Wanafunzi 79 wa Kenya hadi sasa wameondolewa Ukraine kufuatia uvamizi wa Urusi

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,811
4,533
1646212735297.png

Wanafunzi 79 wa Kenya hadi sasa wameondolewa Ukraine kufuatia uvamizi wa Urusi.

Serikali ya Kenya inasema mwanafunzi mmoja tayari ameshawasili Kenya, wengine 74 wako Poland, wawili wako Romania na wawili wako Hungary.

Mamlaka zinaendelea kuratibu uhamishaji wa wanafunzi wengine wengi kutoka miji mbalimbali nchini Ukraine ili kuwaondoa.

Wanafunzi wanne wa Kenya wameelezea nia yao ya kutoondoka Ukraine, wakitaja kwa sababu za kibinafsi.

Wanafunzi kutoka Afrika wameungana na raia wa Ukraine kuondoka nchini humo baada ya uvamizi wa Urusi.

Kulikuwa na wasiwasi wa ubaguzi wa rangi katika vituo vya mpakani na Umoja wa Afrika umezitaka nchi kuheshimu sheria za kimataifa na kuwasaidia wale wote wanaokimbia vita.

BBC Swahili
 
Back
Top Bottom