Wanafunzi UDSM kuishtaki serikali. Wataka kiswahili kiwe lugha ya kufundishia.

kigugumizi

Member
Sep 10, 2009
11
4
wanafunzi wa shahada ya Uzamili - Kiswahili wa Chuo Kikuu cha Dar wapo mbioni kufungua kesi ya kikatiba katika mahakama kuu dhidi ya Serikali ya Tanzania kwa kuzuia uhuru wa kutoa maoni/kujieleza kwa watanzania kwa kuruhusu watanzania wajieleze kwa lugha ya kiingereza, na dhidi ya sera onezi ya lugha mwigo wa ukoloni.

PIA WANADAI + KUSEMA + KULAANI:
  • Wanasema kuwa hakuna Nchi duniani iliyoweza kuendelea kwa lugha za watu wengine.
  • wanalaani mauaji ya halaiki ya watoto wa kitanzania katika fikra zao kwa kusoma katika mazingira yao kwa lugha za wakoloni/wageni.
  • wanalaani viongozi wenye mamlaka makubwa ya kisera kuutukuza ukoloni mkongwe na vipamba ukoloni mkongwe huo ikiwemo lugha, mintaarafu lugha ya kiingereza.
  • Wanazidi kusubiri na kukumbushia ahadi ya Waziri Mkuu aliyoitia mwezi wa saba UDSM kwenye ufunguzi wa TATAKI (IKS) kuwa lugha ya kiswahili itumike kama chombo cha kufundishia.
  • Wanaalani sana kuwa ni sawa na watu waliotupwa katika kisiwa ombwe- kifikra, hivyo kukosa utamaduni wao madhubuti na kitambulisho chao sahihi katika uwanja wa Taifa na kimataifa.
  • Wanasema - China, Urusi, Uturuki, Sweden, Uingereza, Norway, Ubelgiji wameendelea kwa lugha zao wenyewe.
  • Wanakubali umilisi na umahiri wa lugha ya kiingereza kwa watanzania kama lugha yoyote ya ujuzi na utambuzi zaidi, lakini isiwe lugha ya ukuzaji wa fikra pembuzi kwa watanzania.
  • wanadai kuwa maamuzi haya yatapelekea kujuta na kusababisha kifungo cha roho kitakachoplekea kuwa omba omba siku zote kama hali hii inavyoongezeka siku hadi siku kwa watanzania.
  • Fikra bebuzi hutokana na ujuzi wa lugha mama (fact), uletao maendeleo ya kiuchumi.
 
One of the country developed without using its language is America, English wasn't an american language before the British invasion. Many young people in south Africa died becasue they wanted to be taught in English (International language). we are now in globalisation not in colonial era. we want our graduates to be internationally competitive in the job market. wakenya wanachukua vibarua vyetu just because of they speak English. anyway let them go we can know their nosense.
 
points...asilimia 99%ya watanzania hawawezi kuongea fluent english najua kuna mtu atabisha lakini habari ndi hiyonaongelea watz wanaoishi tz
 
Kiswahili si suluhisho.... tatizo ni uongozi mbovu wa CCM na misingi mibovu iliyowekwa na hiyo CCM!!!
 
One of the country developed without using its language is America, English wasn't an american language before the British invasion. Many young people in south Africa died becasue they wanted to be taught in English (International language). we are now in globalisation not in colonial era. we want our graduates to be internationally competitive in the job market. wakenya wanachukua vibarua vyetu just because of they speak English. anyway let them go we can know their nosense.

Kimsingi nakubaliana na mfano wako wa nchi ya Amerikana. Lakini pia yakupasa kufahamu kuwa kishwahili sio lugha ya makabila yote ya Tanzania, ila mkakati uliotumika kukieneza ndio ulichokifanya kiwe kama Kingereza kwa Amerikana. Kama Tanzania ingejizatiti katika kingereza kama nchi zinazotuzunguka, tungekuwa nasi pia tunakimwaga vile, lakini kwa sababu ya msisitizo wa kiswahili ndio maana tumebaki. Nadhani huu ni wakati mwafaka kabisa kama taifa kuhamua kuibeba lunga moja kwa ujumla wake ni nyingine kuzifanya kuwa lugha za nyongeza.

Wenzetu Rwanda walikuwa wanatumia kifaransa, ila walipofanya tathmini ya maendeleo yao siku za usoni ikiwa ni pamoja na Jiographia yao, waliridhika kuwa sio kifaransa wala kiswahili kitakachowafaa, ila ni "KINGEREZA". Asilimia kubwa ya warundi na wanyaruanda wanaongea kiswahili, ila hawajaifanya lugha ya msingi, ila ya ziada. Na hii ndivyo ilivyo kwa afrika yote ya mashariki na kusini isipokuwa Msumbiji.

Ni uamuzi wetu kupanga na bado hatujachelewa.

Shida kubwa, tuna viongozi waliowaoga wa kuthubutu na kufanya maamuzi hata yale yaliyomepesi. Mfano kuzuia magari ya srikali yasibebe nyasi!
 
Hii ni case ya kimasilahi, Kwa kusema "wanafunzi wa shahada ya uzamili-kiswahili". Nikajua wazi kuwa wanataka deal la kutafsiri vitabu vya kiingereza kwenda kiswahili.

Ukweli utabakia pale pale kuwa English now is the world language, Tukitaka kufunga milango ya maendeleo basi tutumie kiswahili mashuleni. Kupata kazi Tanzania tu bila kujua English ni kazi, iwe kusoma kwa kiswahili?.

Waanze na sheria za uwekezaji kuwa ni lazima wawekezaji watumia kiswahili, tuje kwenye international arena, then ndiyo tugeukie kuandika vitabu vya kiswahili. No English no deal for developing countries like TZ
 
  • Wanasema - China, Urusi, Uturuki, Sweden, Uingereza, Norway, Ubelgiji wameendelea kwa lugha zao wenyewe.


Hawa nafikiri wana ajenda yao ya siri tusiyoiujua. Ni kama walimu wao hapo idarani kwao wanaopigania kila siku lugha ya kufundishia hadi chuo kikuu iwe kiswahili ili wapate tenda ya kutafsiri vitabu vya kufundishia. Huku wakitaka hilo watoto wao wanasoma nje ya nchi sijui kwa nini. Mbaya zaidi hawahawa wanaenda kusoma PhD za kiswahili Canada huku wakitumia kiingereza, it is so funny.

Dunia sasa ni kijiji na lugha ya dunia hii ni kiingereza. Hata hizo nchi walizozitaja hapo juu hivi sasa kiingereza kinatumika sana tu. Ukiwa unajua kiingereza China wewe ni mali adimu. Kwa sasa karibu Wanorway na Waswidishi wote wanaongea Kiingereza ukiwatoa wazee japo hata wazee wako wanaoongea kiingereza vizuri tu.

Hatutaendelea kwa kutumia kiswahili na zaidi ndo tutazidi kudidimia, maana pamoja na kutumia kiingereza bado kiingereza cha watanzania wengi si kizuri. Nimeona hata wanafunzi wanaosoma PhD nje ya nchi wakipata shida sana kukiongea, sasa tukileta kiswahili ndo kwisha habari kabisa.

Wajerumani na Wajapan walishatangulia siku nyingi and they are the largest economies in their continents (Germany for Europe and Japan for Asia) kwahiyo tusiwaige hao.

Nawaasa waache ubinafsi na unafiki wao.
 
Hawa watu hawana uchungu kabisa na nchi hii, wananchi na wasomi wa taifa hili. Kanza si ukiwafatilia hao woote utakuta watoto wao wanasome english medium. Ni uwazi usiopingika kwamba nafasi nyingi za makampuni binafsi zimekua zikichukuliwa na wenzetu hasa Kenya kwa kigozo kimoja cha kimombo. Tunapozungumzia ulimwengu wa utandawazi tukikiacha kimombo tutakua tumejichimbia kaburi. Tena with common labour market ya East Africa sijui tunategemea mtanzania mahiri wa methali na nahau za kiswahili asiejua ung'enge aajiriwe na nani.

Imefika wakati ndugu zangu uhamasihaji wa matumizi ya kiingereza yawe kila mahali, elimu yote from chekechea iwe kiingereza, majumbani na hata ikiwezekana kwenye sehemu za ibada makanisani na misikitini ili vijana wetu wakijue barabara.

Kiswahili hakina maslahi tena ndugu zangu,bila kingereza ndugu hata mhindi wa kariakoo nadra akuajiri leo hii mnataka mitaala iwe kwa kiswahili!!!!!!!!!!!!
 
Lugha ya kufundishia ni jambo linalohitaji mjadala mpana na usio hitaji ushabiki. Tunafundisha watu ili waweze kuyakabili mazingira yao na sio waweze kuuchapa umombo. Kuuchapa umombo ukienda tuition ya kiingereza kwa miezi mitatu utaweza.

Tunataka wasomi waliobobea ambao wanaweza kufanya mambo ya kueleweka: Waweze kuitafsiri sayanzi na technolojia kwa vitendo. Hicho ndicho wanachotuzidi wale chui wa Asia. Wanaosema kiingereza ni lugha ya dunia hebu wa bofye hapo chini



http://listverse.com/2008/06/26/top-10-most-spoken-languages-in-the-world/
 
Hoja walizonazo zina ukweli asilimia 80, lakini kwa ulimwengu wa sasa nisingeshauri tuingie huko kwenye kutumia Lugha ya Kiswahili. Pamoja na kusoma Kiingereza toka sekondary, bado kinatukimbiza, iwe tutakapotumia kiswahili, halafu kiingereza unajifunza kama second language? Nafikiri hiyo itakuwa ni hatari zaidi.Tunaweza tukatupwa nje kwenye kila business ya kimataifa.
 
Check Job advertisement magazetini au online,moja ya sifa ni MUST BE FLUENT IN BOTH SPOKEN AND WRITTEN ENGLISH.Swali la English kuwa medium of instruction halina mjadala hasa ukizingatia EA common market na globalization.Further resourse nyingi on web available in english.Consider student learning say Newtons laws motion,uswahilini he / she googles kanuni za mwendo za newtoni matokeo?On the otherhand if student gooolles Newton laws motion results kibao tu.
 
Watawapa mtihani mgumu kweli majaji maana hata wao mwenendo wa kesi wanaandika kwa lugha ya mkoloni!
 
Watu wegi waliochangia hapa bado wametawaliwa na mawazo ya kikoloni. Wanadhani kusoma na kuelimika ni kujua kimombo. Loooooooooooh.
Hapana sababu nyingine ya maana ninayosoma hapa ikipinga kiswahili kutumika kama lugha mbadala hadi mtu kupata PHD.
Mambo ya kazi na nini sijui hayo ni jinsi gani policies zetu zinaelekeza sioni kama kuna shida.
Wakija wageni jambo la kwanza na wajifunze lugha yetu, then wafanye uwekezaji.
Mbona wanakwenda arabuni na sehemu nyingine na wanawekeza huku hao citizens hawajui kimombo?
Kupanga ni kuchagua.
 
Wanaishtaki kwa kuwa Serikali ndio mwenye sera (juu ya lugha ya kufundishia) au sera ni ya chama kinachounda serikali? Nadhani kama wamepania kweli kufungua kesi hii, mshtakiwa wa kwanza awe CCM.

Hata hivyo, hoja ya ukoloni katika hili imepitwa na wakati. Jamani, mimi ni miongoni mwa mashahidi wa kinachoendelea katika mataifa ambayo hayakutawaliwa na mwingereza, lakini mwelekeo wa utandawazi na umataifishaji (internationalisation) wa elimu unakifanya kiingereza kitumike katika elimu za mataifa ambayo wala usingetarajia (matharani katika mataifa wanachama wa EU).
Waleta mashtaka, fikirieni mara mbili.
Mara nyingi madai kama haya yanatokana na tafiti zinazodai kwamba lugha ya mama ndio lugha bora zaidi ya kufundishia. Jiulizeni swali, hivi kweli kwa watanzania, kiswahili ni lugha ya mama? Labda jibu ni ndio kwa baadhi ya watu, lakini wengi wetu tulikutana nacho shuleni, kama tulivyokuta kiingereza huko huko.

Aidha, ikitokea mkashinda hii kesi, kumbukeni nchi yetu vile vile iko katika sera ya ubinafsishaji. Sipendi kutabili, lakini nawahakikishieni siku serikali ikiamua mtakavyo, Kiswahili tutakiona tu kwenye shule za kata (ambazo kabla ya yote hazina walimu) na shule hadi vyuo binafsi, kiingereza kitaendelea. Na mwisho wa siku tofauti ya kimadaraja (social classes) ndio kwanza itaongezeka.
Fikirieni mara mbili
 
OK,

Someni kiswahili, lakini kwanza andikeni vitabu kiswahili, tungeni maneno yatakayoeleza kuanzia quantum mechanics mpaka relativity, complete with "singularity vortex" na action atv a distance spookiness katika kiswahili etc etc

Kiswahili chenyewe kinachoangaliwa kama ufumbuzi watu hawakijui, whats next, mtataka watu wafundishwe kwa lugha za makabila?

Mfa maji heshi kutapatapa.Katika dunia ya leo ya utandawazi ni muhimu tukawa on a par with the rest of the world, especially kwa sababu sisi tuko nyuma, ndipo hapa mchonga alisema wenzetu wakitembea sisi tkimbie.

Sasa tuna demonstrate vipi kukimbia kama hatutaki kutumia kiingereza as a teaching language?

Usiige tembo kunya, utapasuka msamba, hivi mnajua gharama za hiii experiment? katika nchi ambayo inahitaji kila senti?

Chances are, mtu atakayeshindwa kujifunza masomo ya elimu ya juu katika kiingereza atashindwa pia katika Kiswahili.Kwa sababu Kiswahili hiki cha elimu ya juu kitakuwa just as foreign as kiingereza.

I should know about that, nilishaanza kufanya project ya ku translate some popular string theory text into Swahili, ika dawn on me kwamba most people watakaotaka kusoma this type of thing wanajua kiingereza, na wasiojua kiingereza wengi hawatakuwa na interest au wakiwa na interest the physics will be too much for them, watakaofaidika na translation ni wachache sana, it wasnt worth it, unless mtu anataka ujiko na kukiweka Kiswahili kwenye ramani.

Hapa watu wanatafuta sababu tu za ku justify uzembe sehemu nyingine na chuki juu on kiingereza, "lugha ya mkoloni".

As if hatuna wakoloni weusi wanaoongea Kiswahili cha Mkapa na kuki qualify Kiswahili cha Mkapa nacho kama "lugha ya mkoloni" .
 
Ni wazo zuri sana but panatakiwa kuangalia mazingira pamoja na future ya nchi na upepo wa dunia inakokwenda.

wakuu kwa taifa lisilokua na vision kama Bongoland mnataka kujikaanga wenyewe na mafuta yenu maana mtakua mmejiingiza kwenye ,mtego ambao mtaujutia milele.

ntarudi badaaye .....kuwaeleza
 
Watu wana import mpaka pini wanataka kumuiga Mchina, Mswede ma Mturuki!
 
Back
Top Bottom