WanaCCM acheni fitina, Freeman Mbowe ni mtaji mkubwa kwa CCM!

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,171
23,975
Huwa ninawashangaa sana baadhi ya wanaCCM wanaopiga kelele kumtaka Freeman Mbowe aachie cheo cha uenyekiti wa CHADEMA Taifa. Ninadhani hawajui nafasi ya Mbowe katika Maisha ya CCM tokea awe Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa.

Baadhi ya wanaCCM hawajui kuwa CCM imeendelea kushika dola kutokana na mchango mkubwa wa Mbowe kama Mwenyekiti wa CHADEMA.

Siwezi kujua kwa sasa CCM ingekuwa na hali gani kama Mbowe asingekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa lakini ninachojua kuwa mchango wake ndani ya CHADEMA umeiwezesha CCM kuendelea kushika dola.

Ieleweke kuwa Mbowe sio mwanasiasa bali ni mjasiliamali wa kisiasa. Kwa Mbowe, money talks than politics. Ukiweka dau la pesa au siasa mezani na ukamtaka kipi achukue, Mbowe atachukua pesa na kukuachia siasa. Mwaka 2006 wakati akiwa London akiongea na Watanzania kwenye Hotel ya Holiday Inn alinukuliwa akisema, “Politics to me is not a profession. I am a businessman and will remain one.

Historia inachagiza hoja zangu kuhusu msaada wa Mbowe kwa CCM kama ambavyo Mbunge Zitto Kabwe alivyowahi kubainisha katika andiko lake ambalo linapatikana hapa;

LINK>>>Zitto aanika siri nyeti za Mbowe, Adai hatakufa kama Chacha Wangwe

Zitto alibainisha hayo kwa kuandika, "Lissu anasema nimepewa magari 2 na Mzee Mkono. Anasema kaambiwa na Mkono. Naamini Mkono alimwambia pia mwaka 2005 alimpa Freeman Aikaeli Mbowe tshs 40m ili Mbowe asifanye kampeni Musoma vijijini. Nadhani alimwambia pia mwaka 2008 (baada ya orodha ya mafisadi kutangazwa 2007) Mkono alimpa Freeman tshs 20m za uchaguzi wa Tarime na Freeman akasema kwenye chama ametoa mkopo na akalipwa. Nadhani alimwambia pia kuwa Mwaka 2010 Mkono alimpa Mbowe tshs 200m za kampeni ya Slaa. Pia hakusahau kumwambia kuwa Rostam Aziz alimpa Mbowe tshs 100m za kampeni. Lissu anajua kuwa gazeti la Tanzania Daima limeanzishwa na fedha za chama kutoka Conservative party?’’

Zitto aliendelea kuandika, ‘’ Lissu ajue yeye ni kifaranga tu, Mimi namtaka mama wa kifaranga ajitokeze. Aeleze aliingia deal gani na Kinana na Sumaye mwaka 2005 kufuatia deni lake NSSF. Aweke wazi mkataba kati yake na NHC kuhusu nyumba ya Umma ilipo Club Bilicanas’’.

Ukisoma andiko la Zitto utagundua kuwa kwa kiasi kikubwa Mbowe amekuwa akiisaidia CCM kuendelea kushika dola.

Hata pale ambapo CUF ilionekana kutishia uhai wa CCM mwaka 2000-2005, Mbowe alijitokeza na kuisaidia CCM. Hata mwaka 2015 ambapo alionekana CCM iko kwenye hali ngumu sana ya kisiasa, Mbowe aliibuka tena baada ya kuchukua ''dau'' ili kuisaidia CCM kuendelea kushika dola kwa kutoa tiketi ya kugombea Urais kwa Edward Lowassa ambaye alijua vizuri kuwa hatashinda Uchaguzi Mkuu kutokana na Mbowe na kundi lake kumdhoofisha sana kwa kumvisha taji ya ufisadi papa kwa miaka zaidi ya miaka 8 huku wengine wakisema hafai hata kuchukua fomu ya kugombea Urais achilia mbali kupitishwa kuwa mgombea Urais. Msaada wa Mbowe ukaiwezesha CCM kuendelea tena kushika dola lakini kikubwa zaidi hata pale ambapo baadhi ya wapenzi na wanachama wa CHADEMA walipoanza kutoa shikinizo la kutaka kufanya fujo baada ya Uchaguzi Mkuu 2015, Mbowe alijitokeza na kuwapiga stop. Mission accomplished!

WanaCCM watambue kuwa hata mwaka 2020 atawasaidia tena kuendelea kushika dola!

Kumshinikiza Mbowe ili aachie Uenyekiti wa CHADEMA ni kukaribisha tatizo/matatizo ambayo hayajulikani utatuzi wake.

CCM kumbukeni Waingereza wana msemo usemao, ‘if it ain't broke, don't fix it and be careful what you wish for, lest it come true''!

WanaCCM acheni kujitakia matatizo ambayo ninaamini hamjui utatuzi wake!

mbowe.jpg
 
Jamaa katoka usingini hata alichoandika hakieleweki kwa hiyo toka mwaka 1961 ccm ipo madarakani kwa nguvu za mbowe?


Mwenyekiti wako wa ccm anafahamu mchango mkubwa wa polisi ,tume na mahakama vinapotokeleza majukumu yao vizur kuokoa chama kilichojifia cha ccm.
 
Jamaa katoka usingini hata alichoandika hakieleweki kwa hiyo toka mwaka 1961 ccm ipo madarakani kwa nguvu za mbowe?


Mwenyekiti wako wa ccm anafahamu mchango mkubwa wa polisi ,tume na mahakama vinapotokeleza majukumu yao vizur kuokoa chama kilichojifia cha ccm.
Huwezi kuelewa nilichokiandika kwa sababu uwezo wako kiakili na kifikra ndio mwisho wake.

Waache wenye uwezo mkubwa kiakiri na kifikra watajua na kuchanganua nilichokiandika.

Sidhani kama kuna mtu amekulazimisha kuelewa nilichokiandika.
 
Heheh mkuu mi wala sikatai nakubaliana kabisa na hoja yako,nilichotaka kujua ni, mantiki ya huu uzi ni nini,mana ni sawa na kulinda goli la mpinzani wako,au unaona timu pinzani inafanya makosa,alafu badala ya kutake advantage muwafunge eti wewe unakazana kuwaelekeza makosa yao na kuwahimiza wayarekebishe.Wanasema adui muombee njaa badala yake wewe unampelekea chakula na silaha kwangu haiingii akilini kabisa,labda unieleweshe tena komredi.
Hayo maswali ungemuuliza Zitto ambaye alitueleza mchezo anaofanya Mbowe ili CCM iendelee kushika dola.

Kama ni kupeleka chakula basi ni Zitto aliyetuletea chakula ndio maana akafukuzwa CHADEMA.
 
Nilidhani CCM inachaguliwa Sababu inatimiza ahadi kila inapochaguliwa..Kumbe ni tofauti..Kwamba Madhaifu ya Chadema ndiyo yanawapa Ridhaa ya kuongoza Nchi ..
MsemajiUkweli hili Siyo la Kujisifia..zaidi ya 50% siyo Mashabiki wa Vyama..na Wangependa kusikia Serikali ya CCM imeendelea kuchaguliwa sababu inafanya Kile walicho ahidi kwenye kampeni..
Na ndiyo Maana Awamu hii nguvu mnaelekeza kupambana na Wanasiasa Sababu ya hofu kama hizi.
 
Nilidhani CCM inachaguliwa Sababu inatimiza ahadi kila inapochaguliwa..Kumbe ni tofauti..Kwamba Madhaifu ya Chadema ndiyo yanawapa Ridhaa ya kuongoza Nchi ..
MsemajiUkweli hili Siyo la Kujisifia..zaidi ya 50% siyo Mashabiki wa Vyama..na Wangependa kusikia Serikali ya CCM imeendelea kuchaguliwa sababu inafanya Kile walicho ahidi kwenye kampeni..
Na ndiyo Maana Awamu hii nguvu mnaelekeza kupambana na Wanasiasa Sababu ya hofu kama hizi.
Lengo kuu la Chama makini cha siasa ni kushika dola bila kujali kinashika vipi dola.

Hayo mengine ni bla bla tu za kisiasa ambazo zinafichwa kwenye sheria.

Suala la utekelezaji wa ahadi sio la chama cha siasa bali nila serikali.

Ahadi hazitimizwi na chama cha siasa bali zinatimizwa na serikali.

Chama cha siasa na serikali ni taasisi/vitu viwili tofauti
 
Lengo kuu la Chama makini cha siasa ni kushika dola bila kujali kinashika vipi dola.

Hayo mengine ni bla bla tu za kisiasa ambazo zinafichwa kwenye sheria.

Suala la utekelezaji wa ahadi sio la chama cha siasa bali nila serikali.

Ahadi hazitimizwi na chama cha siasa bali zinatimizwa na serikali.

Chama cha siasa na serikali ni taasisi/vitu viwili tofauti
Kama ni hivi basi hakuna haja ya kumlaumu Mbowe..Maana ndiyo Siasa Kununuliwa,Kutumia pesa ,hata Kama alisema yeye ni Mfanyabiashara ni bla bla tu za Kisiasa.
CCM ina Mkataba na Serikali..Serikali hivi sasa inatekeleza Ilani ya CCM ..Siyo vitu Viwili tofauti..Serikali ikishindwa ni CCM imeshindwa.
 
Kama ni hivi basi hakuna haja ya kumlaumu Mbowe..Maana ndiyo Siasa Kununuliwa,Kutumia pesa ,hata Kama alisema yeye ni Mfanyabiashara ni bla bla tu za Kisiasa.
CCM ina Mkataba na Serikali..Serikali hivi sasa inatekeleza Ilani ya CCM ..Siyo vitu Viwili tofauti..Serikali ikishindwa ni CCM imeshindwa.
Ndio maana ninawashangaa wanaCCM wanaofanya fitina ili Mbowe aachie kiti cha Uenyekiti wa CHADEMA. Kwa nini wanamlaumu Mbowe wakati ni mtaji wao!

CCM haina mkataba na serikali. Serikali ina mkataba na katiba.

CCM ina mkataba na wananchi baada ya kushika dola bila kujali imefanikiwa vipi kushika dola.
 
MsemajiUkweli

Tuliwaambia Mbowe ni kisiki baada ya kuona mbinu na propaganda za kutaka asiwe mwenyekiti Chadema ku feli mmekuja kwa staili ya kumpongeza mimi naona ni sawa na kusema sizitaki mbichi hizi.

Ni mwana CCM mwendawazimu tu atakayedai Mbowe anaisaidia CCM, Mbowe huyu huyu aliyechukua karibu majiji yote yaliyokuwa ya CCM na kuyaweka upinzani, Mbowe huyu huyu aliyewanyanganya CCM karibu majimbo 50 na kuwapa upinzani, kafanikisha kuchukua zaidi ya viti maalum 70 vilivyokuwa vya wabunge wa CCM. Mbowe kafanikisha kuchukua halmashauri nyingi zilizokuwa za CCM na viti vya mameya wengi vilivyokuwa vya wana CCM na kuwapa upinzani halafu unasema anaisaidia CCM.

Lazima utakuwa na kasoro kichwani au kama wengi wanavyosema uko usingizini kwa sababu mwana CCM makini mwenye akili timamu hawezi kuwa na mawazo kama haya.
 
Huwa ninawashangaa sana baadhi ya wanaCCM wanaopiga kelele kumtaka Freeman Mbowe aachie cheo cha uenyekiti wa CHADEMA Taifa. Ninadhani hawajui nafasi ya Mbowe katika Maisha ya CCM tokea awe Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa.

Baadhi ya wanaCCM hawajui kuwa CCM imeendelea kushika dola kutokana na mchango mkubwa wa Mbowe kama Mwenyekiti wa CHADEMA.

Siwezi kujua kwa sasa CCM ingekuwa na hali gani kama Mbowe asingekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa lakini ninachojua kuwa mchango wake ndani ya CHADEMA umeiwezesha CCM kuendelea kushika dola.

Ieleweke kuwa Mbowe sio mwanasiasa bali ni mjasiliamali wa kisiasa. Kwa Mbowe, money talks than politics. Ukiweka dau la pesa au siasa mezani na ukamtaka kipi achukue, Mbowe atachukua pesa na kukuachia siasa. Mwaka 2006 wakati akiwa London akiongea na Watanzania kwenye Hotel ya Holiday Inn alinukuliwa akisema, “Politics to me is not a profession. I am a businessman and will remain one.

Historia inachagiza hoja zangu kuhusu msaada wa Mbowe kwa CCM kama ambavyo Mbunge Zitto Kabwe alivyowahi kubainisha katika andiko lake ambalo linapatikana hapa;

LINK>>>Zitto aanika siri nyeti za Mbowe, Adai hatakufa kama Chacha Wangwe

Zitto alibainisha hayo kwa kuandika, "Lissu anasema nimepewa magari 2 na Mzee Mkono. Anasema kaambiwa na Mkono. Naamini Mkono alimwambia pia mwaka 2005 alimpa Freeman Aikaeli Mbowe tshs 40m ili Mbowe asifanye kampeni Musoma vijijini. Nadhani alimwambia pia mwaka 2008 (baada ya orodha ya mafisadi kutangazwa 2007) Mkono alimpa Freeman tshs 20m za uchaguzi wa Tarime na Freeman akasema kwenye chama ametoa mkopo na akalipwa. Nadhani alimwambia pia kuwa Mwaka 2010 Mkono alimpa Mbowe tshs 200m za kampeni ya Slaa. Pia hakusahau kumwambia kuwa Rostam Aziz alimpa Mbowe tshs 100m za kampeni. Lissu anajua kuwa gazeti la Tanzania Daima limeanzishwa na fedha za chama kutoka Conservative party?’’

Zitto aliendelea kuandika, ‘’ Lissu ajue yeye ni kifaranga tu, Mimi namtaka mama wa kifaranga ajitokeze. Aeleze aliingia deal gani na Kinana na Sumaye mwaka 2005 kufuatia deni lake NSSF. Aweke wazi mkataba kati yake na NHC kuhusu nyumba ya Umma ilipo Club Bilicanas’’.

Ukisoma andiko la Zitto utagundua kuwa kwa kiasi kikubwa Mbowe amekuwa akiisaidia CCM kuendelea kushika dola.

Hata pale ambapo CUF ilionekana kutishia uhai wa CCM mwaka 2000-2005, Mbowe alijitokeza na kuisaidia CCM. Hata mwaka 2015 ambapo alionekana CCM iko kwenye hali ngumu sana ya kisiasa, Mbowe aliibuka tena baada ya kuchukua ''dau'' ili kuisaidia CCM kuendelea kushika dola kwa kutoa tiketi ya kugombea Urais kwa Edward Lowassa ambaye alijua vizuri kuwa hatashinda Uchaguzi Mkuu kutokana na Mbowe na kundi lake kumdhoofisha sana kwa kumvisha taji ya ufisadi papa kwa miaka zaidi ya miaka 8 huku wengine wakisema hafai hata kuchukua fomu ya kugombea Urais achilia mbali kupitishwa kuwa mgombea Urais. Msaada wa Mbowe ukaiwezesha CCM kuendelea tena kushika dola lakini kikubwa zaidi hata pale ambapo baadhi ya wapenzi na wanachama wa CHADEMA walipoanza kutoa shikinizo la kutaka kufanya fujo baada ya Uchaguzi Mkuu 2015, Mbowe alijitokeza na kuwapiga stop. Mission accomplished!

WanaCCM watambue kuwa hata mwaka 2020 atawasaidia tena kuendelea kushika dola!

Kumshinikiza Mbowe ili aachie Uenyekiti wa CHADEMA ni kukaribisha tatizo/matatizo ambayo hayajulikani utatuzi wake.

CCM kumbukeni Waingereza wana msemo usemao, ‘if it ain't broke, don't fix it and be careful what you wish for, lest it come true''!

WanaCCM acheni kujitakia matatizo ambayo ninaamini hamjui utatuzi wake!

View attachment 784112
Mnafiki at work! Naona umeshindwa style ile umekuja kivingine sasa.
 
Wewe nadhani unatumia kichwa chako kama kifaa cha kubebea mizigo badala ya kutunza ubongo ili ukusaidia kifikra!

Huwezi kumjua mchawi kama wewe sio mchawi!
Sasa unatumia nguvu kujihami badala ya Ku support hoja yako, unafiki umekuponza
 
Heheh mkuu mi wala sikatai nakubaliana kabisa na hoja yako,nilichotaka kujua ni, mantiki ya huu uzi ni nini,mana ni sawa na kulinda goli la mpinzani wako,au unaona timu pinzani inafanya makosa,alafu badala ya kutake advantage muwafunge eti wewe unakazana kuwaelekeza makosa yao na kuwahimiza wayarekebishe.Wanasema adui muombee njaa badala yake wewe unampelekea chakula na silaha kwangu haiingii akilini kabisa,labda unieleweshe tena komredi.
Wakati mwingine ili kulinda ama kutunza hadhi ya mchezo husika si vyema sana mpinzani wako kumfumga magoli mengi kupitiliza. Likewise kwenye politics, wanaofanya siasa ni wanasiasa kwa ujumla wao bila kujali itiladi. Ili tuendelee kuwaheshimu ni vyema wakajiheshimu. Kwa hivyo si mbaya kwa M-ccm ama M -cuf kumpa ushauri M-udp na kinyume chake.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom