Wanachokosea ni kuendelea kuiamini CCM!!

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
17,871
33,235
Hivi sasa kuna fukuto kubwa miongoni mwa Waislamu kila unapofanywa uteuzi ndani ya Serikali wao huangalia kama kuna muislamu yeyote ameteuliwa. Mara nyingi huambulia patupu. Kwenye vyombo vya habari kama Gazeti la "Mizani" humo kina Sheikh Khalifa kwa juhudi kubwa kabisa hadi wamefikia kuchapisha majina ya waislamu ambao wanadhani wana sifa ya kuteuliwa kwenye teuzi zinazofanywa lakini hawateuliwi.

Mimi si muumini wa siasa au maisha kwa kuangalia vigezo vya dini ya mtu, lakini kama ipo dhana ya dini au kundi fulani la watu katika jamii linaona kama linabaguliwa ni vema jambo lenyewe likafanyiwa kazi. Ni kweli kwamba waislamu wanabaguliwa kwenye nchi hii na chanzo cha kubaguliwa kwao ni nini na anayewabagua ni nani?

CCM ni zao la TANU na ASP, kwa maana nyingine vyama hivyo viwili ndiyo asili ya CCM. Hapa hatuwezi kuijadili ASP kwa kuwa kwa muktadha wa mada hii yenyewe moja kwa moja haifai kujadiliwa. Mara baada ya Uhuru kulikuwa na vyama vingi vya siasa mpaka pale vilipopigwa Marufuku na TANU mwaka 1965. Jee waislamu waliunga mkono chama gani kati ya TANU na hivyo vingine?

Miaka 27 baadaye mwaka 1992 mfumo wa vyama vingi ulirejeshwa hapa nchini na CCM iliyozaliwa kwa kuunganisha vyama vya ASP na TANU, nayo ikajivika uhai kabla haijazaliwa kisheria. Tangu hapo hadi sasa nchi yetu imekuwa inafuata mfumo wa vyama vingi vya siasa. Jee kwa kipindi chote hicho waislamu unapofika wakati wa uchaguzi huunga mkono chama gani cha siasa kama si CCM?

Kwa nini kina Sheikh Khalifa na kina Mohamed Said huwa siwasikii wakisema chama kinachosababisha wao wabaguliwe ni CCM kwa kuiga tabia ile ile ya TANU badala yake wanazungumza kiujumla kwamba wanabaguliwa? Kama Serikaili ndiyo inawabagua waislamu na kuwapendelea wakristo hiyo serikali inatokana na chama gani cha siasa kama si hapo awali na TANU na sasa CCM?

Hao wanaoleta Orodha ndeefu za wasomi wa kiislamu ili wateuliwe na Magufuli mwaka jana walikiunga mkono chama gani kama si CCM? Sheikh Khalifa anasema kuwa wao walimuunga mkono Magufuli kwa kuwa hakuchangiwa na wafanyabiashara kwenda Ikulu. Hilo analisema kama ni ukweli anaousimamia ama kama ni Kada wa CCM kushabikia kauli ya Mwenyekiti wake Taifa kwamba hakuchangiwa na wafanyabiashara?

Waislamu wa nchi hii wakiongozwa na kina Sheikh Khalifa na BAKWATA kosa lao kubwa ni kuiamini CCM ambayo mwisho wa siku ikiunda serikali, wao huja kulalamika kwamba inawabagua kwenye kila nyanja ya maisha. Kosa ni lao wala si la CCM!
 
Kwani wakienda huko serikalini hao waislamu wanaenda kuuendeleza uislamu au kufanya kazi ya nchi?

Awamu iliyopita alikuwa mkuu wa nchi mwenye imani ya kiislamu vipi hao waislamu walipata ulaji huko serikalini?

Hao wanaipigia debe hao waislamu wenzao wapate dili huko serikalini watakuwa wana masilahi binafsi tu.

Sioni sababu ya wao kupiga kelele wakati uhuru wa kuabudu upo pale pale mengine wayaache yapite kwa serikali hii ilivyo sikivu watakuja kupewa onyo sasa hivi na ile wizara ya kufungia magazeti kwa kuitwa wachochezi.
 
waisilamu wao waliamua kujiattach na ccm na serikali yake ndomana hata wakiwa na mambo ya msingi yanayowahusu nivigumu kusimama na kutetea haki yao wanailalamikia ccm ambayo kwakutumia majukwaa yao yadini husimama kuipigia kampeni ishinde..!!Huwa nayapuuza malalamiko ya waisilamu kuhusu kutotendewa haki na serikali katika nyanja mbalimbali wakati wao wenyewe wamekubali kuwa kivuli cha serikali kupitia Bakwata
 
Hivi sasa kuna fukuto kubwa miongoni mwa Waislamu kila unapofanywa uteuzi ndani ya Serikali wao huangalia kama kuna muislamu yeyote ameteuliwa. Mara nyingi huambulia patupu. Kwenye vyombo vya habari kama Gazeti la "Mizani" humo kina Sheikh Khalifa kwa juhudi kubwa hadi wamefikia kuchapisha majina ya waislamu ambao wanadhani wana sifa ya kuteuliwa kwenye teuzi zinazofanywa.

Mimi si muumini wa siasa au maisha kwa kuangalia vigezo vya dini ya mtu, lakini kama ipo dhana ya dini au kundi fulani la watu katika jamii linaona kama linabaguliwa ni vema jambo lenyewe likafanyiwa kazi. Ni kweli kwamba waislamu wanabaguliwa kwenye nchi hii na chanzo cha kubaguliwa kwao ni nini na anayewabagua ni nani?

CCM ni zao la TANU na ASP, kwa maana nyingine vyama hivyo viwili ndiyo asili ya CCM. Hapa hatuwezi kuijadili ASP kwa kuwa kwa muktadha wa mada hii yenyewe moja kwa moja haifai kujadiliwa. Mara baada ya Uhuru kulikuwa na vyama vingi vya siasa mpaka pale vilipopigwa Marufuku na TANU mwaka 1965. Jee waislamu waliunga mkono chama gani kati ya TANU na hivyo vingine?

Miaka 27 baadaye mwaka 1992 mfumo wa vyama vingi ulirejeshwa hapa nchini na CCM iliyozaliwa kwa kuunganisha vyama vya ASP na TANU, nacho kikajivika uhai kabla hakijazaliwa kisheria. Tangu hapo hadi sasa nchi yetu imekuwa inafuata mfumo wa vyama vingi vya siasa. Jee kwa kipindi chote hicho waislamu unapofika wakati wa uchaguzi huunga mkono chama gani cha siasa kama si CCM?

Kwa nini kina Sheikh Khalifa na kina Mohamed Said huwa siwasikii wakisema chama kinachosababisha wao wabaguliwe ni CCM kwa kuiga tabia ile ile ya TANU badala yake wanazungumza kiujumla kwamba wanabaguliwa? Kama Serikaili ndiyo inawabagua waislamu na kuwapendelea wakristo hiyo serikali inatokana na chama gani cha siasa kama si hapo awali na TANU na sasa CCM?

Hao wanaoleta Orodha ndeefu za wasomi wa kiislamu ili wateuliwe na Magufuli mwaka jana walikiunga mkono chama gani kama si CCM? Sheikh Khalifa anasema kuwa wao walimuunga mkono Magufuli kwa kuwa hakuchangiwa na wafanyabiashara kwenda Ikulu. Hilo analisema kama ni ukweli anaousimamia ama kama ni Kada wa CCM kushabikia kauli ya Mwenyekiti wake Taifa kwamba hakuchangiwa na wafanyabiashara?

Waislamu wa nchi hii wakiongozwa na kina Sheikh Khalifa na BAKWATA kosa lao kubwa ni kuiamini CCM ambayo ikiunda serikali na wao huja kulalamika kwamba inawabagua kwenye kila nyanja ya maisha. Kosa ni lao wala si la CCM!
Chadema hamna kiongozi yoyote wa juu muislam
 
chipa GM Huo ndio ukweli wenyewe endeleeni kujificha hukohuko kwenye kivuli cha udini ndomana hata nyie kwa nyie mmegawanyika tu na kamwe hamtakuja kuwa say mbele ya wanaccm na serikali yao damn full
 
Chadema hamna kiongozi yoyote wa juu muislam
Waislamu wanalalmika kuwa serikali inawabagua, na hata ile orodha ya wale waislamu wasomi, Sheikh Khalifa hakuitoa ili Mbowe aitumie bali ili Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM taifa aitumie. Na kwako wewe Mwalimu Salum na Profesa Safari ni wakristo. Halafu Mbona CUF viongozi wake wengi ni waislamu na wala hamuiungi mkono?

Maajabu Lipumba ambaye ni Professa Muislamu alifanya "Jitihada" ili CCM ishinde wakati yeye akiwa ni mwenyekiti wa CUF.
 
Kwani wakienda huko serikalini hao waislamu wanaenda kuuendeleza uislamu au kufanya kazi ya nchi?

Awamu iliyopita alikuwa mkuu wa nchi mwenye imani ya kiislamu vipi hao waislamu walipata ulaji huko serikalini?

Hao wanaipigia debe hao waislamu wenzao wapate dili huko serikalini watakuwa wana masilahi binafsi tu.

Sioni sababu ya wao kupiga kelele wakati uhuru wa kuabudu upo pale pale mengine wayaache yapite kwa serikali hii ilivyo sikivu watakuja kupewa onyo sasa hivi na ile wizara ya kufungia magazeti kwa kuitwa wachochezi.
Kwani kila aliye dai uhuru alifaidi matunda ya kudai uhuru? kuna watu chungu nzima tulianza kudai vyama vingi kwasababu tulijua faida ya vyama vingi ingawa sisi siyo wana siasa.
 
Mimi ni muislam safi kabisa. Kwa mtanzania anayekuja mbele yangu na kunieleza habari za udini kwenye utumishi wa umma huwa simuelewi kabisa na kwa ufupi huwa ni adui yangu. Ni vema ifahamike kuwa Tanzania ya leo mama muislam baba mkristo au baba muislam mama mkristo. Mfano ni Marehemu Spika Samwel Sita ambaye mama yake ni muislam baba mkristo.

Kwahiyo watu wa aina hii Tanzania ni wengi sana wenye mchanganyiko wa dini kifamilia. Unapoleta mambo ya dini kwenye serikali unataka tusemeje. Kama Magufuli anadhana ya namna hii basi naye pia hanifai kama kiongozi wangu.

Acheni kuleta mambo ya dini na ukabila kwenye siasa na kwenye kuendesha serikali. Nalisema kwa wote wanaongoza na sisi wananchi tunaoongozwa.

TUWEKE DINI ZETU PEMBENI.
 
bila kwenye siasa na kwenye kuendesha serikali. Nalisema kwa wote wanaongoza na sisi wananchi tunaoongozwa.

TUWEKE DINI ZETU PEMBENI.
Ndugu yangu haya si mambo ya udini bali ni mambo halisi. Waislamu kila mahala iwe ni kwenye makongamano, kweye Hutuba za misikitini, kwenye mihadhara na hata kwenye vijiwe mitaani, wanalalamika wanabaguliwa na "mfumo Kristu" sasa kwa mtazamo wangu huo mfumo Kristu unalelewa na CCM na CCM ndiyo chama kinachoungwa mkono kwa wingi na waislamu. Sasa kuna haja ya kulalamika kwa matendo ya chama unachokipenda na kukichagua kwenye kila uchaguzi?

Halafu udini na Dini ni vitu viwili tofauti. Udini ni pale watu wawili wenye sifa sawa ukamchagua mmoja kwa sababu ni wa dini yako tu ama ni mmoja kazidiwa sifa na mwenzie wewe ukamwacha yule mwenye sifa na kumchagua asiye na sifa kwa kuwa ni wa dini yako.
 
Hapana, huu Uzi unakosea mashiko, na unamapungufu mengi sana. Kwanza nadhani huu ulikuwa sio uzi wa kuhoji swala alililo zungumzia na Sheikh Khalifa, bali umekuwa uzi wa kuponda CCM na kujaribu kupata wafuasi wa dini ya kiislamu kwenda kwenye chama pinzani.

Ujuwe kwamba raia yoyote wa Tanzania ambaye ni muumini wa dini ya kiislamu au dini yoyote ile, ni mtu huru. Ni mtu mwenye uhuru wa kifikra na wakutenda. Muislamu ana ruhusiwa kuwa mwanachama au hata mpenzi wa chama chochote cha siasa, na ukisema waislamu wote ndio wanapigia kura ccm hapo una-generalised na kuwatendea kosa waislamu kwa kuweka mawazo yako kwenye vichwa vyao.

Jaribu kuelewa uteuzi wa kiongozi wa juu unaofanya na Rais unafanyikaje kabla ya kwenda mbali na kukubali kuwa waislamu wanaonewa. Kuna idara nyingi jina la mteuliwa linanpitia kabla ya kukubalika na mwisho kuteuliwa. Idara ya utumishi, idara ya nidhamu, idara ya usalama, idara husika ambao mteuliwa ataenda kufanya kazi, mpaka wakati mwingine idara aliko toka mteuliwa.

Kote huko unataka kusema kuwa jina la kislamu likifika wanalipinga chini na kuchukuwa wa dini nyingine?, hiyo sio kweli. Na unaposema kuwa ni kosa la waislamu kuichaguwa ccm, unataka kusema kuwa siku ambayo Chadema ikifanikiwa kuingia madarakani, basi malalamiko yote ya waislamu yata kuwa yamekwisha?

Ni mchezo wa hatari kutumia dini kupata wafusi, acha watanzania wenye dini mbali mbali waamuwe wenyewe ni chama gani wanapenda kukiunga mkono.
 
Mwanzi1 mbona huwa hamuwakemei kina Sheikh Khalifa wanapo "Generalize" kwamba wanaongea kwa niaba ya waislamu? Unakumbuka waliposema ni dhambi kwa "waislamu" kushiriki kwenye maandamano ya UKUTA? Halafu unataka kusema kwamba huko ambako majina ya wateuliewa "hupitia" ni majina ya waislamu tu hukwama?
 
nilishawapuza waisilamu siku nyingi
Hapana ndugu yangu, hapa tunachojaribu kufanya ni kutenganisha kati ya wana CCM ambao hujitwika jukumu la "kuwawakilisha" Waislamu na kuwatumia kwa manufaa yao wakati wa Uchaguzi na kugeuka kuwatumia tena CCM inapokuwa madarakani, na waislamu wanaousimamia Uislamu.
 
Hawa jamaa wanachezewa na ccm kila uchaguzi ukifika. Mara utasikia mahakama ya kadhi. Nasikia wengine wakipewa pilau tu wanalainika........
Waislamu wanajua mambo mawili tu
1. Yesu sio Mungu
2. Wanategemea kugawiwa mabikra baada ya kifo
 
Hapana ndugu yangu, hapa tunachojaribu kufanya ni kutenganisha kati ya wana CCM ambao hujitwika jukumu la "kuwawakilisha" Waislamu na kuwatumia kwa manufaa yao wakati wa Uchaguzi na kugeuka kuwatumia tena CCM inapokuwa madarakani, na waislamu wanaousimamia Uislamu.
washajua kuwa wanatumiwa bado wanakubali kutumika sasa hapo nani mwerevu?
waache unafiki ndio nitawaunga mkono
 
Hawa jamaa wanachezewa na ccm kila uchaguzi ukifika. Mara utasikia mahakama ya kadhi. Nasikia wengine wakipewa pilau tu wanalainika........
Waislamu wanajua mambo mawili tu
1. Yesu sio Mungu
2. Wanategemea kugawiwa mabikra baada ya kifo
wenye makalio makubwa na macho km vikombe
 
washajua kuwa wanatumiwa bado wanakubali kutumika sasa hapo nani mwerevu?
waache unafiki ndio nitawaunga mkono
Tatizo siyo waislamu kama waumini bali wale wanaojifanya kuzungumza kwa niaba ya waislamu. Wakati wa Uchaguzi utaona mpaka wanajiapia wakisema CCM ndiyo chama kinachojali waislamu, uchaguzi ukiisha tu wanaanzisha "mihadhara" na mpaka kusoma "Itkaf" kulaani waislamu kubaguliwa na serikali iliyoundwa na chama kile kile walichokipigia chapuo wakati wa uchaguzi!
 
Siku nyingine viongozi wa kiislamu wapeleke majina ya wasomi wao kwa viongozi wa chama, CCM......kuwa tunawapigia kampeni ila mukishika madaraka, hakikisheni haya majina yanakuwa kwenye teuzi......vinginevyo wanyamaze tu wasituchoshe, maana wamekuwa kama tawi LA CCM.
 
Hivi sasa kuna fukuto kubwa miongoni mwa Waislamu kila unapofanywa uteuzi ndani ya Serikali wao huangalia kama kuna muislamu yeyote ameteuliwa. Mara nyingi huambulia patupu. Kwenye vyombo vya habari kama Gazeti la "Mizani" humo kina Sheikh Khalifa kwa juhudi kubwa kabisa hadi wamefikia kuchapisha majina ya waislamu ambao wanadhani wana sifa ya kuteuliwa kwenye teuzi zinazofanywa lakini hawateuliwi.

Mimi si muumini wa siasa au maisha kwa kuangalia vigezo vya dini ya mtu, lakini kama ipo dhana ya dini au kundi fulani la watu katika jamii linaona kama linabaguliwa ni vema jambo lenyewe likafanyiwa kazi. Ni kweli kwamba waislamu wanabaguliwa kwenye nchi hii na chanzo cha kubaguliwa kwao ni nini na anayewabagua ni nani?

CCM ni zao la TANU na ASP, kwa maana nyingine vyama hivyo viwili ndiyo asili ya CCM. Hapa hatuwezi kuijadili ASP kwa kuwa kwa muktadha wa mada hii yenyewe moja kwa moja haifai kujadiliwa. Mara baada ya Uhuru kulikuwa na vyama vingi vya siasa mpaka pale vilipopigwa Marufuku na TANU mwaka 1965. Jee waislamu waliunga mkono chama gani kati ya TANU na hivyo vingine?

Miaka 27 baadaye mwaka 1992 mfumo wa vyama vingi ulirejeshwa hapa nchini na CCM iliyozaliwa kwa kuunganisha vyama vya ASP na TANU, nayo ikajivika uhai kabla haijazaliwa kisheria. Tangu hapo hadi sasa nchi yetu imekuwa inafuata mfumo wa vyama vingi vya siasa. Jee kwa kipindi chote hicho waislamu unapofika wakati wa uchaguzi huunga mkono chama gani cha siasa kama si CCM?

Kwa nini kina Sheikh Khalifa na kina Mohamed Said huwa siwasikii wakisema chama kinachosababisha wao wabaguliwe ni CCM kwa kuiga tabia ile ile ya TANU badala yake wanazungumza kiujumla kwamba wanabaguliwa? Kama Serikaili ndiyo inawabagua waislamu na kuwapendelea wakristo hiyo serikali inatokana na chama gani cha siasa kama si hapo awali na TANU na sasa CCM?

Hao wanaoleta Orodha ndeefu za wasomi wa kiislamu ili wateuliwe na Magufuli mwaka jana walikiunga mkono chama gani kama si CCM? Sheikh Khalifa anasema kuwa wao walimuunga mkono Magufuli kwa kuwa hakuchangiwa na wafanyabiashara kwenda Ikulu. Hilo analisema kama ni ukweli anaousimamia ama kama ni Kada wa CCM kushabikia kauli ya Mwenyekiti wake Taifa kwamba hakuchangiwa na wafanyabiashara?

Waislamu wa nchi hii wakiongozwa na kina Sheikh Khalifa na BAKWATA kosa lao kubwa ni kuiamini CCM ambayo mwisho wa siku ikiunda serikali, wao huja kulalamika kwamba inawabagua kwenye kila nyanja ya maisha. Kosa ni lao wala si la CCM!
Siasa hizi bana,

Kwahiyo mkuu hebu toeni mifano tuone kama kweli mna nia ya kuwasaidia hawa waislamu - maana wanaona wao wanaonewa.Ninyi mtawapa kitu gani ambacho unaona CCM wamewanyima ?

Maana sio waislamu tu hata wanawake nao wanataka uwiano wa jinsia bila kuwasahau Walemavu, kanda fulani nk

Vile vile kuna wanaotaka maendeleo sasa sijui wewe unaemaje kuhusu hili ?
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom