GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,385
- 108,455
Nikiwa kama Mmoja wa Watu niliochukizwa kama siyo kukasirishwa na Kitendo Bondia Mwakinyo cha Kumdhihaki Bondia mwenye Historia iliyotukuka hapa Tanzania Rashid Matumla hadi GENTAMYCINE nikaanzisha Uzi wa Kumsema ambao uliibua Hasira Kali za Watanzania zilizosambaa sehemu mbalimbali hatimaye leo hii kupita Azam Tv Bondia Mwakinyo amemuomba Radhi Matumla na Watanzania wote kwa ujumla tukiwemo Mimi na Wewe.
Hivyo nasi hatuna budi Kiungwana kabisa Kumsamehe na Kuanzia sasa tuweke Silaha zetu chini na tumsaidie akue Kimchezo.
Kwa wale wenye Kumiliki Visimbusi / Vingamuzi vya Azam Tv leo Saa 3 na Nusu msikae mbali na Runinga zenu kwani kutakuwa na marudio yote ya tukio zima ambapo Bondia Mwakinyo alionyesha Heshima ya juu kwa ' The Legend 'Rashid Matumla huku Rashid Matumla nae akionyesha kuwa kweli Yeye ni Mkongwe na amekomaa katika Tasnia hiyo ya Ndondi nchini ambapo nae hakuonyesha ' Kinyongo ' na muda wote alikuwa akimkumbatia Kiupendo na Kumtia Moyo Bondia Mwakinyo hali ambayo inaonyesha kuwa Bondia Mwakinyo amejutia lakini pia amejifunza Kitu na sasa atabadilika.
Kwa wale ambao mlikuwa mnaudharau huu Mtandao wa JamiiForums fikirieni upya kwani kama hamjui na kwa taarifa yenu tu ni kwamba hakuna Mtandao wa Kijamii nchini Tanzania ambao unaibua mambo mengi na una ' Influence ' kubwa ndani ya Jamii ya Watanzania kama huu. Ni Maudhui na Maoni ya huu Mtandao hasa juu ya Uzi niliouanzisha na ambao wengi wenu mlichangia ndiyo umeweza Kuamsha ari kwa Watanzania wengi hadi Kupelekea na Waandishi wa Habari za Michezo nao Kufuata mtiririko na Uzi mzima hadi leo Mwakinyo ameamua Kusalimu Amri na Kuomba Radhi.
Katika hili kila mwana JamiiForums ni Mshindi hivyo unapokuwa hapa jione kuwa Wewe ni sehemu Kuu ya Mabadiliko Kijamii.
Hivyo nasi hatuna budi Kiungwana kabisa Kumsamehe na Kuanzia sasa tuweke Silaha zetu chini na tumsaidie akue Kimchezo.
Kwa wale wenye Kumiliki Visimbusi / Vingamuzi vya Azam Tv leo Saa 3 na Nusu msikae mbali na Runinga zenu kwani kutakuwa na marudio yote ya tukio zima ambapo Bondia Mwakinyo alionyesha Heshima ya juu kwa ' The Legend 'Rashid Matumla huku Rashid Matumla nae akionyesha kuwa kweli Yeye ni Mkongwe na amekomaa katika Tasnia hiyo ya Ndondi nchini ambapo nae hakuonyesha ' Kinyongo ' na muda wote alikuwa akimkumbatia Kiupendo na Kumtia Moyo Bondia Mwakinyo hali ambayo inaonyesha kuwa Bondia Mwakinyo amejutia lakini pia amejifunza Kitu na sasa atabadilika.
Kwa wale ambao mlikuwa mnaudharau huu Mtandao wa JamiiForums fikirieni upya kwani kama hamjui na kwa taarifa yenu tu ni kwamba hakuna Mtandao wa Kijamii nchini Tanzania ambao unaibua mambo mengi na una ' Influence ' kubwa ndani ya Jamii ya Watanzania kama huu. Ni Maudhui na Maoni ya huu Mtandao hasa juu ya Uzi niliouanzisha na ambao wengi wenu mlichangia ndiyo umeweza Kuamsha ari kwa Watanzania wengi hadi Kupelekea na Waandishi wa Habari za Michezo nao Kufuata mtiririko na Uzi mzima hadi leo Mwakinyo ameamua Kusalimu Amri na Kuomba Radhi.
Katika hili kila mwana JamiiForums ni Mshindi hivyo unapokuwa hapa jione kuwa Wewe ni sehemu Kuu ya Mabadiliko Kijamii.