Wana Simba SC wenzangu tuvumiliane ila ukweli wa mechi yetu ya tarehe 23 August, ni huu

Hivi si nilishawaambieni huko nyuma nilipokuja humu JF na hili neno la POPOMA kuwa Mimi niliyelileta sitakiwi kuitwa nalo? Kwahiyo na Mimi GENTAMYCINE leo nimekuwa POPOMA? Hebu nitake radhi upesi Mkuu au tengua haraka Kauli yako hiyo.
MPWA NAHISI WANATAKA
KUKUTOA MHANGA KATAA KABISA HILO NENO
 
Mkuu GENTAMYCINE, naomba uje utoe ufafanuzi tena, maana Simba wanarejea Dar bila kupita katika bandari hizo


View attachment 571427
HAhahaaa kupitaa utaalaamu yakinifu jamaa wamegonga kote bandarini na airporr

Nenda soma juu kipengele cha bandari dar na bandari znz(watu....)..nikwamba hapo labda mpande treni ya znz dar .ila aiport na bandarini kote kazi imeisha
 
Du ww jamaa umenichekesha sana

Sent using Jamii Forums mobile app


Labdaa niwasaidie
Simba mpaka wanafika airport wamefungwa kamoja...wakategewa pale vip...walichojichangany wakauzwa na mtu wasipite norma gate ..hahahaaaaaaa pale tukaongeza bao mbili ila kwa makubaliano ya kufungwa moja

Wanamahesabu ukichukua la znz na la VIP..Unaweza jua simba anakula ngapi leo
1-0
2-1
Nipe total...napita tukutane ....uwanjani

RIP ALI YANGA
 
Najua mtaumia ila kama kawaida yangu mechi ya mwisho ya Simba na Yanga nilikuja humu humu JF na kusema kuwa Yanga itafungwa kwa tofauti ya goli 1 na kwa kwamba kutakuwa na Kadi nyekundu na kweli ndicho kilichotokea na wengi wenu mlinitumia salamu nyingi sana za pongezi japo wapo ambao kabla ya mechi ile kuanza walinidhihaki na kunitukana mno humu Jamvini.

Basi wana Simba SC wenzangu kwa moyo ule ule ambao mlinipa wakati ule naomba leo tena zikiwa zimebaki siku tano ( 5 ) kuelekea huo 'mtanange' wa Dar es Salaam / Mzizima derby ya Simba na Yanga pia na leo mnivumilie na bahati nzuri hata Mimi ni mwana Simba SC mwenzenu tena wa Kindakindaki.

Nipo katika Kamati moja 'Nyeti' ambayo mechi iliyopita tulijitoa sana mhanga hadi kupelekea karibu kuhatarisha hata maisha yetu ili tu Simba SC yetu ishinde na kweli ilishinda. Kataeni kubalini ila mjue kwamba mechi hizi huwa zinachezwa mno 'Kiutamaduni' zaidi na pale Uwanjani huwa ni uwasilishaji tu wa 'majini' na 'tunguri'.

Ni kwamba hii mechi tumeicheza muda mrefu ila ni bahati mbaya sana kwamba Watani zetu Yanga FC 'wameshatutega' sehemu mbili kwanza Bandarini Dar na pale Bandarini Zanzibar ( Watu wa mpira hapa najua mtanielewa ) lakini kama haitoshi walipoenda Yanga FC ni kwa Mtu ambaye siku zote amekuwa 'akituumiza' Simba SC kwani alishawahi kuwa 'Mtaalam' wetu mkubwa ila mmoja wa Viongozi wetu ( ambaye sasa yupo ndani ) alimdhulumu Pesa yake na Yanga FC japo hawana Hela ila wamemfuata huyo huyo kama walivyofanya huko nyuma na mara zote walitufunga.

Ukweli kamili wa mambo ni huu ufuatao na sikulazimishi uukubali ila tunaoihangaikia Simba SC 'Kiutamaduni' hatuna busi kuliweka hili mapema ili wana Simba SC kuanzia leo Ijumaa tuanze kujiandaa Kisaikoloji japo mbele ya Mungu lolote linaweza kutokea na lisitokee ila Mimi hapa nawasilisha 'ripoti' ya masuala yetu haya ya 'Kiutamaduni'.

1. Simba SC tutafungwa goli 1 tena Kipindi cha Kwanza

2. Kuna Kadi Nyekundu za kila Upande ila upande mmoja utamkosa Mchezaji wao muhimu

3. Kipindi cha pili mpira utasimama kwa muda kwani kuna Mchezaji ataumia vibaya

4. Kuna fujo kubwa sana itatokea wakati wa Mapumziko katika moja ya Jukwaa

5. Kuna Nyuki watakatiza Uwanjani ila kuna Njiwa watarushwa na hawataruka

6. Kuna goli litafungwa ila litakataliwa

7. Huenda kabla ya mechi au siku ya mechi au baada ya mechi mmoja wa Viongozi wa hizi Timu tusiwe nae tena duniani

Mtaalam wetu wa mwisho aliyeko Morogoro kasema kuwa anaweza 'Kuicheza' hii mechi na Simba SC tukashinda ila amesema kuwa inabidi 'Kiongozi' mmoja wa Kamati ya Utendaji au wa Matawi ajitoe 'mhanga' Kufa ili 'Nyota' ifunguke kwani 'Kufuru' ambalo Yanga FC wametufanyia Simba SC ni la hatari mno.

Najua fika kuwa Wana Simba SC wenzangu tuna jeuri kwakuwa tuna Kikosi kizuri na imara kuliko Yanga FC na wala hili halina 'ubishi' ila tambueni kuwa hizi mechi huwa zinachezwa sana 'Kiutamaduni / Kindumba' na kuna mengine yanafanyika ambayo nisingependa kuyaweka hapa hadharani kwani naweza nikawatisha au kuwakatisha Watu tamaa.

Hata hivyo Mwenyezi Mungu nae ana yake hivyo wana Simba SC msikate tamaa labda Maulana anaweza kutusaidia na tukashinda ila hadi muda huu tunamaliza 'Kuhangaika' kwa hawa 'Wataalam' wetu bado kuna goli 1 ambalo Yanga FC wanaenda kutufunga na litakuwa la Kipindi cha Kwanza na litakuwa goli lisilo hata na utata wowote.

Naomba radhi kwa nitakaowakera kwa hii taarifa ila nimeona nisiwaficheni kwa kinachoendelea!

Nawasilisha.
Nasubiri kwa hamu kuona.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom