Wanachama wa upinzani huku chini watofautiana na viongozi wao wakuu wa vyama

MwanaPekee

JF-Expert Member
Jul 18, 2014
382
385
Leo 17/11/2019 zinaanza rasmi kampeni za Uchaguzi wa Serikali za mitaa kote nchini. Ikumbukwe kuwa hivi karibuni viongozi wa vyama kadhaa vya upinzani vikiwemo CHADEMA, ACT-Wazalendo, na NCCR-Mageuzi; walitangaza kuwa wagombea wao wanajiondoa kwenye uchaguzi huo kutokana na sababu walizozibainisha.

Leo ukipita katika baadhi ya mitaa unakuta kuna shamrashamra za hapa na pale kwa wanachama wa vyama vilivyotangaza kujitoa kwenye uchaguzi, hali inayoonesha kuwa wanachama wa chini huku mitaani, na matawini hawakubaliani na maamuzi ya viongozi wao.

Wanachama huku chini wanataka kuchagua viongozi wanaowataka wao, hasa baada ya serikali kutangaza kuwa mgombea yeyote aliyechukua fomu na kuirudisha basi anaingia kwenye kinyang’anyiro hicho.

Kitu ambacho viongozi wa upinzani inabidi wajifunze ni kuwa maamuzi yao ya kukurupuka yanawaumiza sana wanachama wao. Na hali hiyo imepelekea wanachama wao wengi kukosa imani nao.

Wanachama wa mitandaoni ni asilimia ndogo sana, hivyo ku-rely kwenye comments za mitandaoni kama ndiyo maamuzi ya wanachama walio wengi ni kosa kubwa sana, ambalo kimsingi ni sawa na kujichimbia kaburi lao wenyewe katika uringo wa siasa.
 
Kama viongoz wa juu wanakurupuka basi hao wanataka kuwachagua viongoz wao wahamie ccm ili wakawachague viongoz wanaowataka hii nchi ya demokrasia wasiwalaum viongoz wao ktk kujitoa kwana hao viongoz wa matawi kama wanajitambua hawawez laum kwa uovu huu ambao ccm umefanya! Mwanachama wa upinzan ambae n mpumbav ndiye atakae laum maamuz ya viongoz wao
 
Inakuuma nini kwani kukaa pamoja ni kosa.Weka hata picha kama unaujasiri.Nimepita pale kijiatonyama ccm wanafanya kampeni mtaa mzima hata watu 10 hawafiki,wengine ni wa masare tu

MwanaPekee
 
hao viongozi wa chini wa upinzani wanaotaka kufanya kampeni , wanafanya kampeni kwa uteuzi upi pia ungetupa hiyo sehemu tujue ni ipi.??
 
Upinzani kila mtu kambale hasa Chadema

Muulize Haji Dunni analifahamu hili swala la ukambale ndani ya Chadema
 
Inakuuma nini kwani kukaa pamoja ni kosa.Weka hata picha kama unaujasiri.Nimepita pale kijiatonyama ccm wanafanya kampeni mtaa mzima hata watu 10 hawafiki,wengine ni wa masare tu

MwanaPekee

Nikiweka picha mtasema imetengenezwa. Nyie subirini matamko ya viongozi wenu ndo mtajua watu wanafanya kampeni au la. Manake hao ndo mnawaamini sana, ila hawa wananchi wa mitaani huku nuksi, hawaambiwi kitu
 
Mimi pia niko mataani wewe uko mtaa upi ambao hao wananchi wanachama wa upinzani ni wamemaindi?Taja huo mtaa halafu tuje tuufanyie evaluation maana WanaJF wapo mitaa yote ya Tz
Nikiweka picha mtasema imetengenezwa. Nyie subirini matamko ya viongozi wenu ndo mtajua watu wanafanya kampeni au la. Manake hao ndo mnawaamini sana, ila hawa wananchi wa mitaani huku nuksi, hawaambiwi kitu
 
Nikiweka picha mtasema imetengenezwa. Nyie subirini matamko ya viongozi wenu ndo mtajua watu wanafanya kampeni au la. Manake hao ndo mnawaamini sana, ila hawa wananchi wa mitaani huku nuksi, hawaambiwi kitu
Wananchi wengi siyo wanachama wa chama chochote hivyo wanahaki ya kushiriki uchaguzi Kadri wanavyoona. Vyama vinainfluence kwa wanachama na wapenzi wao.
 
Mange anawajua vizuri watanzania, watanzania wa mitandaoni na watanzania wa mtaani wako tofauti Sana
 
Unaweza kuweka ushahidi? Sheria ya uchaguzi inaelekeza vyama kupeleka ratiba ya kampeni zake , sasa unaweza kuiambia JF kati ya vyama vilivyojitoa ni kipi kimepeleka ratiba ya kampeni mpaka ulete huu uzushi ?

Ni bahati mbaya moderator anaacha huu upumbavu jukwaani.
 
Back
Top Bottom