KIDUNDULIMA
JF-Expert Member
- Aug 18, 2010
- 966
- 537
Katika hali ya kushanganza chuo kikuu cha Dar es salaam kimewatangazia wanafunzi wanaotarajia kujiunga na chuo hicho kuja kuchukua admission letters kuanzia jumatatu ya leo (Tar. 18/10/2010). Tangazo hilo limewafanya wanafunzi watarajiwa walioko mikoani kumiminika dar kwa ajili ya kuchukuwa barua hizo, huku wengine wakiamini kuwa chuo kimeshafunguliwa. Ukweli ni kuwa chuo kitafunguliwa kuanzia 05/11/10, cha kushanganza ni kwa nini wawaite vijana mapema namna hii? Nani atagharamia nauli ya kwenda na kurudi mikoani mpaka chuo kitakapofunguliwa? nani atagaramia malazi na chakula? Kwa nini wasingetumiwa hizo barua huko huko waliko? au kwa nini wasingechukuwa hizo barua wakati wa orientation week?
Chuo kikuu Dar ni chuo kikongwe ambacho tunategemea kuwa kitafanya mambo yake kisomi bila kuwaingiza katika gharama zisizo za lazima watanzania wengi maskini. Cha kushangaza wanafanya mabo yao kama vile sio wasomi. UD mnaboa sometimes
Chuo kikuu Dar ni chuo kikongwe ambacho tunategemea kuwa kitafanya mambo yake kisomi bila kuwaingiza katika gharama zisizo za lazima watanzania wengi maskini. Cha kushangaza wanafanya mabo yao kama vile sio wasomi. UD mnaboa sometimes