Wanafunzi wa Chuo cha Ualimu Moshi waandamana kupinga utapeli wa ada zao

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,395
EEAY7YVWsAAsyxE.jpg

EEAY7YYXsAAd3ie.jpg

EEAY7YTWwAEaicU.jpg

WANAFUNZI zaidi ya 400 wa Chuo cha Ualimu Moshi zamani Mong'are kilichopo Wilaya ya Hai, mkoani Kilimanjaro wamefunga barabara na kuzuia shughuli nyingine za usafirishaji wakishinikiza serikali kuingilia kati sakata la utapeli wa zaidi ya Sh.milioni 75 za malipo ya ada.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro limeingilia kati maandamano hayo na kuwakamata wanafunzi waliokuwa wanaandamana kudai kulipwa zaidi ya Shilingi milioni 75 malipo ya ada wanazidai kutapeliwa na uongozi wa chuo.

EEAd_uMXkAA1R2D.jpg
EEAeARQWkAABkiJ.jpg
 
Hivi polisi hawanaga akili za kupima madai ya waandamaji?
Kwanini wasingewaita kwa kipaza sauti, wawasikilize na kuwashauri watulie ili madai yao yafikishwe panspohusika?
Unapomkamata mwanafunzi asiyekuwa na madhara ni kumjengea hofu
 
Wanazuia shughuri nyingine kwa watumia barabara. Hebu jenga picha unamgonjwa kabebwa na gari la wagonjwa na likasimama kisa wanachuo wameandamana utajifikiria je. Vipi kama kuna moto na gari la zimamoto likashindwa kupita kwenda kwenye tukio itakuwaje. Nawajua polisi wa tanzania ila kwa mengine wako sahihi.
Polisi sasa badala ya kuwalinda waandamanaji wao wanawatawanya.
 
Usikubali kutapeliwa, usitume pesa kwa mtu usiyemfahamu. Hakiki ujumbe na simu inayokutaka utume pesa. JESHI LA POLISI LINAZINGATIA USALAMA WA PESA ZAKO.



Polisi kila siku mnatukumbusha kuhusu utapeli leo watu wanaandamana kupinga utapeli mnawazuia tena duh!
 
Sijaelewa wametapeliwaje ada? Je huduma wanazopewa chuoni ni hafifu au ni nini?/mkuu hebu fafanua kidogo,.
 
Hivi ukiwa polisi akili huwa zinaondoka?

Wenye ndugu polisi naombeni mnisaidie nijue hili.
 
Hivi polisi hawanaga akili za kupima madai ya waandamaji?
Kwanini wasingewaita kwa kipaza sauti, wawasikilize na kuwashauri watulie ili madai yao yafikishwe panspohusika?
Unapomkamata mwanafunzi asiyekuwa na madhara ni kumjengea hofu
Ila wale walioandamana UBALOZI wa S.A kudai NDEGE walitolewa kiustaarabu wa hali ya juu, wakakamata viongozi 3 tu
 
Wanaona wenzao wapo kitaa hakuna ajira wanabaki wananeng'eneka na mabango yao kitaani kwanini hizo ada wasingeanzisha biashara ndogondogo na kuichangia serikali kwa kukata kitambulisho cha mjasiriamali. Waache usumbufu wenyee tuliopo kwenye kada mateso bila chuki wala hawasikii! Ngoja ninywe zangu Nyakageni nipumzike tuu
 
Hivi polisi hawanaga akili za kupima madai ya waandamaji?
Kwanini wasingewaita kwa kipaza sauti, wawasikilize na kuwashauri watulie ili madai yao yafikishwe panspohusika?
Unapomkamata mwanafunzi asiyekuwa na madhara ni kumjengea hofu
Sio Kazi ya Cops hiyo
 
1568054490134.png

1568054513783.png

1568054535314.png

1568054549008.png

1568054566448.png

Jeshi la Polisi limezuia maandamano ya wanafunzi zaidi ya 400 wa Chuo cha Ualimu Moshi kilichopo wilayani Hai mkoani Kilimanjaro, kisha kuwakamata baadhi yao baada ya kufunga barabara wakishinikiza serikali kuingilia kati sakata la utapeli wa zaidi ya milioni 75 za malipo ya ada.
Shinikizo hilo linachukuliwa na Wanafunzi hao baada kuzuiliwa kuingia kwenye chumba cha mtihani kutokana na Malipo yao ya Ada waliyolipa kupitia Benki kutoonekana kwenye account ya chuo hicho
 
imekuwaje pesa iliyolipwa benki isionekane kwenye akaunti ya chuo? pole kwao kwa masahibu wanayopitia.
 
imekuwaje pesa iliyolipwa benki isionekane kwenye akaunti ya chuo? pole kwao kwa masahibu wanayopitia.
Hata mimi nililipa bili ya dawasa 14,000/- kupitia 'control number' sijapta 'risiti' ya dawasa ya kumpokea malipo! Badala yake nimepata ujumbe wa benki kwamba wamepokea 10,000/-
Sijui nitaambulia upupu kama hao walimu!
 
imekuwaje pesa iliyolipwa benki isionekane kwenye akaunti ya chuo? pole kwao kwa masahibu wanayopitia.
ipo sana hii....smtmes wanafanyaga ma banktellar....anakuprintia pay in slip hewa....na wew unaondoka ukijua tayar...ndo maana kweny taasis makin ukipeleka pay in slip lisit hawakupi...mpka wapate bank statement ndo wanatoa lisit....

ikitokea umepigwa hvo inabd uende tena bank na pis yako ukafatilie hela zako
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom