Wanachuo wa mwaka wa mwaka watatu st joseph songea wagomea

ligendayika

JF-Expert Member
Aug 31, 2012
1,183
198
wanachuo wa mwaka wa tatu wa chuo cha mtakatifu Joseph songea wamegoma kufanya mtihani kwa madai ya kukatywa hela zao walizozipata toka bodi ya mikopo ya elimu ya juu. wanafunzi hao wanadai kiasi cha shilingi 105,000 kwani walistahili kupata sh 472,500 na wamepatiwa sh. 367,500. wanachuo hao walikwenda kwenye ofisi za mkuu wa wilaya kupata ufafanuzi wa hela hizo na mkuu wa wilaya aliwashauri wanachuo hao kuwatuma viongozi wao ili waongee na mkuu wa wilaya pili aliwashauri warudi chuoni na waendelee na taratibu zote za chu na mwisho viongozi wao waje na vielelezo vyote vinavyohusu madai yao. hata hivyo "kuu wa wilaya alowaambia kuwa swala lao alishaongea na mwakilishi wa bodi ya mikopo ili kujua tatizo. Jamani wa JF ebu tujadili tatizo ninini huko bodi ya mikopo ya elimu ya juu? Nawasilisha
 
Ni kweli kuna matatizo mengi ktk chuo hiki cha wahindi,wiki 2 zilizopita mwaka wa pili waligoma,leo hii mwaka wa tatu wamagoma hata kufanya mitihani,majina kuhusu hela ya kujikimu inaonyesha kwamba wametumia copy ya mwaka 2010 kitu ambacho kinaleta mkanganyiko Hatuelewi mchawi ni nani kati ya bodi ya mkopo au uongozi wa chuo,wenye tarifa zaidi watusadia maana hata kusign wanafunzi wamegoma
 
mkuu wa wilaya anasema kwamba alikutana na director wa chuo hotelini alikofikia huyo muhindi(director)kutatua matatizo yanazokabili chuo usiku wa jana.swali langu ni hili,kama issue ni official case kwanini wakutane hotelini?
angemuita ofisini mwake na si kama private issue alivyofanya mkuu huyu wilaya.jamani hawa wanachuo wanadai haki ya msingi
 
Ni kweli kuna matatizo mengi ktk chuo hiki cha wahindi,wiki 2 zilizopita mwaka wa pili waligoma,leo hii mwaka wa tatu wamagoma hata kufanya mitihani,majina kuhusu hela ya kujikimu inaonyesha kwamba wametumia copy ya mwaka 2010 kitu ambacho kinaleta mkanganyiko Hatuelewi mchawi ni nani kati ya bodi ya mkopo au uongozi wa chuo,wenye tarifa zaidi watusadia maana hata kusign wanafunzi wamegoma kufanya hivyo,elimu yao(wahindi) imeshuka sana






 
Issue ya mikopo haaina uhusiano na vyuo hivyo kugomea masomo kwa sababu ya mikopo ni kvunja sheria mnatakiwa mfukuzwe mara moja
 
Back
Top Bottom