TUKUTUKU
JF-Expert Member
- Sep 14, 2010
- 11,768
- 4,033
Serikali ya shirikisho la wanafunzi wa chuo kikuu Dodoma (UDOSO) imekanusha taarifa iliyotolewa na msemaji wa wanafunzi wa vyuo vikuu mkoani Dodoma na waziri wa sheria na katiba wa chuo kikuu cha Dodoma kwa tamko la kukitaka chama cha democrasia na maendeleo (CHADEMA) kiombe radhi kwa kitendo cha kususia hotuba ya rais Kikwete bungeni.Tamko la serikali ya shirikisho lililosainiwa na katibu mkuu wa UDOSO bw.Marwa Joseph linaweka wazi kwa umma kwamba Bw.Thobias Mwasiga sio msemaji wa vyuo vikuu kanda ya Dodoma kama alivyojinadi na pia sio waziri wa katiba na sheria wa chuo kikuu cha Dodoma.Kwa mujibu wa habari hizo Bw.Mwasiga ni waziri katika chuo cha sanaa,lugha na sayansi ya jamii moja kati ya vyuo vinavyounda chuo kikuu cha Dodoma.Kwamba hata chuo chake hakikumtuma kusema alivyosema na kuandikwa na gazeti hili toleo lake la tarehe 20/11/2010 kwa kichwa cha habari vyuo vikuu Dodoma wataka CHADEMA iombe radhi.
Tamko hilo liliongeza kwamba serikali ya wanafunzi ina majukumu yake ya kikatiba na haijihusishi kabisa na masuala ya siasa za vyama hivyo limesikitishwa sana na kitendo cha kiongozi huyu na kusisitiza kwamba taarifa hiyo haikuwa ya kweli kwa vile sio maoni wala mtazamo wa serikali ya wanafunzi.
Serikali ya wanafunzi haina mpango wa kutoa tamko lolote kuhusiana na kilichotokea bungeni.Aidha ieleweke kwamba kiongozi huyo alitoa tamko lake kwa maoni na mtazamo wake binafsi kwa vile hakutumwa na mamlaka yeyote.(Chanzo cha habari hii:Majira, 28/11/2010,pp.3)
My take
Inasikitisha sana kuona wanafunzi wa vyuo vikuu ambao ni kioo cha jamii wanakuwa mara kwa mara wakitoa habari za kushangaza jamii, na jamii kuanza kutilia shaka uwezo wa kuchanganua mambo wa wanafunzi hawa wa vyuo vikuu katika miaka ya hivi karibuni. Hatukatai kuwa wanafunzi hawa wana haki ya kikatiba ya kutoa maoni yao ilimladi tu wasivunje sheria za nchi,lakini ni matumaini ya wanajamii kupata maoni ya mawazo yaliyopevuka kwa kuwa ni wasomi ambao wanapaswa kuwa kioo cha jamii.Nakumbuka wakati sisi tulipokuwa tunasoma chuo vikuu,jamii ilikuwa ikiheshimu sana maoni yetu kwa kuwa tulikuwa makini sana.Lakini katika miaka ya hivi karibuni utasikia wamesema hivi mara vile,wamekuwa kama bendera ambayo daima hufuata upepo na kukosa msimamo thabiti hii ni aibu kubwa kwa wanafunzi wa vyuo vikuu.Cha kuziuliza ni kwamba wanafunzi hawa wanatumiwa na wanasiasa?wananjaa ndiyo maana wanatapata sana?au ndiyo maendeleo ya sayansi na teknolojia?au ni uwezo mdogo wa kizazi cha sasa? au ni mmomonyoko wa maadili?Wadodo zangu epukeni aibu hii, tujenge nchi yetu kwa kutoa mawazo yatakayotatua matatizo ya nchi yetu mbalimbali.
Tamko hilo liliongeza kwamba serikali ya wanafunzi ina majukumu yake ya kikatiba na haijihusishi kabisa na masuala ya siasa za vyama hivyo limesikitishwa sana na kitendo cha kiongozi huyu na kusisitiza kwamba taarifa hiyo haikuwa ya kweli kwa vile sio maoni wala mtazamo wa serikali ya wanafunzi.
Serikali ya wanafunzi haina mpango wa kutoa tamko lolote kuhusiana na kilichotokea bungeni.Aidha ieleweke kwamba kiongozi huyo alitoa tamko lake kwa maoni na mtazamo wake binafsi kwa vile hakutumwa na mamlaka yeyote.(Chanzo cha habari hii:Majira, 28/11/2010,pp.3)
My take
Inasikitisha sana kuona wanafunzi wa vyuo vikuu ambao ni kioo cha jamii wanakuwa mara kwa mara wakitoa habari za kushangaza jamii, na jamii kuanza kutilia shaka uwezo wa kuchanganua mambo wa wanafunzi hawa wa vyuo vikuu katika miaka ya hivi karibuni. Hatukatai kuwa wanafunzi hawa wana haki ya kikatiba ya kutoa maoni yao ilimladi tu wasivunje sheria za nchi,lakini ni matumaini ya wanajamii kupata maoni ya mawazo yaliyopevuka kwa kuwa ni wasomi ambao wanapaswa kuwa kioo cha jamii.Nakumbuka wakati sisi tulipokuwa tunasoma chuo vikuu,jamii ilikuwa ikiheshimu sana maoni yetu kwa kuwa tulikuwa makini sana.Lakini katika miaka ya hivi karibuni utasikia wamesema hivi mara vile,wamekuwa kama bendera ambayo daima hufuata upepo na kukosa msimamo thabiti hii ni aibu kubwa kwa wanafunzi wa vyuo vikuu.Cha kuziuliza ni kwamba wanafunzi hawa wanatumiwa na wanasiasa?wananjaa ndiyo maana wanatapata sana?au ndiyo maendeleo ya sayansi na teknolojia?au ni uwezo mdogo wa kizazi cha sasa? au ni mmomonyoko wa maadili?Wadodo zangu epukeni aibu hii, tujenge nchi yetu kwa kutoa mawazo yatakayotatua matatizo ya nchi yetu mbalimbali.