mbingunikwetu
JF-Expert Member
- Feb 17, 2015
- 13,663
- 18,036
Wanachokifanya Marekani, NATO na mataifa ya magharibi kwa ujumla dhidi ya urusi ni kuifunga mikono na miguu Urusi wakati ikipigana na ukraine, ili kuisaidia Ukraine kwenye vita hivyo. Hakuna asiyejua kuwa nguvu ya kiuchumi ndiyo mikono na miguu inayohitajika sana wakati wa vita ili kuwezesha vita.
Kwa hiyo kuifunga nchi inayopigana miguu na mikono ni sawa na kumbana paka kwenye kona. Akijiridhisha kuwa umembana na hana mahali pa kutokea, atabadilika ghafla na kuwa mnyama mkali na mwenye nguvu hujawahi kuona!! Lazima akuvamie na aondoke na pua zako!
Urusi inaishiwa nguvu za kiuchumi kwa haraka sana kutokana na vikwazo vya kiuchumi na kuporwa mali zake zote ilizowekeza nchi za nje.
Niamini, urusi itafanya unyama wa kutisha maana haiwezi kukubali kushindwa hata kama imefungwa miguu na mikono, lakini kichwa kiko wazi. Tutegemee vita vya nyuklia muda wowote tangu sasa na mlengwa wa kwanza ni marekani na uingereza.
Wenye ndugu nchi hizo waambieni warudi nyumbani kabla hawajachelewa!! Mark my words!
Kwa hiyo kuifunga nchi inayopigana miguu na mikono ni sawa na kumbana paka kwenye kona. Akijiridhisha kuwa umembana na hana mahali pa kutokea, atabadilika ghafla na kuwa mnyama mkali na mwenye nguvu hujawahi kuona!! Lazima akuvamie na aondoke na pua zako!
Urusi inaishiwa nguvu za kiuchumi kwa haraka sana kutokana na vikwazo vya kiuchumi na kuporwa mali zake zote ilizowekeza nchi za nje.
Niamini, urusi itafanya unyama wa kutisha maana haiwezi kukubali kushindwa hata kama imefungwa miguu na mikono, lakini kichwa kiko wazi. Tutegemee vita vya nyuklia muda wowote tangu sasa na mlengwa wa kwanza ni marekani na uingereza.
Wenye ndugu nchi hizo waambieni warudi nyumbani kabla hawajachelewa!! Mark my words!