Wanafunzi 400 uhasibu wakwama kwa Msolla

Zee la shamba

Member
Oct 17, 2007
55
3
WANAFUNZI wapatao 400 wa Chuo cha Uhasibu Arusha wako hatarini kufukuzwa masomo baada ya Wizara ya Elimu ya Juu, Sayansi na Teknolojia, kuwathibitishia kuwa hawawezi kupata mkopo wa Bodi ya Mikopo, kwa vile hawana sifa.


Juzi wanafunzi hao walikwenda Dodoma kuonana na Waziri Peter Msolla ambaye aliwaeleza hana uwezo wa kutengua uamuzi uliokwisha kufanywa na mamlaka za juu.


Wanafunzi hao walikwenda kuanza masomo baada ya majina yao kuorodheshwa kwenye tovuti ya bodi ya mikopo ya elimu ya juu kuonyesha kuwa baada ya kufanyiwa tathmini ya uwezo wa uchumi watapewa mkopo na kutajwa asilimia wanayostahili kupewa.


Lakini baada ya kufika chuoni na kuanza kufuatilia mkopo huo, Bodi iliwaeleza kuwa ingawa wamefanyiwa tathmini ya uwezo wao wa uchumi, hawawezi kukopeshwa kutokana na kutokuwa na sifa. Moja ya vigezo ni kutokuwa na alama ya daraja la kwanza au la pili, wengi wao wana daraja la tatu katika mtihani wa kidato cha sita.


Baada ya kutoridhika na majibu hayo ya bodi, wanafunzi hao walituma wawakilishi wapatao 76 kwenda kwa Waziri Msolla aone namna ambavyo anaweza kuwasaidia. Lakini majibu ya waziri huyo jana yanaonyesha kuwakatisha tamaa wanafunzi hao.


Akizungumza jana, Rais wa serikali ya wanafunzi wa chuo hicho, Erick Gabriel, alithibitisha kuwa Profesa Msolla aliwaambia kuwa bajeti iliyopo haikidhi kuwakopesha wanafunzi waliopata daraja la tatu badala yake aliwaambia kuwa wenye sifa ni wale waliopata daraja kuanzia la pili.


“Tulimwomba atusaidie ili wanafunzi hawa wasifukuzwe masomo, lakini amesema hana uwezo huo, kwa vile tayari serikali imepitisha sera hiyo,” alisema Gabriel.


Kutokana na hali hiyo, Gabriel alisema wanamwomba Waziri Mkuu, Edward Lowassa na Rais Jakaya Kikwete waingilie kati suala hilo, waone namna ambavyo watawasaidia wanafunzi hao ili wasifukuzwe masomo yao.


Alisema wanafunzi hao hawakufanya makusudi, bali tangazo la kwenye tovuti ndilo lililowapa matumaini na hivyo wakaona kuwa wamebahatika kupata mkopo huo. Alisema wengi wa wanafunzi hao wametoka mikoani na wazazi wao hawana uwezo wa kuwasomesha.


Gabriel alisema kutokana na utata uliojitokeza, Profesa Msolla aliahidi kuwa katika mwaka ujao watahakikisha usumbufu wa namna hiyo haujitokezi.


Kwa mujibu wa taratibu za Bodi ya Mikopo, wanafunzi ambao wana sifa za kupewa mkopo bila kujali madaraja yao ni wale wanaosomea udaktari, ualimu na fani nyingine za sayansi.


Lengo la kutoa ahueni kwa watu wanaosomea fani hizo ni kuhamasisha wanafunzi zaidi ili fani hizo zenye upungufu wa wataalamu ziweze kukidhi mahitaji yaliyopo.


Lakini wanafunzi wengine wanaosoma fani za sanaa, sheria, uhasibu watapewa mkopo huo tu kama
 
Msola Must go Out,Anshindwa vipi kumshauri RAis Apunguze Safari ili pesa wapewe Wanafunzi hawa ?
Mie nawashauri hawa wanafunzi waandamane na Mabango leo wakati waziri wa Fedha wa Marekani atakopokuwa Arusha,wamueleze usumbufu wanaoupata kutoka kwa serikali wakitaka pesa za mikopo huku zinatolewa na wahisani. anaweza kumuuliza Muungwana kwanini hajawapa pesa,Mie najua Msola ndio anamalizia kazi,
Plan B,Najua huyu waziri ataendelea kuwapo mpaka kesho,Nawashauri hawa wanafunzi wafanye utaratibu wa kumuona.
 
sheria hiyo ya bodi ya mikopo ni kinyume cha Katiba. Katika Ibara ya 13:2 Katiba inasema:

(2) Ni marufuku kwa sheria yoyote iliyotungwa na mamlaka
yoyote katika Jamhuri ya Muungano kuweka sharti lolote ambalo
ni la ubaguzi ama wa dhahiri au kwa taathira yake
.

Sasa hiyo inaweza kueleweka vizuri ukisoma na kipengele kifuatacho cha Katiba:

Ibara 11:
(2) Kila mtu anayo haki ya kujielimisha, na kila raia
atakuwa huru kutafuta elimu katika fani anayopenda hadi kufikia
upeo wowote kulingana na stahili na uwezo wake.
(3) Serikali itafanya jitihada kuhakikisha kwamba watu
wote wanapata fursa sawa na za kutosha kuwawezesha kupata
elimu na mafunzo ya ufundi katika ngazi zote za shule na vyuo
vinginevyo vya mafunzo.


sasa ni nani huyo aliyekuja na wazo la kusema kuwa ukiwa na daraja la tatu basi hustahili elimu na sheria ikubague?
 
mkjj,
hilijambo tumelijadili sana bila mafanikio,na kama katiba ndio inasema hivyo kwa nini hivi vyama vya wanafunzi wasifungue kesi mahakamani ilikudai haki yao ya kikatiba.
Mnyika uko wapi kuhamasisha ilisuala liwezekupatiwa ufumbuzi.
 
Hapo Uhasibu Kuna Watu Wanasoma Advanced Diploma Za Computer Science Na Information Tecknology Na Wao Bado Hawajapata Fedha Yoyote Toka Bodi Japokuwa Bodi Ilisema Ndo Vipaumbele Katika Fani Za Sayansi Na Teknolojia Vile Vile Watu Wa Mwaka Wa Pilim Bodi Iliwatangazia Kutuma Maombi Ya Kuomba Mkopo Ikiwa Ni Pamoja Na Kulipia Fomu Ya Loan Board Tsh10000 Wengi Wakiwa Ni Wanaosoma It Na Computer Science Lakini Mpaka Sasa Hawajapata Pesa Yoyote Japokuwa Wanasoma Kprogram Ambazo Zimo Katika Vipaumbele
 
WANAFUNZI wapatao 400 wa Chuo cha Uhasibu Arusha wako hatarini kufukuzwa masomo baada ya Wizara ya Elimu ya Juu, Sayansi na Teknolojia, kuHwathibitishia kuwa hawawezi kupata mkopo wa Bodi ya Mikopo, kwa vile hawana sifa.


Juzi wanafunzi hao walikwenda Dodoma kuonana na Waziri Peter Msolla ambaye aliwaeleza hana uwezo wa kutengua uamuzi uliokwisha kufanywa na mamlaka za juu.


Wanafunzi hao walikwenda kuanza masomo baada ya majina yao kuorodheshwa kwenye tovuti ya bodi ya mikopo ya elimu ya juu kuonyesha kuwa baada ya kufanyiwa tathmini ya uwezo wa uchumi watapewa mkopo na kutajwa asilimia wanayostahili kupewa.


Lakini baada ya kufika chuoni na kuanza kufuatilia mkopo huo, Bodi iliwaeleza kuwa ingawa wamefanyiwa tathmini ya uwezo wao wa uchumi, hawawezi kukopeshwa kutokana na kutokuwa na sifa. Moja ya vigezo ni kutokuwa na alama ya daraja la kwanza au la pili, wengi wao wana daraja la tatu katika mtihani wa kidato cha sita.


Baada ya kutoridhika na majibu hayo ya bodi, wanafunzi hao walituma wawakilishi wapatao 76 kwenda kwa Waziri Msolla aone namna ambavyo anaweza kuwasaidia. Lakini majibu ya waziri huyo jana yanaonyesha kuwakatisha tamaa wanafunzi hao.


Akizungumza jana, Rais wa serikali ya wanafunzi wa chuo hicho, Erick Gabriel, alithibitisha kuwa Profesa Msolla aliwaambia kuwa bajeti iliyopo haikidhi kuwakopesha wanafunzi waliopata daraja la tatu badala yake aliwaambia kuwa wenye sifa ni wale waliopata daraja kuanzia la pili.


“Tulimwomba atusaidie ili wanafunzi hawa wasifukuzwe masomo, lakini amesema hana uwezo huo, kwa vile tayari serikali imepitisha sera hiyo,” alisema Gabriel.


Kutokana na hali hiyo, Gabriel alisema wanamwomba Waziri Mkuu, Edward Lowassa na Rais Jakaya Kikwete waingilie kati suala hilo, waone namna ambavyo watawasaidia wanafunzi hao ili wasifukuzwe masomo yao.


Alisema wanafunzi hao hawakufanya makusudi, bali tangazo la kwenye tovuti ndilo lililowapa matumaini na hivyo wakaona kuwa wamebahatika kupata mkopo huo. Alisema wengi wa wanafunzi hao wametoka mikoani na wazazi wao hawana uwezo wa kuwasomesha.


Gabriel alisema kutokana na utata uliojitokeza, Profesa Msolla aliahidi kuwa katika mwaka ujao watahakikisha usumbufu wa namna hiyo haujitokezi.


Kwa mujibu wa taratibu za Bodi ya Mikopo, wanafunzi ambao wana sifa za kupewa mkopo bila kujali madaraja yao ni wale wanaosomea udaktari, ualimu na fani nyingine za sayansi.


Lengo la kutoa ahueni kwa watu wanaosomea fani hizo ni kuhamasisha wanafunzi zaidi ili fani hizo zenye upungufu wa wataalamu ziweze kukidhi mahitaji yaliyopo.


Lakini wanafunzi wengine wanaosoma fani za sanaa, sheria, uhasibu watapewa mkopo huo tu kama
Haya majanga yalianzishwa na ile Timu yetu ya Boyz Two Men
 
sheria hiyo ya bodi ya mikopo ni kinyume cha Katiba. Katika Ibara ya 13:2 Katiba inasema:



Sasa hiyo inaweza kueleweka vizuri ukisoma na kipengele kifuatacho cha Katiba:

Ibara 11:
(2) Kila mtu anayo haki ya kujielimisha, na kila raia
atakuwa huru kutafuta elimu katika fani anayopenda hadi kufikia
upeo wowote kulingana na stahili na uwezo wake.
(3) Serikali itafanya jitihada kuhakikisha kwamba watu
wote wanapata fursa sawa na za kutosha kuwawezesha kupata
elimu na mafunzo ya ufundi katika ngazi zote za shule na vyuo
vinginevyo vya mafunzo.


sasa ni nani huyo aliyekuja na wazo la kusema kuwa ukiwa na daraja la tatu basi hustahili elimu na sheria ikubague?

Nahitaji kufahamu kama huu uzalendo bado upo.
 
Back
Top Bottom