Wanafunzi wa Afrika wazidi kunufaika na ufadhili wa masomo kutoka China

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,034
11.jpg

Na Tom Wanjala

Mwezi Juni mwaka huu, maelfu ya wahitimu kutoka vyuo vikuu nchini China walifuzu na shahada mbalimbali. Miongoni mwao, walikuwa wanafunzi kutoka bara la Afrika. Wahitimu hawa walijumuika na wenzao wa China, wakiwa wamevalia majoho rasmi, tayari kupokea vyeti vya kuashiria kuwa sasa walikuwa wametekeleza yote waliyokuwa wakisomea vyuoni.

Mmoja wa mamia ya wanafunzi kutoka Afrika waliofuzu katika vyuo vikuu mbalimbali nchini China, ni Silas Totolela, ambaye hivi sasa anatoa huduma zake za ukufunzi katika shule ya upili ya wavulana ya Kibabii, iliyo kaunti ya Bungoma, nchini Kenya. Alibahatika kupata ufadhili wa masomo na kwenda China mwaka wa 2019, alikojiunga na chuo kikuu cha Central China Normal University, kilicho katika mji wa Wuhan, mkoa wa Hubei. Totolela alifuzu shahada ya uzamili katika taaluma ya Elimu, akizamia kitengo cha mtaala na mbinu za ukufunzi.

“Ni furaha isiyo na kifani kwangu na wenzangu, haswa kutoka Afrika tuliofuzu pamoja. Kwa muda wa miaka miwili tuliyokuwa China, maisha yalikuwa mazuri. Tulijihisi nyumbani kabisa,’’ bwana Totolela alisema alipokuwa akihojiwa na CRI Kiswahili.

1222.jpg

Kuhusu namna walivyopata ufadhili huu, Totolela anasema kuwa kila mwaka, serikali ya China hutoa nafasi kadhaa kwa wanafunzi kutoka mataifa mbalimbali Afrika wanaotaka kwenda kuendeleza masomo yao nchini China.

“Mwishoni mwa mwaka wa 2018, Wizara ya Elimu ya Kenya iliweka wazi tangazo rasmi kwenye tovuti yake na kutoa mwaliko kwa Wakenya waliotaka ufadhili wa kuendeleza masomo yao ya ngazi ya juu nchini China. Nilituma maombi na nikabahatika kuwa miongoni mwa makumi ya Wakenya waliojaliwa nafasi hizi za kipekee za ufadhili wa masomo kwa hisani ya serikali ya China.” ,anasema Totolela.

Siku zote kuku mgeni hakosi kamba mguuni. Totolela anaungama kwamba walipofika China, walikuwa na hisia mseto. Furaha, na upande mwingine kuchanganyikiwa wasijue lipi la kufanya na kutofanya. Ila, wenyeji wao wa China, walikuwa nao sako kwa bako tayari kuwasaidia na kuwafaa kwa hali na mali ili watulie kiakili na kuanza masomo yao.

‘’Sisi kutoka Afrika tumezoea vyakula vyetu. Tulipata changamoto kwa siku kadhaa katika upande wa chakula na vile vile mawasiliano. Hata hivyo, baada ya siku kadhaa, tulikuwa sawa kabisa. Tulijifunza Kichina sanifu “Mandarin” na hili likarahisisha mawasiliano kati yetu na Wachina,’’ anasema Totolela.

Kuhusu mfumo wa elimu wa China, Totolea ambaye hivi sasa amerejea Kenya, anasema kwamba Afrika inaweza kujifunza mengi sana kutoka kwenye mfumo huu wa China. Akitoa mfano wa wahandisi wa Kichina ambao wana kandarasi za kujenga miundo mbinu aina mbalimbali katika mataifa mengi ya Afrika, Totolela anahimiza mataifa ya Afrika kubadilisha mifumo yao ya elimu na kuzingatia mno katika vyuo vya kiufundi au vya anuwai.

‘’Vyuo vya Mafunzo ya Ufundi (Technical Training Institutes) ndivyo vimeshikilia uchumi wa China. Bara letu la Afrika linapaswa kuwekeza katika vyuo hivi. Wachina wengi wanaojenga barabara, majumba ya kifahari, madaraja ya kipekee, na reli za kisasa, wamesomea katika vyuo vya Mafunzo ya Ufundi. Waafrika wengi tuna dhana kwamba, mtu akisomea katika chuo cha kiufundi hana thamani. Hapa ndipo teknolojia ya China inaibukia,’’ anasema Totolela.

Mnamo mwaka wa 2018, serikali ya China ilitoa nafasi 50,000 za ufadhili wa masomo ya ngazi za juu kwa wanafunzi kutoka Afrika. Mwaka huo huo, China ilishuhudia idadi kubwa zaidi ya wanafunzi kutoka Afrika, hali ambayo imesalia hadi sasa. China inazidi kupokea wanafunzi wengi kutoka mataifa ya Afrika kushinda mabara mengine duniani, hii ikiwa ni kutokana na ushirikiano mwema kati ya China na bara la Afrika.

Kulingana na mchambuzi wa masuala ya elimu kutoka Kenya, Felix Jones, masomo ya ngazi za juu ya China ni nafuu ikilinganishwa na mataifa mengine yaliyoendelea duniani.

“Kando na kuwa elimu ni nafuu nchini China, viwango vyake vya ubora pia vipo juu zaidi ukilinganisha na mataifa mengine duniani. Vile vile, ufadhili wa masomo na serikali ya China kwa Waafrika na kurahisishwa kupata viza ya masomo, ni baadhi ya sababu kuu ambazo zinafanya wanafunzi wengi wa Afrika na mabara mengine kwenda China kwa masomo zaidi,’’ anasema bwana Jones.

Kila mwaka, China hutoa nafasi za ufadhili wa mafunzo ya taaluma mbali mbali na masomo ya ngazi za juu kwa raia wa mataifa mengi ya Afrika.
 
We ndo yupi hapo? Sasa uwe umesoma NADHARIA uanze kutupigia kelele kuhusu AJIRA tutakutukana hadi ushangae.
 
Dah mi nataka za Europe ili nikapige na maisha huko kabisa. Nataka kutumia daraja la elimu kama gia wazee nani tuungane?
 
Back
Top Bottom