Wana MATAGA tunawaza, jamaa yetu ataacha LEGACY ipi? Maana haka ka corona kamevuruga mapato, na miradi haijaisha

chiembe

JF-Expert Member
May 16, 2015
11,996
20,644
Sisi MATEGE msituone tuko kimya, tuna mawazo sana, tulijua tungemaliza miradi mingi 2021, baada ya hapo tukaanza nyimbo za kuimba na kusifu mafaniko na kumpa send off jamaa yetu iliyojaa furaha na jina lisilosahaulika kwa wananchi.

Ng'ombe wa masikini hazai, kamekuja ka korona, biashara zimesimama,kodi hazilipwi, na sisi wakandarasi wako saiti wanasubiri hela.

Kwa kawaida wanapoondoka, hupenda kuacha alama za kukumbukwa, naona miradi ya alama inaweza isiishe,na wataalam wanasema haka ka kirusi kanaweza kurandaranda mtaani kwa miaka miwili mpaka 2022, sasa tunabakiza miaka miwili au mmoja na nusu, hapohapo tufufue uchumi,ndipo tupate hela za kumalizia miradi.

Halafu huwa inakuwaje kwamba kipindi cha pili cha uongozi huwa kanatokea ka kitu kanakomfanya aliyeshika hatamu aonekane namna gani mbele ya jamii?
 
Corona tutaishinda Mkuu

Tuendelee kuchukua tahadhari zinazotolewa na viongozi wetu wa Afya kuhusu kupambana na corona
 
Hivi hii kweli inaingia akilini kuona mtu anashangilia ikikwama miradi ya maendeleo ambayo faida zake zingenufaisha wote akiwemo na yeye na nduguze au uzao wake, wanufaika ni wale wanao mchukia Magufuli na wanao mpenda?
 
Kweli inaingia akilini mtu anashangilia gonjwa la Corona linauwa watu kisa kiongozi wa nchi ashindwe kuleta maendeleo?
Mkuu huwezi jua next victim atakuwa nani, wewe, nduguyo au mimi au huyo unaye mchukia. Wewe huna exception katika kupata maambukizi ya hili gonjwa au pengine kupata madhara mabaya kabisa ya gonjwa hili.

Siasa zingine za ajabu sana na kujitoa ufahamu.
 
Hivi hii kweli inaingia akilini kuona mtu anashangilia ikikwama miradi ya maendeleo ambayo faida zake zingenufaisha wote akiwemo na yeye na nduguze au uzao wake, wanufaika ni wale wanao mchukia Magufuli na wanao mpenda?
Hao ni misukule ya ufipa
 
Sisi MATEGE msituone tuko kimya, tuna mawazo sana, tulijua tungemaliza miradi mingi 2021, baada ya hapo tukaanza nyimbo za kuimba na kusifu mafaniko na kumpa send off jamaa yetu iliyojaa furaha na jina lisilosahaulika kwa wananchi.

Ng'ombe wa masikini hazai, kamekuja ka korona, biashara zimesimama,kodi hazilipwi, na sisi wakandarasi wako saiti wanasubiri hela.

Kwa kawaida wanapoondoka, hupenda kuacha alama za kukumbukwa, naona miradi ya alama inaweza isiishe,na wataalam wanasema haka ka kirusi kanaweza kurandaranda mtaani kwa miaka miwili mpaka 2022, sasa tunabakiza miaka miwili au mmoja na nusu, hapohapo tufufue uchumi,ndipo tupate hela za kumalizia miradi.

Halafu huwa inakuwaje kwamba kipindi cha pili cha uongozi huwa kanatokea ka kitu kanakomfanya aliyeshika hatamu aonekane namna gani mbele ya jamii?
Jiwe kupata u-Rais ilikuwa ni ajali. Matokeo ya ujinga wa JK kumlazimishia Benard Membe awe next President badala ya hasimu wake na rafiki wa zamani Lowassa ndiyo yaliyompa huyu fursa kuwa Rais.

Wazungu husema "Fortune favours fools". Yaani bahati huwaendea wapumbavu. Jiwe ametumia U-Rais wake kukomoa maadui zake binafsi kwa kuwafukuza makazini, kuwatupa rumande kwenye kesi zisizo na ushahidi na kutumia hazina ya Serikali kufanya miradi mikubwa isiyo na tija. Yeye Ali Mradi anapata 10% yake hajali kujenga dude lolote.

Legacy atakayoacha itakuwa sawa na aliyoacha Mobutu Seseseko wa iliyokuwa Zaire.
 
Hivi hii kweli inaingia akilini kuona mtu anashangilia ikikwama miradi ya maendeleo ambayo faida zake zingenufaisha wote akiwemo na yeye na nduguze au uzao wake, wanufaika ni wale wanao mchukia Magufuli na wanao mpenda?
Miradi gani? Miradi isiyo na feasibility study
na isiyoheshimu environmental impact assessment ni misuse of money. Acheni kushangilia ujinga,
 
Kweli inaingia akilini mtu anashangilia gonjwa la Corona linauwa watu kisa kiongozi wa nchi ashindwe kuleta maendeleo?
Mkuu huwezi jua next victim atakuwa nani, wewe, nduguyo au mimi au huyo unaye mchukia. Wewe huna exception katika kupata maambukizi ya hili gonjwa au pengine kupata madhara mabaya kabisa ya gonjwa hili.

Siasa zingine za ajabu sana na kujitoa ufahamu.
Kaka hata watoto wa wachawi wanaopaa na ungo huwa wanaendesha magari ya mamilioni barabarani, ukikutana nao wala huwezi kuitambua asili ya wazazi wao.
 
Jiwe kupata u-Rais ilikuwa ni ajali. Matokeo ya ujinga wa JK kumlazimishia Benard Membe awe next President badala ya hasimu wake na rafiki wa zamani Lowassa ndiyo yaliyompa huyu fursa kuwa Rais.

Wazungu husema "Fortune favours fools. Yaani bahati huwaendea wapumbavu. Jiwe ametumia U-Rais wake kukomoa maradhi zake binafsi kwa kuwafukuza makazini, kuwatupa rumande kwenye kesi zisizo na ushahidi na kutumia hazina ya Serikali kufanya miradi mikubwa iliyo na tija. Yeye Ali Mradi anapata 10% yake hajali kujenga tube and lolote.

Legacy atakayoacha itakuwa sawa na aliyoacha Mobutu Seseseko wa iliyokuwa Zaire.

Uko sahihi! Angalia mamilioni aliyoyatumia kujengea Ikulu yake ya kisasa Chamwino Dodoma! Kisa tu eti Rais wa Kwanza alitamani makao makuu ya nchi yawe Dodoma! For what!! Halafu bora hata angekuwa anaishi basi! Muda huu anaishi kwenye Ikulu yake nyingine isiyo rasmi ya Chato!

Sasa Ikulu ya Magogoni atamuachia nani! Si wangeweka tu mgawanyo wa kimamlaka! Dodoma ungebakia kuwa mji wa Kibunge, Dar ungebakia kuwa mji wa Kiserikali, nk.

Tumepatwa!! JK Mungu anakuona. Na hii dhambi uliyotufanyia Watanzania, itakuletea majuto ya moyoni, kwenye maisha yako yote hapa duniani.
 
Kweli inaingia akilini mtu anashangilia gonjwa la Corona linauwa watu kisa kiongozi wa nchi ashindwe kuleta maendeleo?
Mkuu huwezi jua next victim atakuwa nani, wewe, nduguyo au mimi au huyo unaye mchukia. Wewe huna exception katika kupata maambukizi ya hili gonjwa au pengine kupata madhara mabaya kabisa ya gonjwa hili.

Siasa zingine za ajabu sana na kujitoa ufahamu.
Mkuu,janga ni fact, ujifiche au use me,lipo
 
Back
Top Bottom