Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 17,871
- 33,235
Hivi sasa kuna fukuto kubwa miongoni mwa Waislamu kila unapofanywa uteuzi ndani ya Serikali wao huangalia kama kuna muislamu yeyote ameteuliwa. Mara nyingi huambulia patupu. Kwenye vyombo vya habari kama Gazeti la "Mizani" humo kina Sheikh Khalifa kwa juhudi kubwa kabisa hadi wamefikia kuchapisha majina ya waislamu ambao wanadhani wana sifa ya kuteuliwa kwenye teuzi zinazofanywa lakini hawateuliwi.
Mimi si muumini wa siasa au maisha kwa kuangalia vigezo vya dini ya mtu, lakini kama ipo dhana ya dini au kundi fulani la watu katika jamii linaona kama linabaguliwa ni vema jambo lenyewe likafanyiwa kazi. Ni kweli kwamba waislamu wanabaguliwa kwenye nchi hii na chanzo cha kubaguliwa kwao ni nini na anayewabagua ni nani?
CCM ni zao la TANU na ASP, kwa maana nyingine vyama hivyo viwili ndiyo asili ya CCM. Hapa hatuwezi kuijadili ASP kwa kuwa kwa muktadha wa mada hii yenyewe moja kwa moja haifai kujadiliwa. Mara baada ya Uhuru kulikuwa na vyama vingi vya siasa mpaka pale vilipopigwa Marufuku na TANU mwaka 1965. Jee waislamu waliunga mkono chama gani kati ya TANU na hivyo vingine?
Miaka 27 baadaye mwaka 1992 mfumo wa vyama vingi ulirejeshwa hapa nchini na CCM iliyozaliwa kwa kuunganisha vyama vya ASP na TANU, nayo ikajivika uhai kabla haijazaliwa kisheria. Tangu hapo hadi sasa nchi yetu imekuwa inafuata mfumo wa vyama vingi vya siasa. Jee kwa kipindi chote hicho waislamu unapofika wakati wa uchaguzi huunga mkono chama gani cha siasa kama si CCM?
Kwa nini kina Sheikh Khalifa na kina Mohamed Said huwa siwasikii wakisema chama kinachosababisha wao wabaguliwe ni CCM kwa kuiga tabia ile ile ya TANU badala yake wanazungumza kiujumla kwamba wanabaguliwa? Kama Serikaili ndiyo inawabagua waislamu na kuwapendelea wakristo hiyo serikali inatokana na chama gani cha siasa kama si hapo awali na TANU na sasa CCM?
Hao wanaoleta Orodha ndeefu za wasomi wa kiislamu ili wateuliwe na Magufuli mwaka jana walikiunga mkono chama gani kama si CCM? Sheikh Khalifa anasema kuwa wao walimuunga mkono Magufuli kwa kuwa hakuchangiwa na wafanyabiashara kwenda Ikulu. Hilo analisema kama ni ukweli anaousimamia ama kama ni Kada wa CCM kushabikia kauli ya Mwenyekiti wake Taifa kwamba hakuchangiwa na wafanyabiashara?
Waislamu wa nchi hii wakiongozwa na kina Sheikh Khalifa na BAKWATA kosa lao kubwa ni kuiamini CCM ambayo mwisho wa siku ikiunda serikali, wao huja kulalamika kwamba inawabagua kwenye kila nyanja ya maisha. Kosa ni lao wala si la CCM!
Mimi si muumini wa siasa au maisha kwa kuangalia vigezo vya dini ya mtu, lakini kama ipo dhana ya dini au kundi fulani la watu katika jamii linaona kama linabaguliwa ni vema jambo lenyewe likafanyiwa kazi. Ni kweli kwamba waislamu wanabaguliwa kwenye nchi hii na chanzo cha kubaguliwa kwao ni nini na anayewabagua ni nani?
CCM ni zao la TANU na ASP, kwa maana nyingine vyama hivyo viwili ndiyo asili ya CCM. Hapa hatuwezi kuijadili ASP kwa kuwa kwa muktadha wa mada hii yenyewe moja kwa moja haifai kujadiliwa. Mara baada ya Uhuru kulikuwa na vyama vingi vya siasa mpaka pale vilipopigwa Marufuku na TANU mwaka 1965. Jee waislamu waliunga mkono chama gani kati ya TANU na hivyo vingine?
Miaka 27 baadaye mwaka 1992 mfumo wa vyama vingi ulirejeshwa hapa nchini na CCM iliyozaliwa kwa kuunganisha vyama vya ASP na TANU, nayo ikajivika uhai kabla haijazaliwa kisheria. Tangu hapo hadi sasa nchi yetu imekuwa inafuata mfumo wa vyama vingi vya siasa. Jee kwa kipindi chote hicho waislamu unapofika wakati wa uchaguzi huunga mkono chama gani cha siasa kama si CCM?
Kwa nini kina Sheikh Khalifa na kina Mohamed Said huwa siwasikii wakisema chama kinachosababisha wao wabaguliwe ni CCM kwa kuiga tabia ile ile ya TANU badala yake wanazungumza kiujumla kwamba wanabaguliwa? Kama Serikaili ndiyo inawabagua waislamu na kuwapendelea wakristo hiyo serikali inatokana na chama gani cha siasa kama si hapo awali na TANU na sasa CCM?
Hao wanaoleta Orodha ndeefu za wasomi wa kiislamu ili wateuliwe na Magufuli mwaka jana walikiunga mkono chama gani kama si CCM? Sheikh Khalifa anasema kuwa wao walimuunga mkono Magufuli kwa kuwa hakuchangiwa na wafanyabiashara kwenda Ikulu. Hilo analisema kama ni ukweli anaousimamia ama kama ni Kada wa CCM kushabikia kauli ya Mwenyekiti wake Taifa kwamba hakuchangiwa na wafanyabiashara?
Waislamu wa nchi hii wakiongozwa na kina Sheikh Khalifa na BAKWATA kosa lao kubwa ni kuiamini CCM ambayo mwisho wa siku ikiunda serikali, wao huja kulalamika kwamba inawabagua kwenye kila nyanja ya maisha. Kosa ni lao wala si la CCM!