Ndugu zangu wana- Mara tuamke sasa nasi tudai vivutio vyote vya kitalii vitangaziwe Mara, kama moja wapo ya kuleta maendeleo katika Mkoa wa Mara. Kama wengi mjuavyo hasa Mbuga ya Wanyama iliyopo Wilaya ya Serengeti imekuwa siku zote ikiwanufaisha watu wa Arusha na Mkoa wetu kusahaulika kabisa. Mkoa wetu umejaliwa sana Mali asili pamoja na Dhahabu lakini maendeleo hakuna. Arusha kuna madini ya Tanzanite one pamoja na Mlima Meru lakini kiuchumi wako juu kuliko sisi.Najua kabisa watalii wanaoenda Arusha moja kwa moja badala ya kupita Mara ili wananchi wa eneo husika wanufaike na ujio wao, wanasababishwa na mipangilio mibovu iliyowekwa na watangulizi wetu. Sasa ifikie wakati nasi watujali