Wanadamu tunazibiana ridhiki

Rweye

JF-Expert Member
Mar 16, 2011
16,958
7,512
1. Hivi sisi wanaume kama tukiamua kwa sauti moja tukaamua kuwasaidia akina dada na wamama kweli tunashindwa?

2. Ni kwanini tuwe na wasichana wengi mtaani wasioolewa japo wanaitaji wa kuwaoa badala yake tunakuwa wabinafsi mno eti mke mmoja mmoja angali tungewakubalia kuwaoa wengi wengi wangefurahi na kuruka ruka?

3. Ni wapi kwenye Biblia imeandikwa idadi fulani kwamba ni lazima uoe mwanamke mmoja tu, na ni nani kwenye Biblia aliyehadhibiwa kwasababu ya kuoa wanawake wengi?

4. Tumewaona akina Daudi, Sulemani, Yakobo, Isaka n.k wengi wao walioa wanawake wengi tu, ila ni wapi imeandikwa Mungu aliwalaani kisa wameoa wanawake wengi?

5. Sasa bora kipi kwa Mungu, yaani kati ya polygamism na homosexuality? tunajua Mungu aliiharibu Sodoma si kwasababu ya polygamism bali kwasababu ya homosexuality. Alafu Mungu kasema tuzae tuwe wengi kama nyota, hivi tunaijaza dunia kwa kuoa mke mmoja?

6. Najua sote tunafanana na Mungu, tumetoka kwenye mavumbi na huwa tunarudi pia kupitia mavumbi, kwa maana hiyo sote ni sawa! Sasa inakuwaje linapokuja suala la kuoa tunaonekana wa tofauti ilhari sote tu wa Mungu mmoja?

7. Ni kwanini iwe sawa fulani kuoa wake wanne alafu iwe kosa kwa mwingine, hivi sote si wa Mungu mmoja? sasa iweje tukataze zaidi polygamism na badala yake tushadadie homosexuality, hivi kwa Mungu ni hipi dhambi hasa?

Tuache kujichanganya, wazungu wanatuchezea kama midori. Kuliko kuwa na wasichana kibao wasioolewa lakini wanashinda wanakwapua wa wenzao na huku kiukweli tunawatamani, ni bora tukawaoa ilimradi uweze kuwatunza, tujaribu kubalansi mahitaji na malengo ya Mungu, tuache ubinafsi wakati wengine wakitahabika na ndo maana wanaamua hata kulambana wao kwa wao. Yangu ndo hayo kwa leo.
 
Kwa waislam mwisho wanne ila kipindi kingne wanawake ndio kikwazo kuwa zaidi ya mmoja ni vita kwao utakoma.
 
Kwa waislam mwisho wanne ila kipindi kingne wanawake ndio kikwazo kuwa zaidi ya mmoja ni vita kwao utakoma.
Teh, teh, teh!! wanawake wabinafsi mno, wanabaniana ridhiki wakati sie tumejitoa kuwasaidia. Alafu hawatambui anayekukatalia usimwongeze ndo yule yule anayemnyima yeye nyama na maini hapo ndani, sasa si bora akakubali tu.
 
Teh, teh, teh!! wanawake wabinafsi mno, wanabaniana ridhiki wakati sie tumejitoa kuwasaidia. Alafu hawatambui anayekukatalia usimwongeze ndo yule yule anayemnyima yeye nyama na maini hapo ndani, sasa si bora akakubali tu.
hapo kwenye red,ina maana hili neno "Alafu" ndio limeshakua mbadala wa "Halafu?" Nauliza tu....
 
MIE HUYO 1 NATAKAA ANIFYONYE NIMUACHE WE UNA PLAN KUOWA 10 NA USAWA HUU MBONI HAMFIKILII KUNDA HATA KIKOMBE CHA SHABA KWA KNYWEA MAJI TU NA SHABA TUNACHIMBA WENYEWE AFRICA
 
Back
Top Bottom