Wanafunzi wa Diploma mliodhulumiwa fedha zenu fungueni kesi mahakamani dhidi ya TCU

herikipaji

JF-Expert Member
Aug 23, 2016
1,198
1,345
Wasalaamu wanajukwaa!

Hivi karibuni Tanzania Commission for Universities - TCU ilibadilisha kwa kupanga upya viwango, vigezo na sifa vya udahili wa wanafunzi kujiunga na vyuo vikuu kwa upande wa wahitimu wa Diploma na wale walohitimu kidato cha sita au Form six.

Viwango hivyo vipya vimebadilishwa gafla na TCU na kutaka vitumike tena kipindi ambacho wanafunzi tajwa hapo juu wamekwisha fanya mitihani yao ya mwisho na wanasubiria matokeo.
Wanafunzi wengine wengi tuu walikwisha fanya application HESLB na kulipia ada ya udahili wakitumia viwango vya awali hawa wamedhulumiwa fedha yao.

Wanafunzi wote waloathiriwa kwa namna yoyote ile kimwili na kisaokolojia kwa uamuzi huo wa TCU kubadilisha viwango vya udahili kwa haraka ni muda sasa kufungua kesi mahakamani dhidi ya TCU kwa kufanya dhulma ya fedha za wanafunzi waliokwisha fanya application.
Ni wakati sasa kudai na kuitafuta HAKI yao mahakamani sababu TCU wamefanya uzembe na dhulma kwa wanafunzi hawa hivyo yafaa waburuzwe mahakamani na kuwajibishwa kwa uzembe huo ulosababishwa usumbufu na matatizo makubwa kwa wanafunzi.

TCU wawajibike kwa hili na inapaswa walipe kwa kurudisha zile fedha na gharama nyingine zote zilizotumiwa na wanafunzi wakifanya application pamoja na muda walotumia.

Hilo likifanyika itakuwa ni fundisho kwa TCU na taasisi nyingine zinazoendesha Elimu ya juu kuacha kufanya maamuzi ya haraka kwa kukurupuka na kuwaumiza wanafunzi.

Tunahitaji Elimu bora na haitopatikana kwa kuhangaika na vitu visivyo na maana kama kubadilisha viwango vya kujiunga na elimu ya juu sababu tatizo la elimu ya Tanzania ni mfumo mzima wa elimu kuwa mbovu kuanzia Primary level to High education pamoja na mitaala inahitaji kufanyiwa marekebisho ili iendane na high rate of growing science and technology in the world.

Sababu walizotoa TCU kubadilisha hivi viwango ni kuwa wahitimu wa vyuo vikuu kutokuwa na ubora unskilled na kukosa creativity inapelekea waajiri kulalamika.
Hili tatizo naomba TCU inayoongozwa na wasomi waliotukuka wafahamu haiwezi kutatuliwa kwa kubadilisha viwango vya kujiunga na vyuo vikuu sababu wahitimu kukosa competence kwenye soko la ajira halisababishwi na viwango kuwa vidogo kujiunga chuo kikuu.

Wadau wa elimu tunataka mshughulikie matatizo makubwa yanayoendelea kuua elimu yetu kufanya iwe bora na yenye kuleta tija kwa jamii na taifa sio kufanya maamuzi ya hovyo yanayozidi kuua Elimu.

Maamuzi haya mabaya mfahamu kuwa yanazidi kutupeleka gizani tunahitaji ELIMU BORA itayokuwa mwanga kwa jamii ya watanzania.
 
Je,ni WANGAPI wanaofikiri kama WEWE..!?
Ukipata JIBU la SWALI langu utajua kama ULICHOKIANDIKA kinawezekana au ni NDOTO..!
 
Je,ni WANGAPI wanaofikiri kama WEWE..!?
Ukipata JIBU la SWALI langu utajua kama ULICHOKIANDIKA kinawezekana au ni NDOTO..!
wengi waliokumbwa na kadhia hii wanalalamika tu wasijue nini cha kufanya, mie nimetoa ushauri ili kusaidia katika kutafuta haki yao kwanini unafikiri haiezekani?
 
Kwa sababu ya WOGA na KUTOJIAMINI..!
Ni kweli ndugu vijana wengi wamejawa na woga, hofu na hawajiamini na hata kuhoji haki zao zinapovunjwa hawawezi. Katika kudai HAKI hupaswi kuwa muoga, woga hausaidii kitu.

Hii ndio sababu ya watoa maamuzi ya mambo muhimu kama hilo la elimu kuamua kufanya watakavyo, wanajua hata maamuzi wanayofanya yakiwa mabaya na yataumiza wengi hamna atakayeweza kupinga kwa kuchukua hatua kali za kisheria dhidi yao.

Wasipopingwa wataendelea kufanya maamuzi mabaya zaidi na zaidi yanayoumiza na kuharibu ndoto za vijana wengi.
 
Only happens in Tanzania, ukitaka haki utapigwa mabomu mkapa ukimbie. anyway wamezee mate tu wengine twende chuo kikuu kwasababu wemeichagua CCM wenyewe bila kulazimishwa. Na kale ka wimbo nakapenda kanasema hivi "TUMEJIPANGA MWAKA HUU WATAISOMA" acha tuisome namba ni heri mm nilichagua upinzani lakini nilisoma kwa jihudi zangu zote. Mchana mwema
 
Only happens in Tanzania, ukitaka haki utapigwa mabomu mkapa ukimbie. anyway wamezee mate tu wengine twende chuo kikuu kwasababu wemeichagua CCM wenyewe bila kulazimishwa. Na kale ka wimbo nakapenda kanasema hivi "TUMEJIPANGA MWAKA HUU WATAISOMA" acha tuisome namba ni heri mm nilichagua upinzani lakini nilisoma kwa jihudi zangu zote. Mchana mwema

Elimu inafanyiwa makidamakida na majaribio wakati wote tena sio first priority kwa serikali tutarajie madudu zaidi na zaidi.
 
wahanga tupo wengi mm nilifanya application kupitia nacte Mwezi wa Tano kabla hawajaweka vigezo vipya ilikiwa gpa ya 2.7 sasa hatujajua hatma yetu tutapata chuo au la na kama hatutopata pesa zetu zirudishwe maana hii nchi inafanya mambo yake kwa KIKI ni vyema tukafanya maisha mengine tuu diploma itanitosha..
 
Hata mimi ni muhanga niko mkoani ila tunaweza kupata wawakilishi kwa hapo dar na ikiwa ni pamoja na mawakili kwa pamoja tukatoa michango yetu ikiwa recorded na kufungua kesi.
Wahanga ni wengi mnooo....tuko tayari na kuna magroup mengi ya vijana waathirika... mwanzilishi wa wazo hili nakuomba ujitolee tena kuanzisha group la whatsapp. Kwa upande wangu nina kundi kubwa hasa la waliosoma engineering na tukaathiliwa na vigezo vipya.
 
wahanga tupo wengi mm nilifanya application kupitia nacte Mwezi wa Tano kabla hawajaweka vigezo vipya ilikiwa gpa ya 2.7 sasa hatujajua hatma yetu tutapata chuo au la na kama hatutopata pesa zetu zirudishwe maana hii nchi inafanya mambo yake kwa KIKI ni vyema tukafanya maisha mengine tuu diploma itanitosha..
Hata mimi ni muhanga niko mkoani ila tunaweza kupata wawakilishi kwa hapo dar na ikiwa ni pamoja na mawakili kwa pamoja tukatoa michango yetu ikiwa recorded na kufungua kesi.
Wahanga ni wengi mnooo....tuko tayari na kuna magroup mengi ya vijana waathirika... mwanzilishi wa wazo hili nakuomba ujitolee tena kuanzisha group la whatsapp. Kwa upande wangu nina kundi kubwa hasa la waliosoma engineering na tukaathiliwa na vigezo vipya.

Ni wakati sasa tuamue kuchukua hatua ili kufahamu hatima yetu mie naomba kwa pamoja tuungane hata wale waliofikisha GPA 3.5+ tushirikiane leo mie kesho wewe.

Leo uamuzi huu kama haujakugusa maamuzi ya hovyo yahusuyo elimu hii yanaendelea kutolewa hivyo siku uamuzi mbaya zaidi utatolewa na utaumia.

Haya matatizo tuone ni yetu sote, kama mdau hapo juu alivyopendekeza tuanzishe group la whatsapp kufanikisha hili mnaeza kunipa namba zenu wadau.
 
Kikubwa tuungane tufanye mawasiliano na nacte.. ili watupe neno la mwisho ndipo tuchukue uamuzi mwingine... maana baada ya vigezo vipya nacte na loan board waliochukua pesa zetu wako kimya sana. Huu ni utapeli wa kiwango cha juu.
 
Kikubwa tuungane tufanye mawasiliano na nacte.. ili watupe neno la mwisho ndipo tuchukue uamuzi mwingine... maana baada ya vigezo vipya nacte na loan board waliochukua pesa zetu wako kimya sana. Huu ni utapeli wa kiwango cha juu.
Kweli neno watalolitoa litatusaidia tuchukue hatua ipi.

Ni vema tufanye organization tuanzie huko nacte walioko Dar support mie npo hapa Dar.
 
Tatizo kesi kama hizi mahakamani zitawacost sana kuliko pesa yenyewe waliyotumia kufanya application, na ikitokea TCU wameshinda then loss inakua imeongezeka, kuendesha kesi ingekua bure sidhani kama wanafunzi wote wangechukulia poa. Watu ni vizuri wajifunze kudai haki zao, ni jambo la muhimu sana hasa nchi kama Tanzania ambayo watu wanajiamulia kiholela mahakama ndiyo inabaki kua mkombozi wetu.
 
Hilo tangazo wametoa lini?Tunachohitaji kutoka kwao sio fedha pekee.
Fedha kama watarudisha vipi kuhusu hatima ya wenye point pungufu tunapigania mustakabali wa maisha yetu.

GPA 3.499 kushuka chini wanaenda wapi sababu hii sio failure.
 
Back
Top Bottom