Wana-mara tudai mapato ya mbuga ya wanyama ya serengeti yajemara na siyo arusha.

tata mura

JF-Expert Member
Sep 27, 2012
275
49
Ndugu zangu wana- Mara tuamke sasa nasi tudai vivutio vyote vya kitalii vitangaziwe Mara, kama moja wapo ya kuleta maendeleo katika Mkoa wa Mara. Kama wengi mjuavyo hasa Mbuga ya Wanyama iliyopo Wilaya ya Serengeti imekuwa siku zote ikiwanufaisha watu wa Arusha na Mkoa wetu kusahaulika kabisa. Mkoa wetu umejaliwa sana Mali asili pamoja na Dhahabu lakini maendeleo hakuna. Arusha kuna madini ya Tanzanite one pamoja na Mlima Meru lakini kiuchumi wako juu kuliko sisi.Najua kabisa watalii wanaoenda Arusha moja kwa moja badala ya kupita Mara ili wananchi wa eneo husika wanufaike na ujio wao, wanasababishwa na mipangilio mibovu iliyowekwa na watangulizi wetu. Sasa ifikie wakati nasi watujali
 
Hili siyo swala la kudai kwa maandamano kwani ni la kibiashara zaidi kuliko siasa. Ni kujitambua na kuona namna ya kutumia fursa. Linahitaji investment na mikakati ya mtu mmoja mmoja na makundi ya watu. Mfano kuvutia kampuni mpya na zilizopo ku operate kutoka mara. Ila mtahitaji kuwa na uwanja wa ndege wa kimataifa na pia kuweka mazingira mazuri kwa wafanyabiashara kuanzisha na kuoperate kutoka arusha.
 
Back
Top Bottom