Wanafunzi 7 wafariki baada ya kuanguka kutoka ghorofa ya nne nchini Bolivia

Sam Gidori

Senior Member
Sep 7, 2020
165
414
Takriban wanafunzi saba wamefariki dunia na wengine watano wamejeruhiwa vibaya baada ya kuanguka kutoka ghorofa ya nne kufuatia kuvunjika kwa chuma kilichokuwa katika korido katika Chuo Kikuu cha El Alto kilichopo karibu na mji mkuu wa Bolivia, La Paz.

Video za tukio hilo zinawaonesha wanafunzi wakisukumana kuingia katika ukumbi kabla ya chuma hicho kuvunjika na kusababisha baadhi yao kuanguka.



Waziri Mambo ya Ndani amesema waliofariki wana umri kati ya miaka 20 na 24, akiagiza uchunguzi wa tukio hilo.

Chanzo: Al Jazeera
 
Back
Top Bottom