WanaCCM wenzangu, kwanini hatujiamini? Wagombea wetu watabebwa na maneno na matendo yao

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
CCM ni chama kikubwa na kikongwe hapa nchini. Ni chama tawala. Ni chama dola. Kimeshinda chaguzi zote kuu za vyama vingi kuanzia ule wa 1995 hadi wa 2015. Pamoja na uwepo wa wagombea machachari na 'hatari' wa Urais (mfano wa Mrema, Slaa na Lowassa), CCM imekuwa ikiibuka kidedea na bendera kuendelea kupepea.

Hata kwenye Ubunge na Udiwani, CCM hulidhibiti Bunge na Halmashauri nyingi mno kwa kushinda kwa wingi wa Wabunge na Madiwani. CCM ni nambari wani! Huu wasiwasi uliopo sasa unatokea wapi? Huu wasiwasi hadi kuanza kampeni za Urais mapema unatokana na nini hasa? Hatumuamini mgombea wetu mtarajiwa? Hajafanya lolote? Hasemi na kufanya yaliyo mema?

Serikali hii imeimarisha miundombinu (barabara, reli, madaraja nk); imefufua Shirika letu la Ndege; inajenga Bwala la Umeme la Nyerere; imedhibiti nidhamu ya watumishi wa umma na kupunguza pakubwa rushwa na ufisadi; imewaweka akiba watumishi wa umma kuhusu mishahara na stahiki zao nyingine; imekifanya chama chetu cha CCM kubaki pekee kilicho 'active' na kadhalika.

Yote hayo hayatoshi na kutupa amani moyoni ya kuibuka kidedea mwaka huu? Kama chama, kama ilivyo kawaida yetu, tunazo lulu zetu za ushindi. Tunayo ile ya 'kupita bila kupingwa', Tume Huru ya Uchaguzi, Polisi, Wazee wa Suti na 'kekundu'. Wasiwasi wetu unatokea wapi kama chama kila kitu cha kuhakikisha ushindi unapatikana? Tujiamini

Inashangaza CCM kusafiria nyota ya Msanii kama Diamond ili kumpigia debe Dr. Magufuli na 'kumhakikishia' ushindi mwaka huu. Ni aibu na inatia ghadhabu. Tunamuogopa nani ikiwa tuna mema na vitendea kazi vya kuibuka washindi kuliko wahindi. CCM tunapaswa kutembea vifua-mbele hadi kwenye kilele. Kuanza kampeni mapema ni uoga na aibu kwa chama!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
Kwa hiyo mkapa anayedai tume huru ya uchaguzi anataka imsaidie kupata ushindi wa ( 800 X 640 ).jpg
 
Yote hayo hayatoshi na kutupa amani moyoni ya kuibuka kidedea mwaka huu? Kama chama, kama ilivyo kawaida yetu, tunazo lulu zetu za ushindi. Tunayo ile ya 'kupita bila kupingwa', Tume Huru ya Uchaguzi, Polisi, Wazee wa Suti na 'kekundu'. Wasiwasi wetu unatokea wapi kama chama kila kitu cha kuhakikisha ushindi unapatikana? Tujiamini


Yaani hii paragraph ndo kila kitu kwa ccm ndo maana hawajiamini kwa sababu wanajua hawapendwi wanatumia nguvu tangu kale hara jamaa yule anajua fika shida iliyopo ndani ya genge lao
 
Nafsi inawasuta hasa huyu bwana aliyeandika mada hii amejitutumua sana kuonyesha wasiwe na wasiwasi ingawa yeye mwenyewe imani yake iko kwenye mashinary yao
 
Ukiona mtu ana hofu juu ya jambo fulani ovu/baya alilolitenda. Ujue bado ana vichembe vya Uungu nafsini mwake. Ila nafsi ikifubaa kwa matendo maovu, hawezi kuwa na hofu hata kama kidogo. Ni unyama unyama tu. Tuendelee kujionea yajayo mwaka huu.
 
CCM ya Magufuli imekataliwa Tanganyika na Zanzibar, Duniani na Mbinguni.

CCM NI LAANA NA MaCCM WOTE WAMELAANIWA
 
CCM haina wapiga kura wa kada yoyote ila polisi, usalama na tume yetu ya uchaguzi. CCM haipendwi na wafanyakazi, wafanya biashara , waliokosa ajira tangu2015 (magraduate wote) , wakulima nk.

Sent using Jamii Forums mobile app
Huo ndio ukweli, kiongozi wa nchi kila siku anapambana na wapinzani kila siku tangu achaguliwe uchaguzi uliopita,kampeni za muda Mrefu,kuchakachua ushindi chaguzi za marudio na serikali za mitaa.
Hiki chama Tawala kinapendwa na Watanzania wa nchi gani?Hawajiamini hata kumalizia mchakato wa katiba mpya,tume huru ya uchaguzi ni tishio kwao.
Wanatawala badala ya kuongoza.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
CCM ni chama kikubwa na kikongwe hapa nchini. Ni chama tawala. Ni chama dola. Kimeshinda chaguzi zote kuu za vyama vingi kuanzia ule wa 1995 hadi wa 2015. Pamoja na uwepo wa wagombea machachari na 'hatari' wa Urais (mfano wa Mrema, Slaa na Lowassa), CCM imekuwa ikiibuka kidedea na bendera kuendelea kupepea.

Hata kwenye Ubunge na Udiwani, CCM hulidhibiti Bunge na Halmashauri nyingi mno kwa kushinda kwa wingi wa Wabunge na Madiwani. CCM ni nambari wani! Huu wasiwasi uliopo sasa unatokea wapi? Huu wasiwasi hadi kuanza kampeni za Urais mapema unatokana na nini hasa? Hatumuamini mgombea wetu mtarajiwa? Hajafanya lolote? Hasemi na kufanya yaliyo mema?

Serikali hii imeimarisha miundombinu (barabara, reli, madaraja nk); imefufua Shirika letu la Ndege; inajenga Bwala la Umeme la Nyerere; imedhibiti nidhamu ya watumishi wa umma na kupunguza pakubwa rushwa na ufisadi; imewaweka akiba watumishi wa umma kuhusu mishahara na stahiki zao nyingine; imekifanya chama chetu cha CCM kubaki pekee kilicho 'active' na kadhalika.

Yote hayo hayatoshi na kutupa amani moyoni ya kuibuka kidedea mwaka huu? Kama chama, kama ilivyo kawaida yetu, tunazo lulu zetu za ushindi. Tunayo ile ya 'kupita bila kupingwa', Tume Huru ya Uchaguzi, Polisi, Wazee wa Suti na 'kekundu'. Wasiwasi wetu unatokea wapi kama chama kila kitu cha kuhakikisha ushindi unapatikana? Tujiamini

Inashangaza CCM kusafiria nyota ya Msanii kama Diamond ili kumpigia debe Dr. Magufuli na 'kumhakikishia' ushindi mwaka huu. Ni aibu na inatia ghadhabu. Tunamuogopa nani ikiwa tuna mema na vitendea kazi vya kuibuka washindi kuliko wahindi. CCM tunapaswa kutembea vifua-mbele hadi kwenye kilele. Kuanza kampeni mapema ni uoga na aibu kwa chama!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Hivi mgombea wenu mtarajiwa alishawahi kumpgia Lissu cm na kumjulia hali? Hata alipokuwa Nairobi tu( aghakan hospital)? Na Kama hapana why? Hivi zile hela alizikuwa anawahonga Mnyeti wa diwani wa Arumeru alikuwa anazitoa wapi? Hivi wimbi la kutekana na kupotezana ulishawahi kuliona kwa kiwango hiki kwenye awamu zilizopita? Wana ccm wenzako wanacheka usoni moyoni hawana amani kabsa
 
Tusimshambulie mleta mada bali tushambulie hoja. Mleta mada ni ccm mpya ila inaonesha anafahamu hali halisi ilivyo kulingana na uelewa wake . Anachotaka mleta mada ni kutaka kufahamu iwapo kuna watu wengine wanaoweza kuona mapungufu ama uimara wa cha chama cha ccm na kuleta mezani hoja zao kulingana na uelewa wao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom