Ndugu wana JF mimi ni mwanafunzi wa chuo kikuu Mzumbe mkoani morogoro niko mwaka wa kwanza nachukua shahada ya production and operation management niliwahi kusoma seminari ya Mtakatifu Maria Visiga kwa O-level na baadaye Ilboru special school kwa A-level , sasa marehemu mama yangu alikuwa mwandishi wa vitabu vya hadithi za watoto na mimi nikazaliwa na kipaji cha uandishi , nikageuka mtunzi wa vitabu, mashairi n.k , mpaka gazeti la Dira wakanikubali na kwasasa naandikia kwenye gazeti hilo kama mchambuzi upande wa makala za kisiasa na kihistoria. Sasa kinachonichanganya akili ni kuwa licha ya watu kukiri kuwa nina uwezo wa kuandika na kutunga ila bado hawako tayari kunisaidia, huku wakijua gharama za uchapaji ni kubwa mno sitoweza ku-afford, katika purukushani zangu nimefanikiwa kusajili kampuni yangu iitwayo Vijana Intellectual Company mwaka huu mwanzoni mwa mwezi wa tano ila sina pesa za kuchapa vitabu , wengi wa watu wanaojifanya wanasaidia ni wagumu mno na ni matapeli wa mjini, kwasasa nina umri wa miaka 21 ni kijana wa kiume na ni mtanzania pure kabisa . Huwa nafikiria kusubiri labda baadae nitakapokuwa na fedha za kutosha kuchapa lakini hofu yangu ni kuwa kwasasa ndiyo kijana mbichi na nguvu na akili yangu inachemka sana hivyo ni heri nikachakarika kutunga sasa kabla uzee haujaninyemelea, hivyo lengo hasa la kuja hapa jamvini ni kuwa natafuta mtu aliyetayari kunifadhili au kusimamia kazi zangu ili zichapwe na kusambazwa awe mtu mwenye uzoefu na aliyetayari kukuza vipaji vya vijana, awe na maono na mtazamo wa kimaendeleo mimi niko tayari hata kuingia mkataba naye ila cha msingi awe serious na kazi sitaki longolongo au blah blah, kifupi sipendi porojo za kupotezeana muda,naweza kuandika kwa lugha mbili yaani kiingereza na kiswahili kwa ufasaha kabisa bila matatizo yoyote, hivyo tafadhali aliyetayari tuwasiliane tuanze kazi haraka, sipendi kufa na kipaji changu nataka kuacha urithi kwa taifa letu na ulimwengu mzima...ASANTENI SANA
Contacts zangu ni 0717-709618 au novakambota@gmail.com
Contacts zangu ni 0717-709618 au novakambota@gmail.com