G Sam
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 11,555
- 35,880
Magufuli, Polepole na Bashiru walinunua weee wakanunua weee wakuchukua viongozi wengi Chadema. Wakajisahau jambo moja kubwa ambalo ni wao kuibua vipaji vyao na kuacha kutegemea toka Chadema.
Mungu mkubwa, leo kila kona vijana wapo na Chadema tena vijana machachari, wajengaji wa hoja kuanzia kwenye mitandao mpaka kwenye majukwaa. Mumeumbuka mchana peupe peeeee!
Silinde alipokuwa kwetu alikuwa Silinde kweli kweli, kaenda CCM kawa "Silindege" kipaji chote chali! Kule Kilombero habari mnazo. Mwanza na Mara mnaona wenyewe. Hapa Dar ndiyo kabisaaa.
Mbaya zaidi mnamchukua mtu leo, kesho anasahaulika hata jimboni kwake. Mliegemea siasa za hovyo hovyo yamewashuka sasa.
Tukutane Oktoba tunyoane kweli kweli majukwaani! Upinzani wa mwaka huu haijawahi kutokea Tanzania! Ni hoja baada ya hoja! Na mbaya zaidi tumejipanga kila idara. Msitegemee tena sisi kulia lia.
Sisi tulipokuwa tunafanya Chadema ni msingi, nyie mpo bize kufanya utopolo. Mkatumia vyombo vyote kujinadi lakini wapi. Hamuuziki na mbaya zaidi unyama wenu hadharani peupee! Njooni na hizo hoja zenu nyepesi sijui za ndege, stigilaz, sijui standard geji, na sasa kuna nyingine ya uchumi wa kati tutazivunja vunja mapema tu. Haina kuogopa polisi wala nani.
Mungu mkubwa, leo kila kona vijana wapo na Chadema tena vijana machachari, wajengaji wa hoja kuanzia kwenye mitandao mpaka kwenye majukwaa. Mumeumbuka mchana peupe peeeee!
Silinde alipokuwa kwetu alikuwa Silinde kweli kweli, kaenda CCM kawa "Silindege" kipaji chote chali! Kule Kilombero habari mnazo. Mwanza na Mara mnaona wenyewe. Hapa Dar ndiyo kabisaaa.
Mbaya zaidi mnamchukua mtu leo, kesho anasahaulika hata jimboni kwake. Mliegemea siasa za hovyo hovyo yamewashuka sasa.
Tukutane Oktoba tunyoane kweli kweli majukwaani! Upinzani wa mwaka huu haijawahi kutokea Tanzania! Ni hoja baada ya hoja! Na mbaya zaidi tumejipanga kila idara. Msitegemee tena sisi kulia lia.
Sisi tulipokuwa tunafanya Chadema ni msingi, nyie mpo bize kufanya utopolo. Mkatumia vyombo vyote kujinadi lakini wapi. Hamuuziki na mbaya zaidi unyama wenu hadharani peupee! Njooni na hizo hoja zenu nyepesi sijui za ndege, stigilaz, sijui standard geji, na sasa kuna nyingine ya uchumi wa kati tutazivunja vunja mapema tu. Haina kuogopa polisi wala nani.