RockCarnegie
JF-Expert Member
- Jan 17, 2019
- 963
- 1,927
Great thinkers,
Leo ninawaomba jambo muhimu linalohusu uhai wa mwana JF mwenzetu: Tundu Lisu ulio hatarini.
Mtu aliyejipambanua kuyaweka maisha ya Lissu hatarini ni Naibu Waziri wa TAMISEMI Wizara iliyo chini ya ofisi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Waziri Mwita Waitara amesikika wazi kwenye mitandao akihamasisha mipango ya "kumtanguliza mtu." Ukweli ni kuwa Waziri huyu anahamasisha mauaji ya Watanzania wasiokubaliana na mtazamo wa Serikali na sote tunajua Mtanzania namba moja asiyekubaliana na sera za Serikali hii hasa zinazosimamia maendeleo na haki za binadamu ni Tundu Lissu. Sasa Waitara anatamka wazi "kumtanguliza" bila kuwajibika!!!
Wana JF tumtake, si kumwomba Mhe Rais wetu mpendwa amwondoe Waitara Serikalini vinginevyo Serikali yake itaonekana wazi kuwa inapanga na kutekeleza matukio ya utekaji na mauaji ya Wananchi.
Ukweli ni kuwa Mwalimu Nyerere, Baba wa Taifa letu aliwahi kutuasa kuwa "Ikulu ni mahali Patakatifu" hivyo hatutegemei pawe mahali pa kupanga "kuwachinja" Watanzania wenzetu kwa sababu yoyote ile.
Mhe Rais huwa anapita humu, wana JF tuko zaidi ya laki tano, hivyo anapaswa kutusikiliza, tukiungana wote kwa pamoja tutasikilizwa. Waitara Must Go.
Nina mashaka na Jiwe kukubali rai yako, kwani Waitara anaƴasema hayo kwa kuwa yanamfurahisha boss wake!
Kama msimamo wa Jiwe ungekuwa kinyume na tamko la Waitara, mteule huyu asingeweza kufungua mdomo na kutamka kuondoa uhai wa TL wazi wazi bila hofu!
Kwa kuwa tumemujua nia yake tuweke kumbukumbu, ili mda muafaka ukifika Waitara na kundi lake wapelekwe mbele ya sheria!