ligendayika
JF-Expert Member
- Aug 31, 2012
- 1,183
- 198
wanachuo wa mwaka wa tatu wa chuo cha mtakatifu Joseph songea wamegoma kufanya mtihani kwa madai ya kukatywa hela zao walizozipata toka bodi ya mikopo ya elimu ya juu. wanafunzi hao wanadai kiasi cha shilingi 105,000 kwani walistahili kupata sh 472,500 na wamepatiwa sh. 367,500. wanachuo hao walikwenda kwenye ofisi za mkuu wa wilaya kupata ufafanuzi wa hela hizo na mkuu wa wilaya aliwashauri wanachuo hao kuwatuma viongozi wao ili waongee na mkuu wa wilaya pili aliwashauri warudi chuoni na waendelee na taratibu zote za chu na mwisho viongozi wao waje na vielelezo vyote vinavyohusu madai yao. hata hivyo "kuu wa wilaya alowaambia kuwa swala lao alishaongea na mwakilishi wa bodi ya mikopo ili kujua tatizo. Jamani wa JF ebu tujadili tatizo ninini huko bodi ya mikopo ya elimu ya juu? Nawasilisha