokelewa na Jeshi la Urusi na kupelekwa hadi eneo la Belgorod ambapo watapokelewa na mafisa wa Balozi ya Tanzania.

Hii ni habari njema ila bado kuna changamoto kadhaa ambazo zimefanya wanafunzi wa Tanzania hadi sasa kutoanza safari. Mwanzo tulijua kuna usafiri na Escort kutoka Sumy, Ukraine hadi eneo la Sudzha -Urusi ila baada ya kufuatilia tumegundua ya kwamba hakuna Usafiri wala Escort ya kuwasindikiza wanafunzi hawa kutoka Sumy, Ukraine hadi Sudzha-Urusi jambo ambalo ni hatari sana kwa watanzania wenzetu hawa.

Kutoka Sumy, Ukraine hadi Sudja(Sudzha) Urusi ni Kilometa 67 ,kwa Mguu ni mwendo wa masaa 12 . Kwa taarifa ni kwamba Chuo kimejitenga kuwasindikiza hao wanafunzi ,hakuna usafiri wowote na hawana Escort yeyote ile kutokea Sumy kufika huko Sudzha -Urusi ambapo ndio watapokelewa na wanajeshi wa Urusi.

Serikali tunaomba mliangalie hili,hii ni vita kwani sio salama kabisa. Mwendo wa masaa 12 kwa mguu bila Escort wala usafiri ni hatari.Wanaweza shambuliwa njiani na jeshi lolote ili kusingizia Jeshi la nchi fulani ndio limeuwa Raia (civilians),wanaweza shambuliwa na Urusi ili kusingizia Ukraine,na wanaweza shambuliwa na Ukraine ili kusingizia Urusi.

Ushauri na Mapendekezo.

Serikali ya Tanzania kupitia Balozi yetu Stockholm iombe Serikali ya Ukraine kutoa Escort kupitia Jeshi la Ukraine kwa hawa wanafunzi kutokea Sumy, Ukraine hadi Sudja (Sudzha) au Red Cross itoe Escort kwa hawa wanafunzi kutoka Sumy, Ukraine hadi eneo la Sudja (Sudzha) Urusi au Pia Serikali ya Tanzania kupitia Ubalozi wetu wa Moscow (Urusi) uzungumze na Serikali ya Urusi na Red Cross ili Red Cross kutoka Urusi iwafuate hawa wanafunzi kutoka Sumy, Ukraine hadi eneo la Sudja (Sudzha) kuliko kuwaacha peke yao kwa mguu kutembea kwa masaa 12.

Abdul Nondo.

Mwenyekiiti wa Ngome ya Vijana Taifa- ACT wazalendo.

5/Machi/2022.
Serikali imefanya jitihada kubwa hata kabla hamjaja na ushauri wenu wa michongo. Tuache siasa uchwara kwenye mambo ya msingi. Tuache hatua zinazofanyika zifike tamati kwani wanafunzi wameanza kuwasili moscow ili wavuke kupitia mataifa jirani kama Helsinki, Sweeden au German
 
Back
Top Bottom