Wanafunz 8 waliokamatwa gesti Dodoma ni wagen wa Kawambwa

Bajabiri

JF-Expert Member
Jan 1, 2011
9,730
1,201
Wanafunz 8 ambao walikamatwa na Polis wakiwa wamelala kwenye nyumba ya kulala wagen ya Vatican huko mkoani dodoma inasemekana kuwa walikuwa ni wageni wa waziri wa Elim dr Kawambwa,,,,,,,,,

Wanafunz hao ambao wengine ni viongoz wa serikali ya Wanafunz wa chuo cha Ustawi wa jamii wanasema kuwa wao walikwenda Dodoma kwa lengo la kumuona wazir ili kujadili mustakabal wa Matatzo ya wana USTAWIIII.......
 
Mod muvizisha hii post kwenye post ya jana ili watu wajadili kwa uhalisia.,inasikitisha kuwa wachangiaji wengi waliwatuhumu hawa watoto wetu kuwa they were for udultery.
 
nilitaka nikuambie kipo chini ya wizara ya nishati na madini.sema nimepoteza kwa kuwa nakuheshimu sana.habari yako bana.
Kwa kifupi CBE,CCP,Ustawi,Uhazili na baadhi ya Shule za Msingi na Seekondari havipo kwenye wizara ya elimu... Habari yako binafsi Kiongozi...
 
wale vijana walienda kumuona waziri wa afya na wa elimu wote wanahusika pale,hawakuwa na mambo mabaya kama watu wanavyotaka kuwa hukumu,swala liko hivi wakati chuo kinafungwa na viongozi wababe,wanafunzi walipitisha azimio la kutaka kujua hatma yao,iliundwa kamati ambayo ilipewa jukumu la kumuona waziri mkuu, waziri wa afya na waziri wa elimu ilikujua hatma yao,serikali ya wanafunzi waliahidi kutoa pesa za safari hiyo,lkn mwishoni walichomoa kutoa hiyo pesa, na sababu hazijulikani hivyo watu walipigiwa simu kuombwa kuchangia,hivyo ilipatikana pesa kidogo ambayo waliondoka nayo,nafikiri ili kubana matumizi ndiko kulikopelekea kuchukua chumba kimoja,na ukiangalia kiongozi ni mmoja tu maana raisi yuko upande wa uongozi cha kushangaza hatakwenye vikao vya chuo anaingia sasa hapa sijui kama nani! wakipanga hili kesho anajeuka,mimi ushauri wangu serikali iingilie kati iokoe watoto wanaohangaika huku mitaana maana kodi za vyumba ilishaisha tangu mwezi wa sita ambapo walitarajia kumaliza,wasichana wanadhalilika sana mtaani hawana pesa wazazi wao ndo hao wakulima waliozuiwa kuuza mazao yao,jamani naomba kama yupo mwenye uwezo awasidie hao vijana hapo dodoma waweze kuwaona hao viongozi
 
Aksanteni kwa Updates silaumu waliowalaumu hawa wanachuo kwani kiukweli kilichofanyika si cha kawaida katika hali ya kawaida.Tuwalaumu waandishi wetu wanaoandika habari nusu nusu pengine wangewahoji wakabalansisha habari yao comment zingekuwa tofauti!
 
Back
Top Bottom