Wanafunzi 18000 wa kidato cha 3 hawajui kusoma na kuandika-nani alaumiwe?

engmtolera

JF-Expert Member
Oct 21, 2010
5,150
1,437
Haya wadau
mkoa wa pwani unawanafunzi zaidi ya elfu 18 wa shule ya msingi na sekondary wa kidato cha 3,hawajui kusoma na kuandika je
nani wakulaumiwa hapo?

kwa upande wangu mimi nailaumu serikali kwani nimekuwa mwalimu wa fizikia na hisabati huko malinyi ulanga,nimekumbana na matatizo mengi sana na haya yote yanasababisha na sera mbovu zilizowekwa na kulazimishwa ziwepo ktk elimu yetu,

1. tunalazimisha wanafunzi wote waliomaliza darasa la saba wajiunge na sekondary hata kama mwanafunzi huyo hajui kusoma wala kuandika
na shule zinazofelisha mala nyingi zimekuwa zikipewa adhabu.

2.Kuondoa adhabu za viboko kwa wanafunzi kiasi kwamba mwanafunzi yupo huru kufanya lolote lile atakalo, mliopo nje ya system ya ualimu hamuoni tatizo lakini tuliokuwepo humo hili ni tatizo kubwa sana,

3.Serikali imeondoa mitihani ya kidato cha pili na hata kama ipo mwanafunzi haruhusiwi kurudia darasa hata kama akiferi,hii imeondoa nguvu ya wanafunzi kusoma na wanafanya bora liende tu wamalize kidato cha nne

4.Pia serikali imeondoa mtihani wa darasa la nne kama ulivyokuwa zamani huu wa sasa hata ukiferi ni lazima usonge mbele

5.Ktk shule za kata mamlaka yapo chini ya kata husika kiasi kwamba inakuwa ni vigumu kwa viongozi wa kata kufuatilia maendleo ya shule husika kutokana na viongozi hao kuwa na upeo tofauti wa uelewa kuhusu elimu na kutingwa na mambo mengi nje ya kusimamia shule za kata

6. Maslahi ya walimu kutokutiliwa mkazo na kuwafanya walimu hao kuona kuwa ualimu ni kazi yakitumwa zaidi ukilinganisha na kzi nyingine

Yapo mengi sana matatizo yanayopelekea tuwe na idadi kubwa ya wasiojua kusoma na kuandika kubwa zaidi ni

kutaka kuwaonyesha wananchi na watoa misaada kuwa tumeweza kuingiza wanafunzi wengi shule ya msingi,wote wamefauru kwenda sekondari na wote wamemaliza sekondari,pasipo kuangalia mwisho wa siku tunazalisha wasomi watakao kuja kuididimiza nchi hii na kuimaliza kabisa
 
Tatizo ni kwamba walimu wapo kwenye mgomo siku nyingi sanaaa. ndo mana wanafunzi wengi hawajui kusoma. usione wanakwenda kazini lakini hawafundishi kabisa sababu ni mishahara midogo na malimbikizo ma madai yao. habari kamili uliza cwt.
 
Tatizo ni kwamba walimu wapo kwenye mgomo siku nyingi sanaaa. ndo mana wanafunzi wengi hawajui kusoma. usione wanakwenda kazini lakini hawafundishi kabisa sababu ni mishahara midogo na malimbikizo ma madai yao. habari kamili uliza cwt.

sikubaliani na hili,kwani tatizo hili la kupata wanafunzi wasiojua kusoma na kuandika imeanza tu baada ya kuondoa mitihani ya Darasa la nne,na kuingiza sera za kuandikisha wanafunzi wengi kwa mkupuo kwa lengo la kuwa na wanafunzi wengi wanaomaliza Darasa la saba na kuingia Sekondari

walimu wamekuwa na moyo sana wa kufundisha ingawaje wanamatatizo mengi moja wapo likiwa hilo ulilolitaja

sera mbovu ktk elimu yetu bado ni tatizo mkuu
 
sikubaliani na hili,kwani tatizo hili la kupata wanafunzi wasiojua kusoma na kuandika imeanza tu baada ya kuondoa mitihani ya Darasa la nne,na kuingiza sera za kuandikisha wanafunzi wengi kwa mkupuo kwa lengo la kuwa na wanafunzi wengi wanaomaliza Darasa la saba na kuingia Sekondari

walimu wamekuwa na moyo sana wa kufundisha ingawaje wanamatatizo mengi moja wapo likiwa hilo ulilolitaja

sera mbovu ktk elimu yetu bado ni tatizo mkuu

Engineer!

Mtihani wa Darasa la nne umeondolewa mwaka gani?

Mimi nakubaliana na MWL MTZ - Walimu wa shule za Serikali walishaacha kufundisha zaidi ya miaka 6 iliyopita! Walimu (kwenye shule za umma) hawafundishi bali uenda ku-sign na kusoma magazeti na kupiga soga... Halafu siku za mwisho wa wiki wanafundisha "tuition" wanafunzi wale wale ambao wamekuwa nao juma zima!

Tuition inalipiwa sh 200-500 kwa kila mwanafunzi ... then ... wanafunzi wakifanya mazoezi baada ya tuition ... walimu wanawaambia wasahishane wenyewe!

Katika sector ya Elimu (Msingi & Secondary) kumekufa kabisa wanasubiri kuanua matanga!
 
Engineer!

Mtihani wa Darasa la nne umeondolewa mwaka gani?

Mimi nakubaliana na MWL MTZ - Walimu wa shule za Serikali walishaacha kufundisha zaidi ya miaka 6 iliyopita! Walimu (kwenye shule za umma) hawafundishi bali uenda ku-sign na kusoma magazeti na kupiga soga... Halafu siku za mwisho wa wiki wanafundisha "tuition" wanafunzi wale wale ambao wamekuwa nao juma zima!

Tuition inalipiwa sh 200-500 kwa kila mwanafunzi ... then ... wanafunzi wakifanya mazoezi baada ya tuition ... walimu wanawaambia wasahishane wenyewe!

Katika sector ya Elimu (Msingi & Secondary) kumekufa kabisa wanasubiri kuanua matanga!

Yaani huelewi kuwa mtihani wa sasa wa Darasa la nne upo tofauti na ule tuliofannya sisi zamani? hujui kuwa mwanafunzi wa darasa nne akiferi sasa hivi anaruhusiwa kuendelea na darasa la tano?
fikilia kuwa kijana huyo kapitishwa bila kupingwa kuendelea na darasa la 5 unategemea nini mbele ya safari,ukizingatia tena wanafunzi wote wanatakiwa kupita bila kupingwa kuingia sekondari na elewa kuwa mtuhani wa kidato cha pili haumzuii mwanafunzi kurudia darasa,kwa hiyo ulemwendelezo wa kumpata kujana asiyejua kusoma na kuandika unaendelea hadi amalizapo kidato cha nne
 
Shukrani kwa serikali ya awamu ya 4, imeweza kujenga shule kilakata na sasa kila mwanafunzi anakwenda shule, au mnataka nini zaidi?! Kwani sisi watanzania shida yetu si shule bwana! Haya mambo ya kufaulu na kujua kusoma ni anasa tu.

Hata hili la mchakato wa katiba nalo lipo hivyo hivyo. Sisi shida yetu ni kutoa maoni tu. Kama yatafanyiwa kazi au kuwekwa tu si shida yetu. Ndio maana hata hotuba ya Mh. Dokta alipoongea na wacheza bao wa dar ilitosha kumaliza kiu yetu. Mkumbuke Mh. Dokta alisema wote tutatoa maoni, sasa kazi kwenu mnaotaka maoni yenu yafanyiwe kazi.

Juzi waziri alikuwa anajisifia kuwa ni Tanzania pekee ndio imefanikiwa kupeleka sekondari 80% ya wahitimu wa darasa la saba. Nichukue nafasi hii kutoa pongezi kwa Mh. Dokta na serikali yake kwa kukuza idadi ya wahitimu.
 
Yaani huelewi kuwa mtihani wa sasa wa Darasa la nne upo tofauti na ule tuliofannya sisi zamani? hujui kuwa mwanafunzi wa darasa nne akiferi sasa hivi anaruhusiwa kuendelea na darasa la tano?
fikilia kuwa kijana huyo kapitishwa bila kupingwa kuendelea na darasa la 5 unategemea nini mbele ya safari,ukizingatia tena wanafunzi wote wanatakiwa kupita bila kupingwa kuingia sekondari na elewa kuwa mtuhani wa kidato cha pili haumzuii mwanafunzi kurudia darasa,kwa hiyo ulemwendelezo wa kumpata kujana asiyejua kusoma na kuandika unaendelea hadi amalizapo kidato cha nne


Engineer,

Nadhani sikuelewi!

Kwanza, Mimi sijawahi kuafanya mtihani wa darasa la nne - nilianza darasa la kwanza najua kusoma na kuandika mwaka 1975 - hatukuwa na mtihani wa Darasa la nne!

Pili, Kujua kusoma na kuandika haitegemei mtoto amefanya mitihani mingapi bali inategemea mtoto amefundishwa na kufahamu, hata kama hajawahi kufanya mtihani - nadhani unakumbuka Elimu ya Watu Wazima kwenye miaka ya 70-80 - hawa hawakuwa na mitihani bali walifundishwa na kufahamu kusoma na kuandika ...

The bottom line is - Siku hizi watoto hawafundishwi (kwa sababu walimu hawapendi kufundisha), on top of that walimu wengi ni wale waliopata "credit" za chini katika masomo ya O- or High- Level!
 
Engineer,

Nadhani sikuelewi!

Kwanza, Mimi sijawahi kuafanya mtihani wa darasa la nne - nilianza darasa la kwanza najua kusoma na kuandika mwaka 1975 - hatukuwa na mtihani wa Darasa la nne!

Pili, Kujua kusoma na kuandika haitegemei mtoto amefanya mitihani mingapi bali inategemea mtoto amefundishwa na kufahamu, hata kama hajawahi kufanya mtihani - nadhani unakumbuka Elimu ya Watu Wazima kwenye miaka ya 70-80 - hawa hawakuwa na mitihani bali walifundishwa na kufahamu kusoma na kuandika ...

The bottom line is - Siku hizi watoto hawafundishwi (kwa sababu walimu hawapendi kufundisha), on top of that walimu wengi ni wale waliopata "credit" za chini katika masomo ya O- or High- Level!
[NI KWELI WALIMU HAWANA KHALI YA KUFUNDISHA KABISA WENGI WAPO KWENYE MIRADI YAO WAKATI WA VIPINDI. swala la"credit" za chini katika masomo ya O- or High- Level ni uongo kwani hao hao ndio waliokuwa wanafundisha na wanafunzi wanafauru. ]
 
Tunatakiwa tuwe na lengo kuhusu elimu kwa miaka 50 sio Kila waziri anakuja na system yake,hapana hii haikubaliki hata kidogo ndio sababu kuyumbishwa huku,laiti tungeamua na kuikomalia hata ile elimu ya mkoloni tuisimamie kwa makini Basi mpaka Leo tungekuwa mbali sana,kuliko haya mabadiliko yasiyoeleweka Kila waziri anakuja na system yake camon guys! Badilikeni
Nalog off
 
Back
Top Bottom