Mtu wa Pwani
JF-Expert Member
- Dec 26, 2006
- 4,187
- 670
Wanafunzi Sekondari ya Chidya `wapagawa`
na abdallah bakari, mtwara
WANAFUNZI wa Sekondari ya Wavulana Chidya, iliyopo Wilaya ya Masasi, mkoani hapa, wamechoma shule hiyo na kuharibu mali mbalimbali, zikiwamo za mkuu wa shule, kwa kile wanachodai kuchoshwa kunywa uji usio na sukari.
Tukio hilo lilitokea juzi, saa 2:30 usiku, baada ya baadhi ya wanafunzi shuleni hapo, kujikusanya na kuanza vurugu zilizosababisha hasara ya zaidi ya Sh milioni 34.
Habari kutoka eneo la tukio zinadai kuwa wanafunzi hao licha ya kuchoma shule hiyo, pia walichoma gari la shule aina ya Isuzu, tani saba, zizi la ngombe, mbolea na dawa ya mimea mali ya mkuu wa shule hiyo, Gaitan Mwatenga. Pia wanafunzi hao wanadaiwa kuvunja na kusomba vitu vilivyokuwamo katika duka linalomilikiwa na mhasibu wa shule hiyo, Salum Napinda.
Habari hizo zinadai kuwa wanafunzi hao walichoma ofisi ya walimu na maktaba ya shule na kufanikiwa kuteketeza kila kilichokuwamo ndani yake.
Wanafunzi hao wanadaiwa kuvunja luninga ya shule pamoja na kinasa mawimbi chake (Satellite Dish) kabla ya vurugu na moto huo kuzimwa na wanakijiji, baada ya walimu kuomba msaada.
Kabla ya kufanya uovu huo, wanafunzi hao walifanya mkutano katika moja ya chumba cha darasa na baadaye walizima umeme shuleni hapo.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Ephraim Mrema, wanafunzi hao walivunja stoo ya kuhifadhia vifaa vya shule hiyo na kuchukua mapanga na fyekeo na fagio ambazo walizitumia katika uharibifu huo.
Kamanda Mrema alisema polisi walipofika eneo la tukio walikuta vibutu vya fagio vilivyotumika kuchoma gari, ofisi, maktaba, na zizi la ngombe.
Alisema inadaiwa kuwa chanzo cha vurugu hizo ni wanafunzi hao kunywa uji usio na sukari kuanzia Machi, 30 mwaka huu, hadi siku ya tukio. Hali ya wanafunzi kunywa ujio usio na sukari imeelezwa na walimu kuwa imetokana na ufinyu wa bajeti.
Mrema alisema tangu kutolewa kwa taarifa za uji kutokuwa na sukari, wanafunzi walianza kupungua katika foleni ya uji siku hadi siku, jambo ambalo lilianza kuwatia shaka walimu.
Hata hivyo, licha ya walimu hao kutilia shaka mwenendo wa wanafunzi wao, hawakutoa taarifa katika vyombo vya dola.
Taarifa za kiupelelezi zinaonyesha kuwa hakukuwapo na mawasiliano mazuri kwa wanafunzi juu ya kuwapo kwa uji usio na sukari, walimu hawakuwa wazi kwa wanafunzi. Hata kama walitoa taarifa ni kwa wachache ambao nao hawakufikisha ujumbe kwa wenzao, alisema Kamanda Mrema.
Kamanda alisema jeshi lake linawatuhumu wanafunzi watano, akiwamo Kiranja Mkuu wa shule hiyo, Hamidu Matema (18) ambaye ni wa kidato cha nne. Hata hivyo, Matema amefanikiwa kutoroka na hajulikani alipo. Wanafunzi wengine wanne wamekamatwa.
Aliwataja wanaotuhumiwa na ambao watafikishwa mahakamani wakati wowote kuwa ni Hamidu Haruna (18) wa kidato cha nne, Mwahamudu Issa (18) kidato cha tatu, na wengine wawili wa kidato cha pili ambao ni Shabani Ramadhani (18) na Ramadhani Bofu (18).
Katika vurugu hiyo, wanafunzi 20 walitajwa kuhusika na tukio hilo. Uchunguzi wa awali wa polisi uliwabaini watuhumiwa hao kuhusika moja kwa moja, hivyo watafikishwa mahakamani na wengine 15 watajadiliwa katika vikao vya Bodi ya Shule na kuadhibiwa.
Shule hiyo ya bweni iliyoko umbali wa kilomita 22 kutoka barabara kuu ya Mtwara kwenda Masasi, ni miongoni mwa shule kongwe nchini. Ilianzishwa mwaka 1923, ikiwa chini ya Kanisa la Anglikana. Kwa sasa inamilikiwa na Serikali, ikiwa na mafanikio ya kuridhisha kitaaluma. Mwaka jana, wanafunzi 47 walichaguliwa kujiunga na kidato cha tano na hivyo shule hiyo kushika nafasi ya kwanza katika Mkoa wa Mtwara.
mtanzania
na abdallah bakari, mtwara
WANAFUNZI wa Sekondari ya Wavulana Chidya, iliyopo Wilaya ya Masasi, mkoani hapa, wamechoma shule hiyo na kuharibu mali mbalimbali, zikiwamo za mkuu wa shule, kwa kile wanachodai kuchoshwa kunywa uji usio na sukari.
Tukio hilo lilitokea juzi, saa 2:30 usiku, baada ya baadhi ya wanafunzi shuleni hapo, kujikusanya na kuanza vurugu zilizosababisha hasara ya zaidi ya Sh milioni 34.
Habari kutoka eneo la tukio zinadai kuwa wanafunzi hao licha ya kuchoma shule hiyo, pia walichoma gari la shule aina ya Isuzu, tani saba, zizi la ngombe, mbolea na dawa ya mimea mali ya mkuu wa shule hiyo, Gaitan Mwatenga. Pia wanafunzi hao wanadaiwa kuvunja na kusomba vitu vilivyokuwamo katika duka linalomilikiwa na mhasibu wa shule hiyo, Salum Napinda.
Habari hizo zinadai kuwa wanafunzi hao walichoma ofisi ya walimu na maktaba ya shule na kufanikiwa kuteketeza kila kilichokuwamo ndani yake.
Wanafunzi hao wanadaiwa kuvunja luninga ya shule pamoja na kinasa mawimbi chake (Satellite Dish) kabla ya vurugu na moto huo kuzimwa na wanakijiji, baada ya walimu kuomba msaada.
Kabla ya kufanya uovu huo, wanafunzi hao walifanya mkutano katika moja ya chumba cha darasa na baadaye walizima umeme shuleni hapo.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Ephraim Mrema, wanafunzi hao walivunja stoo ya kuhifadhia vifaa vya shule hiyo na kuchukua mapanga na fyekeo na fagio ambazo walizitumia katika uharibifu huo.
Kamanda Mrema alisema polisi walipofika eneo la tukio walikuta vibutu vya fagio vilivyotumika kuchoma gari, ofisi, maktaba, na zizi la ngombe.
Alisema inadaiwa kuwa chanzo cha vurugu hizo ni wanafunzi hao kunywa uji usio na sukari kuanzia Machi, 30 mwaka huu, hadi siku ya tukio. Hali ya wanafunzi kunywa ujio usio na sukari imeelezwa na walimu kuwa imetokana na ufinyu wa bajeti.
Mrema alisema tangu kutolewa kwa taarifa za uji kutokuwa na sukari, wanafunzi walianza kupungua katika foleni ya uji siku hadi siku, jambo ambalo lilianza kuwatia shaka walimu.
Hata hivyo, licha ya walimu hao kutilia shaka mwenendo wa wanafunzi wao, hawakutoa taarifa katika vyombo vya dola.
Taarifa za kiupelelezi zinaonyesha kuwa hakukuwapo na mawasiliano mazuri kwa wanafunzi juu ya kuwapo kwa uji usio na sukari, walimu hawakuwa wazi kwa wanafunzi. Hata kama walitoa taarifa ni kwa wachache ambao nao hawakufikisha ujumbe kwa wenzao, alisema Kamanda Mrema.
Kamanda alisema jeshi lake linawatuhumu wanafunzi watano, akiwamo Kiranja Mkuu wa shule hiyo, Hamidu Matema (18) ambaye ni wa kidato cha nne. Hata hivyo, Matema amefanikiwa kutoroka na hajulikani alipo. Wanafunzi wengine wanne wamekamatwa.
Aliwataja wanaotuhumiwa na ambao watafikishwa mahakamani wakati wowote kuwa ni Hamidu Haruna (18) wa kidato cha nne, Mwahamudu Issa (18) kidato cha tatu, na wengine wawili wa kidato cha pili ambao ni Shabani Ramadhani (18) na Ramadhani Bofu (18).
Katika vurugu hiyo, wanafunzi 20 walitajwa kuhusika na tukio hilo. Uchunguzi wa awali wa polisi uliwabaini watuhumiwa hao kuhusika moja kwa moja, hivyo watafikishwa mahakamani na wengine 15 watajadiliwa katika vikao vya Bodi ya Shule na kuadhibiwa.
Shule hiyo ya bweni iliyoko umbali wa kilomita 22 kutoka barabara kuu ya Mtwara kwenda Masasi, ni miongoni mwa shule kongwe nchini. Ilianzishwa mwaka 1923, ikiwa chini ya Kanisa la Anglikana. Kwa sasa inamilikiwa na Serikali, ikiwa na mafanikio ya kuridhisha kitaaluma. Mwaka jana, wanafunzi 47 walichaguliwa kujiunga na kidato cha tano na hivyo shule hiyo kushika nafasi ya kwanza katika Mkoa wa Mtwara.
mtanzania