mi ni graduate,ktk kutafuta Kali nimeshapatwa na masahibu mimi had nashindwa nifanyeje,yote ya kutakwa kimapenzi.hivi hay yataisha kweli?coz naona kama nimejichokea kwa sasa,
Mtoa mada njoo ujieelezee vizuri wengi hatujakuelewa uliposema kutafuta kali, kama ulimaanisha kazi unaweza kutumia elimu yako kujiajiri mwenyewe na maisha yakawa bomba tu, usijali sana unaweza kuanza hata kwa kuuza vitumbua,nyanya au pipi, kwa kuwa unaelimu nzuri baada ya muda fulani biashara yako itakuwa kubwa na kuwasaidia wasio na elimu kwa ajira ndogondogo. Mlio na elimu wote tumieni limu zenu kulisaidia taifa siyo taifa liwasaidie.
Shosti hayo sio masaibu,na nenda katafute kazi kama mwanamke unaejiamini na usijishushe thamani yako eti kisa upate kazi
kama rizki yako utaipata bila kuvuliwa nguo...
mi ni graduate,ktk kutafuta Kali nimeshapatwa na masahibu mimi had nashindwa nifanyeje,yote ya kutakwa kimapenzi.hivi hay yataisha kweli?coz naona kama nimejichokea kwa sasa,
Mvumilivu hula mbivu, endelea kutafuta tu iko siku usiyoijua utapata. Usikabali kudhalilishwa kwa ajili ya ahadi za kazi. Wapo waliowavulia nguo hao mabosi na mpaka leo hawajapata kazi na mbaya zaidi wameambulia magonjwa tu ...
Take care na Muombe Mungu pia.
ni jambo la kawaida sana sikuhizi ofisi zimejaa rushwa tupu hasa za ngono! Hicho kisiwe kikwazo kwako bali changamoto kwako! Usichoke kwani si kila offisi ina rushwa!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.