Wanafunzi msijichoshe kufaulu sana, ajira haziangalii ufaulu mkubwa

Jokajeusi

JF-Expert Member
Jun 1, 2018
6,305
10,564
Nimecheka leo nilipokuwa maeneo ya mjini huko, nilisikia vijana wakilalamika kuwa; wanajuta kufaulu kwa kiwango cha juu kwani hakuna maana yoyote na haisaidii popote pale.

Nina kiji-internet Cafe changu hapa mjini, sasa baada ya kusikia tangazo la ajira za waalimu na afya, nikasema acha nisimamie shoo mwenyewe kupiga pesa za wasaka ajira. Ofisi yangu ilianza kufurika jana saa tisa na mpaka saa nne usiku nilikuwa nao waomba ajira.

Sasa kinachonifanya niandike hapa, ni mwalimu mmoja mwenye umri wa miaka 29, aliyemaliza mwaka 2015 chuo cha DUCE.
Maneno yake yalinifanya nicheke lakini yalinitafakarisha sana.

Vyeti vyake vya O Level ana divisheni one ya 16 masomo tisa. A'Level ana divisheni one ya 9 Combination ni PCM. Transcript yake niliona anaka-GPA ka 3.8 kutoka pale mlimani/Duce Ambapo GPA hiyo sio haba kwa kweli hasa kwa masomo ya Physics na Mathematics.

Yule kijana alisema akiwaambia wenzake aliokuja naye, baada ya kusifiwa kwa ufaulu huo ambao kimsingi ni mkubwa, yule kijana akasema;

"Kinachoniumiza ni kuwa nilijitesa bure ili nipate ufaulu mkubwa kwa lengo nikimaliza shule na chuo nisipate shida kupata ajira. Ninachoshangaa ni kuwa wenzangu wenye ufaulu mdogo wao ndio wanaajiriwa, mimi niliyekaza na kukesha usiku na kufaulu mpaka sasa nasota. Huu mwaka unaenda wa sita naomba ajira serikalini nakosa"

Maelezo hayo yalinichekesha kwani ni kweli kabisa, na yalinigusa hata mimi kwani mimi nilifaulu kwa madaraja ya mwisho kabisa.
O'Level nilipata divisheni three ya 24, A'Level nikapata divisheni three ya 15, Chuo kikuu nikapata GPA ya 2.6:D:D:D:D:D:D:D:DIngawaje sijasoma ualimu wala udaktari, lakini nilipata kazi mapema sana, miaka ya 2011 licha ya kuwa fani niliyosomea ajira zake ni ngumu kupatikana na wasomi ni wengi. Nilipata kazi nikiwaacha solembe wenye shule na misonge yao:D:D:D:D:D:D

Kufaulu sana sio kupewa kazi, acheni kujichosha vijana walioko chuoni au wanafunzi mlioko shuleni.

Muhimu elimu ikae kichwani zaidi.

Poleni sana mliojifanya chuoni hamli bata kisa kitabu

Povu Ruksa
 
Jokajeusi Ufaulu mkubwa unasaidia kama ukitaka kuendelea kusoma huko vyuoni na siyo kwenye kupata Ajira.

Huyo kachelewa sana kujua hilo.

Mimi kuna watu nawajua wanafanya kazi, mishahara mpaka 1.5M kwa mwezi, kusafiri ndani ya nchi kwa siku malipo Tsh 10,000 na pesa ya nauli ya ofisi, tena sonetimes ndege.

Hotel ya kufikia inakodishwa na ofisi na kulipiwa kila kitu.

Lakini elimu darasa la 7 tu tena wengine hawajui hata kusoma vizuri. Sisi tuliotoka vyuoni ndio tunawasaidia kutoa pesa ATM.

Narudia tena ufaulu mkubwa utakusaidia kusoma mikozi huko vyuoni, kwenye ajira ni mara chache sana.
 
Ufaulu mkubwa unasaidia kama ukitaka kuendelea kusoma huko vyuoni na siyo kwenye kupata Ajira.

Huyo kachelewa sana kujua hilo.

Mimi kuna watu nawajua wanafanya kazi, mishahara mpaka 1.5M kwa mwezi, kusafiri ndani ya nchi kwa siku malipo Tsh 10,000 na pesa ya nauli ya ofisi, tena sonetimes ndege.

Hotel ya kufikia inakodishwa na ofisi na kulipiwa kila kitu.

Lakini elimu darasa la 7 tu tena wengine hawajui hata kusoma vizuri. Sisi tuliotoka vyuoni ndio tunawasaidia kutoa pesa ATM.

Narudia tena ufaulu mkubwa utakusaidia kusoma mikozi huko vyuoni, kwenye ajira ni mara chache sana.

Kweli Mkuu!!

Huyu kijana alinichekesha sana kimoyo moyo nikasema laiti angejua matokeo yangu sijui kama angekuja pale stationary
 
Nimecheka leo nilipokuwa maeneo ya mjini huko, nilisikia vijana wakilalamika kuwa; wanajuta kufaulu kwa kiwango cha juu kwani hakuna maana yoyote na haisaidii popote pale.

Nina kiji-internet Cafe changu hapa mjini, sasa baada ya kusikia tangazo la ajira za waalimu na afya, nikasema acha nisimamie shoo mwenyewe kupiga pesa za wasaka ajira. Ofisi yangu ilianza kufurika jana saa tisa na mpaka saa nne usiku nilikuwa nao waomba ajira.

Sasa kinachonifanya niandike hapa, ni mwalimu mmoja mwenye umri wa miaka 29, aliyemaliza mwaka 2015 chuo cha DUCE.
Maneno yake yalinifanya nicheke lakini yalinitafakarisha sana.

Vyeti vyake vya O kevel anadivisheni one ya 16 masomo tisa. A'Level anadivisheni one ya 9 Combination ni PCM. Transcript yake niliona anaka-GPA ka 3.8 kutoka pale mlimani/Duce Ambapo GPA hiyo sio haba kwa kweli hasa kwa masomo ya Physics na Mathematics.

Yule kijana alisema akiwaambia wenzake aliokuja naye, baada ya kusifiwa kwa ufaulu huo ambao kimsingi ni mkubwa, yule kijana akasema;
"Kinachoniumiza ni kuwa nilijitesa bure ili nipate ufaulu mkubwa kwa lengo nikimaliza shule na chuo nisipate shida kupata ajira. Ninachoshangaa ni kuwa wenzangu wenye ufaulu mdogo wao ndio wanaajiriwa, mimi niliyekaza na kukesha usiku na kufaulu mpaka sasa nasota. Huu mwaka unaenda wa sita naomba ajira serikalini nakosa"

Maelezo hayo yalinichekesha kwani ni kweli kabisa, na yalinigusa hata mimi kwani mimi nilifaulu kwa madaraja ya mwisho kabisa.
O'level nilipata divisheni three ya 24, A'Levele nikapata divisheni three ya 15, Chuo kikuu nikapata GPA ya 2.6:D:D:D:D:D:D:D:D. Ingawaje sijasoma ualimu wala udaktari, lakini nilipata kazi mapema sana, miaka ya 2011 licha ya kuwa fani niliyosomea ajira zake ni ngumu kupatikana na wasomi ni wengi. Nilipata kazi nikiwaacha solembe wenye shule na misonge yao:D:D:D:D:D:D

Kufaulu sana sio kupewa kazi, acheni kujichosha vijana walioko chuoni au wanafunzi mlioko shuleni.

Muhimu elimu ikae kichwani zaidi.

Poleni sana mliojifanya chuoni hamli bata kisa kitabu

Povu Ruksa

Sasa mfano mtu anataka kuwa profesa bado unashauri asisome sana ili apate ka gpa ka 2.6 kama kako?
 
Nimemaliza Chuo na Lower Second ya Kawaida saana.. though Advance na Olevel Nlikuwa Kipanga..

Ila Nilipata Kazi Safii tu..a week after university..Vipanga mpaka leo wanasota.. sana sana waliofanikiwa wanapata 400K per Month.

Anyways kwa Mfumo wa Maisha wa sasa Bandugu ajira sio issue sana.. Tutengeneze other sources of income.
 
Maelezo hayo yalinichekesha kwani ni kweli kabisa, na yalinigusa hata mimi kwani mimi nilifaulu kwa madaraja ya mwisho kabisa.
O'Level nilipata divisheni three ya 24, A'Level nikapata divisheni three ya 15, Chuo kikuu nikapata GPA ya 2.6:D:D:D:D:D:D:D:DIngawaje sijasoma ualimu wala udaktari, lakini nilipata kazi mapema sana, miaka ya 2011 licha ya kuwa fani niliyosomea ajira zake ni ngumu kupatikana na wasomi ni wengi. Nilipata kazi nikiwaacha solembe wenye shule na misonge yao:D:D:D:D:D:D
 
Huu uzi unapoelekea watakuja kina Joseph Musukuma kusema yaleyale.

Mnavyoonekana mnaweza kwenda mbali zaidi kusema hata elimu haina maana kisa kuna wachache waliosimama(kuridhika) kimaisha ambao hawana elimu kubwa mkasahau wengi wenye na walio swaafi.

Taifa lina vituko, haya malizeni kwanza ya Tiefuefu na Simba/Yanga afu mgeukie tena elimu na uelewa wa watu wenu.
 
Acheni kujustify low performance wazee...Kama mtu anaweza kusoma akapata alama za juu afanye hivyo,hayo ya ajira ni majaaliwa tu.Kuna wenye low grades za darasani wengi sana wako mtaani kutokana na grades zao maana pia kuna ajira nyingi tu zinatolewa kwa kigezo cha grade za ufaulu so wewe kupata ajira kwa ufaulu wa chini sio kuwa ndio standard ya maisha.Always be the best on what you do.
 
10 Reactions
Reply
Back
Top Bottom