akajasembamba
JF-Expert Member
- Dec 24, 2010
- 1,012
- 1,475
Nilisikitishwa na kufadhaika sana, kuona baadhi ya wananchi wa jimbo la Igunga wakiangua kilio na baadhi yao kupoteza fahamu kisa Mbunge wao Rostam Aziz kajiuzulu! Mbunge aligubikwa na tuhuma na kashfa lukuki,ambaye Tanzania nzima ilikuwa ikipaza sauti ya kumkataa wakiwemo wana CCM wenyewe! Mbunge ambaye Bungeni hachangii hata hoja moja kimya muda wote, alinukuliwa bunge lililopita kukaa kimya miaka yote! Najiuliza Wanyamwezi hawa wanaelewa haswa maana ya Mbunge?!
Au kwao wao ni MFADHILI anayegawa tu pesa na kugawa Mahindi na Vyerehani!!Bila kujua hizo gharama anazotumia pesa amezitoa wapi!! Anatoa hela mfukoni wakati bungeni anaachia mabilioni ya fedha zinazotokana na kodi walizotozwa wao wenyewe katika madini, mazao yao na ng'ombe wao yakipotea katika Bajeti mbovu!
Wanategemea maendeleo ya nchi yataletwa kwa fedha za mfuko wa mfanyabiashara mmoja na siyo Mbunge mwenye hoja nzito bungeni, anayehoji zinapokwenda fedha zinazotokana na madini yetu!! Wanatabora hao hao hatukuona wakilia walau tone moja kumlilia Mbunge GODWIN SELELEIII ambaye Watanzania wengi wenye fikra timamu walikuwa wakimpenda na kumtegemea kama mtetezi wao bila kujali ni wa chama gani!
Huu mkoa una tatizo wajiangalie upya.
Au kwao wao ni MFADHILI anayegawa tu pesa na kugawa Mahindi na Vyerehani!!Bila kujua hizo gharama anazotumia pesa amezitoa wapi!! Anatoa hela mfukoni wakati bungeni anaachia mabilioni ya fedha zinazotokana na kodi walizotozwa wao wenyewe katika madini, mazao yao na ng'ombe wao yakipotea katika Bajeti mbovu!
Wanategemea maendeleo ya nchi yataletwa kwa fedha za mfuko wa mfanyabiashara mmoja na siyo Mbunge mwenye hoja nzito bungeni, anayehoji zinapokwenda fedha zinazotokana na madini yetu!! Wanatabora hao hao hatukuona wakilia walau tone moja kumlilia Mbunge GODWIN SELELEIII ambaye Watanzania wengi wenye fikra timamu walikuwa wakimpenda na kumtegemea kama mtetezi wao bila kujali ni wa chama gani!
Huu mkoa una tatizo wajiangalie upya.