Wana JF tumwambie Rais Magufuli kwa kauli moja, amfukuze kazi Waitara

Waangalie mawaziri kama lugola, mpina, kigwangala na ata waziri Mpya wa viwanda. Utagundua wana Sifa moja kubwa. Uwezo wa akili unafanana sna.
 
Mi uwa nashangaa sana nchi hii Mtu anayeshutumiwa sana ndio upandishwa cheo.

Ila wachapakazi ndio upotea na kutoweka na kufanyiwa Rafu.


Mtu kama Bashe anakosa wizara mtu kama Lugola na Waitara eti ni mawaziri.

Halafu unajiuliza kwanini tupo hapa tulipo?
Mkuu alisema wale wanaongea sana bungeni siwateui ng'o, wanatakiwa mazombi kuteuliwa hawezi kuteua wanaojielewa.
 
"Msaliti hawezi kuachwa hivi hivi akisavaivu" (Magu, 2017). Kesho yake kilichotokea pale Dodoma "Area D" wote ni mashahidi. Huyu ndiye wakumshitaki kwa mahakama na kwa Mungu. Waitara cha mtoto. Hana hata asiyejulikana mmoja wa kumlinda.
 
Huyo unaemtetea unajua anachokifanya sasa huko ubeligiji?????Lissu kwa sasa yupo mkwenye mkakati mzito sana na watu wenye MASLAHI YAO NCHINI TANZANIA,leo hii tunaambiwa kachangiwa zawadi ya GARI NA WATANZANIA waishio belgium HIKI NI KITUKO CHA KARNE hao watanzania waliopo GIZANI HAPO BELGIUM tunawaslimia sana.....A
seme tu ukweli hilo gari kapewa na watu alio nao kwenye mkakati maalumu wa wao kumfadhili kwa hali na mali achukue URAIS wa nchi hii.....
KILA SIKU TUNASEMA HUMU LISSU hatibiwi hapo BELGIUM anatuadahaa tu sisi WATANZANIA kuna uchafu mkubwa sana HUYU JAMAA ANAANDALIWA KUULETA NCHINI TANZANIA kulinda MASLAHI YA HAO WAP.U.UZI wenzio
NA HATUTAKUBALI HUU UPUUZI WAKE.......
hii post mbona Kama ya yule mwandishi wa gazeti la jamvi la habari
 
Labda wangekufukuza wewe kwanza huko ulipo then tutafikiria upya..jambo lisilokuwa na ushahidi wa kimahakama unalitamkaje hapa..we vip bana. Acha wivu wa kitoto wacha achape kazi...najua issue ni uwaziri wake...bahati ya mwenzio usiilalie mlango wazi
Wewe kweli ni "Babeli" Tuambie ni Babeli ile ya kale au ni huyu Mama wa Makahaba!!!?
Hoja Ni kuwa Waitara Ni kiongozi, tena Waziri ambaye ofisi yake iko chini ya Ikulu. Tunahitaji ushahidi gani wakati hajakanusha kuwa siyo yeye anayetoa povu kwenye clip inayozunguka. Hakuna Cha wivu, hatuwezi kuacha kuwakemea viongozi walevi na kuwaacha watekeleze nia zao ovu dhidi ya Watanzania.
Unapaswa kujua kuwa kule Ujerumani Hitler hakuwa peke yake. Walikuwepo akina Goering waliotenda ukatili hata kuliko Hitler mwenyewe. Hivyo basi tuungane kusema kwa sauti: Waitara must Go!!!
 
"Give them enough rope to hang themselves " Tuwaambie ili wajue kuwa wapo watu ambao hawakubaliani na hiyo kauli. Tumwambie mkuu Waitara must go.
Definitely, Ni wazimu kuwa na kiongozi anayetangaza hadharani tena akiwa mbele za watu kwamba serikali ikikosolewa basi imekwamishwa!!! Haya kama si mawazo ya enzi za ujima nini hasa.
Mhe. Rais, wewe ni Rais wa nchi yetu, umeapa kuwalinda Watanzania wote bila kujali ni wazima, wagonjwa, vilema au hata vichaa. Kwa Katiba na sheria zetu ni Mahakama tu plus saini yako ndivyo vinaweza "kumtanguliza" mtu aliyefanya makosa hata ya uhaini.Sasa Waitara Ni nani hata atamke kutanguliza watu. Hivyo Mhe Rais timiza wajibu wako, mfukuze Waitara serikalini. Waitara must Go!!!
 
Mkuu Zakaria, acha kumuonea wivu wa bure Waitara.

Huu utakuwa wivu tuu, Waitara afukuzwe kwa kosa gani?.

Wewe ungekuwa mpiginia haki wa ukweli, ungeanza na aliyezungumzia "msaliti hawawezi kuachwa hivi hivi akisurvive tuu" ndipo kwa Waitara, vinginevyo ni wivu tuu wa maendeleo ya Waitara unakusumbua.
P
HAHAHAAAAAAAAAAAAAA......MANENO MAZITO SANA HAYA PASKALI KHAAAAA!!!
 
Yeye huwa hapangiwi...
Hapangiwi!!!? Labda na Mabeberu, lakini sisi Wananchi lazima tumpangie. Moja la muhimu la kumpangia ni kumwondoa Waitara ofisini kwake Tena kwa kumfukuza kazi. Haiwezekani Waziri tunayemlipa sisi ale njama ya kutaka "kumtanguliza" Mtanzania mwenzetu kinyume Cha Katiba na Sheria zetu, halafu kiongozi wetu mkuu aliyemteua mtu huyo adai "hapangiwi!!!" Kwa hili atambue kuwa Waitara must Go!!!
 
Ni kweli mkuu ila kumbuka nchi kwa sasa inaongozwa kidikteta sheria kufuatwa inahitaji hisani binafsi ya rais.

Kwa sasa hata ile haki ya kukusanyana na kutoa maoni yenu ya moyoni kupitia makongamano mbalimbali ya haki za binadamu na mikutano ya vyama vya siasa ni marufuku labda iwe ya kusifu juhudi za serikali.

Halafu kumbuka Magufuli pia aliwahi kusema kuwa "nashangaa sana kuona wasaliti wakiendelea kusurvive hadi sasa" hii ilikuwa ni ndefu kidogo nimeifupisha tu, hii aliitoa baada ya Lissu kuikosoa ripoti ya madini maarufu makinikia na kuiita uchafu wa kitaaluma, kweli baada ya muda mfupi Lissu alipigwa risasi.

Kwa mazingira haya inahitajika nguvu kubwa ya umma kuwashinikiza kutenda kadri ya katiba na sheria za nchi hii zinavyotaka, najua wananchi wakiamua hakuna mtawala anaweza kubaki madarakani.
Iwapo Rais alisema maneno uliyonukuu basi alikosea. Sasa tusimruhusu kutoa matamshi ya aina hiyo, na njia muafaka ni kumwambia wazi kuwa kila . Mtanzania ana haki ya kuishi Hadi mahakama itoe hukumu ya kifo na Rais aidhinishe kwa saini. Si kinyume chake. Rais kwa kujua hatari ya matamshi ya aina hiyo amchukulie Waitara hatua. Amfukuze kazi maana Hakuna namna: Waitara must Go!!!
 
16 Reactions
Reply
Back
Top Bottom