Huyu Abdlaziz Makame ni bonge la kiungo Fei Toto na Mkude wanasubiri. Kama kweli kapona vizuri goti lake na atarudi kuwa fiti ligi ijayo itakuwa na ushindani sana. Tatizo la timu zetu sio risk taker. Huyu jamaa aliumia kama sikosei goti kwenye challenge cup Kenya kama miaka miwili iliyopita. Lakini hakuna klabu iliyotaka kumtibu ili ije imtumie baadae. Jamaa akaamua kukaa pembeni mwaka mzima anajitibu goti. Leo karudi uwanjani Simba na Yanga zinapigana vikumbo na inasemekana Yanga wamefanikiwa kumpata.
Kwa kuwa ni mchezaji mzuri timu makini ingemchukua wakati mgonjwa kwa mkataba wa kumtibu baada ya kufanya assessment ya majeraha yake na kumpa mkataba rafiki ambao ungekuwa wa faida kwa pande zote mbili. Ila timu zetu zinapenda sana ready made na kwa mtindo huu huwa tunapoteza sana vipaji vizuri kwa wale wachezaji wasioweza kujitibu.
Kwa kuwa ni mchezaji mzuri timu makini ingemchukua wakati mgonjwa kwa mkataba wa kumtibu baada ya kufanya assessment ya majeraha yake na kumpa mkataba rafiki ambao ungekuwa wa faida kwa pande zote mbili. Ila timu zetu zinapenda sana ready made na kwa mtindo huu huwa tunapoteza sana vipaji vizuri kwa wale wachezaji wasioweza kujitibu.