Wana CCM wamshukia Dk. Slaa

Ochu

JF-Expert Member
May 13, 2008
975
47
Waandishi Wetu
Daily News; Monday,August 25, 2008 @00:02

Kauli ya Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbrod Slaa, kupinga uamuzi wa Rais Jakaya Kikwete kuwekeza fedha inayotokana na malipo ya Akaunti ya Nje (EPA) ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) katika kuinua kilimo, imeshutumiwa na baadhi ya wananchi.

Wananchi hao wamesema hatua hiyo ni ya kushangaza na kuhoji siasa za baadhi ya viongozi wa upinzani nchini akiwamo Dk. Slaa. Katika mahojiano na gazeti hili Dar es Salaam jana, Mohammed Abdul alisema kauli ya Slaa inathibitisha jinsi wapinzani wasivyoelewa siasa za nchi, maslahi ya wananchi na matakwa ya walio wengi.

“Hii ni nchi ya wakulima na wafanyakazi, sasa kuna ubaya gani kutoa fedha kuwasaidia wakulima ambao tunasema uti wa mgongo wa nchi yetu unaotegemea kilimo? Slaa aseme jingine, lakini si hili,” alisema Abdul jana akiwa katika maandamano ya wanachama wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam.

“Kauli ya Slaa ni matusi kwa mamilioni ya wakulima wa nchi hii wanaohitaji kila aina ya msaada kuhimili dhiki zao. Na kwa maoni yangu, ni viongozi kama Rais Kikwete na hatua zake wanaoweza kuwasaidia wakulima kuondokana na hali zao za sasa,” alisema mwananchi huyo.

Naye Mussa Ibrahim ambaye anaishi Temeke, alisema bila ya shaka baadhi ya viongozi wa siasa nchini wanachanganya mambo na hawaonyeshi uchungu na wananchi kama wanavyodai. “Bila kilimo, Tanzania haiwezi kwenda. Hatuwezi kupiga hatua katika uchumi kama mkulima wetu ataendelea kuwa wa hali ya chini.

Sasa Rais Kikwete anachukua hatua, watu wanaanza kumpinga. Hivi kweli wana uchungu na wananchi wetu wakiwamo wakulima. Huu si ndio ukombozi wao,” alisema. Mwanamke aliyejitambulisha kwa jina la Mary Alphonce, alisema kauli ya Dk. Slaa ni kielelezo kuwa baadhi ya wanasiasa nchini wametosheka, kwa kuwa tu wanazo fedha za kutosha, hivyo wanatoa kauli ambazo zinaonyesha wakulima kwao si kitu chochote.

“Hawa si ndiyo wanaokaa bungeni na kudai maisha ya Watanzania yamekuwa magumu…sasa Rais anatenga fedha kuwasaidia wakulima, wao wanasema anagawa fedha. Hivi afanye nini? “Sasa ni aina gani ya uongozi ambao viongozi wanataka kuendelea kushiba na kuneemeka wakati wananchi waliowaweka madarakani tunaendelea kuwa masikini zaidi,” alisema.

Naye Moses Elias wa Tabata, alimpongeza Rais Kikwete kwa uamuzi wake wa busara kuiingiza fedha za EPA katika kilimo na ruzuku ya mbolea. “Hizi fedha ambazo Rais ameziingiza katika kilimo, zitakuwa na manufaa zaidi kwa nchi hii hasa katika uzalishaji. Tuache kauli za siasa.

Ruzuku ya mbolea ni kwa Watanzania wote. Pengine Slaa hana shida kwa sababu ana uhakika wa posho ya bungeni,” alisema Elias. Katika hotuba yake bungeni Alhamisi iliyopita mjini Dodoma, Rais Kikwete licha ya kueleza mafanikio ya serikali yake tangu iingie madarakani Desemba 2005, alielezea kwa undani hatua alizozichukua kuhusu suala la EPA.

Hatua hizo ni pamoja na kuamua kuwa fedha zote zitakazolipwa na wadaiwa, ziingie katika mifuko miwili maalumu, mmoja ukiwa ni kuongeza ruzuku ya mbolea kwa wakulima na ya pili ni kutumia sehemu ya fedha hizo kuongeza mtaji wa fedha za kukopesha wakulima katika Benki ya Rasilimali Tanzania (TIB). Wananchi mbalimbali wameunga mkono hatua hizo, wakiwamo wakulima wa Songea waliokaririwa na gazeti hili jana pamoja na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), walioandamana sehemu mbalimbali nchini kupongeza hatua hiyo ambayo kwa Slaa, anaiona haifai.
 
Ukisoma kwa makini utaona kuwa aliyesema alikuwa kwenye maandamano ya CCM na ukizidi kujiuliza utakuta ukijiuliza ilikuwaje mwandishi akaenda kumuuliza mwananchi huyo swali hilo moja kwa moja huku akijua kuwa walikuwa ni wananchama wa CCM , gazeti lingeandika tuu kuwa mwana CCM amshukia Dr.Slaa na sio wananchi kama wanavyotaka ionekane.

Kwanza huyu mwanachi hajui kinachoendelea na angekuwa anajua asingekubali kwenda kwenye maandamano ya kupongeza hotuba ambayo haina majibu kwenye masuala ya msingi, asingeenda kuipongeza hotuba ambayo inawataka wezi kurudisha fedha badala ya kuswekwa ndani, asingeenda kupongeza hotuba ambayo inawafanya wezi wa EPA kuwa daraja la kwanza na ambao sheria zetu haziwahusu.

Angekuwa mwana ccm wa kweli asingekubali kuandamana kupongeza hotuba ambayo inatambua uwepo wa Serikali tatu wakati CCM ikiwa inatambua uwepo wa Serikali mbili, kwani JK alitamka kuwa kwenye masuala ya ndani ipo Tanganyika na Zanzibar ila kwenye masuala ya nje ipo Tanzania , sioni mantiki ya wananchi hawa ambao hawaoni kuwa hotuba hiyo ilikuwa ni ya kutupiliwa mbali.
 
Ikumbukwe pia kuwa alichosema Slaa ambacho naona gazeti hili la serikali linataka kupotosha ni kuwa Rais hana mamlaka ya kugawa fedha kwani hiyo ni kazi ya Bunge ,sasa kutakuwa na maana gani bunge kukaa na kupitisha bajeti huku Rais naye akiwa na fedha zake na kuamua zitumike wapi, huku ni kukiuka katiba ya nchi.
 
kusema ukweli gazeti hilo linadanganya wananchi maana alichosema Mhe slaa ni kwamba bunge ndio lina kazi ya kupanga na kupitisha matumizi ya pesa hiyo ya EPA( kama kweli imerudi)
 
Ikumbukwe pia kuwa alichosema Slaa ambacho naona gazeti hili la serikali linataka kupotosha ni kuwa Rais hana mamlaka ya kugawa fedha kwani hiyo ni kazi ya Bunge ,sasa kutakuwa na maana gani bunge kukaa na kupitisha bajeti huku Rais naye akiwa na fedha zake na kuamua zitumike wapi, huku ni kukiuka katiba ya nchi.

Katika habari inayochefua hii ni moja wapo na kwa kweli Watanzania wataidharau kupita kiasi kwa kuwa haiendani kabisa na maoni ya Watanzania walio wengi hata hao wana CCM. Ukiangalia kwa undani utaona wanataka kubadili mwelekeo na kuwa sasa tofauti ni kama fedha ziende kwenye kilimo ama la na si walioiba hizo fedha wanafanywa nini na kama hizo fedha zimerudishwa kweli na kama zimerudishwa zimerudishwa na nani na wapi na waliorudisha ni wale kweli waliofoji nyaraka, na kama ni wale waliofoji wanakwenda KEKO au kule UKONGA VIP lini? Mengineyo ni longo longo tupu ambazo Watanzania hawataelewa kamwe, Watanzania hawataelewa hata wakisheherekea kwa maandamano (yaliyofadhiliwa na mafisadi kwa kivuli cha CCM), party za Kempisk, ufadhili wa kutoa matoleo maalumu ya magazeti na kadhalika
 
Habari leo, deilenyuzi, tibisii na wachovu wengine kama Nyu habari korporesheni, uhuru na mzalendo ni virusi vya hatari katika jumuiya ya media Tanzania yenye dhamana ya nguzo ya nne ya dola.
 
Maigizo yataendelea sana mwaka huu na haswa kwenye kupindisha hoja ili jamii ichanganyikiwe na kuacha kuhoji masuala ya kimsingi.
 
yetu macho. hata hivyo watanzania bado ni wapumbavu sana. jana nilishangazwa wanaandamana na kunyeshewa na mvua eti wanaunga mkono hotuba. maajabu
 
yetu macho. hata hivyo watanzania bado ni wapumbavu sana. jana nilishangazwa wanaandamana na kunyeshewa na mvua eti wanaunga mkono hotuba. maajabu

Sidhani kama ni wapumbavu kihivyo kwani kwa mtu ambaye hajui watoto wake watakula nini na akafuatwa nyumbani na balozi ama katibu wa tawi wa CCM na kumwambia kuwa wakienda kuandamana watapewa nauli ya shilingi 5000 utafikiri anaweza kuacha kwenda?

Mtaji wa CCM ni umasikini wa watanzania, wamefanikiwa kutufukarisha na sasa wanatumia ufukara wetu kama mtaji wao wa kututawala , naamini yote kuna siku yatakwisha.
 
....walichoona ni mbolea tuu ambazo hawatazipata,kazi ipo kweli kweli kwa hawa wapiga kura.
 
Tanzaniaaa Tanzaniaaaa!!

Nakupenda kwa moyo woooteee

Nchi yangu Tanzaniaaaa

Stori zako ni tamuu saanaaa!!

Nilalapo nawaza Vijisentiiii

Niamkapo JK baba weee!

Tanzania Tanzaniaaaa

Nakupenda na EPA zakoooooo

TANZANIA!!!

TANZA NIA

The only country THAT its footballers play BUT do not win!!

The only country where Mzungu comes with one dollar and leaves with millions of them!!

The only country where ufisadi is a Prestige!!!

The only country with many toothless TUMEz!!

The only country in which its development is in Figures!! But invisible!!

The only country where both English and Kiswahili Languagez iz a problem!!

AND THE ONLY COUNTRY which its PRESIDENT keeps on SMILING despite of national difficulties!!!

I REALLY LUV THIS COUNTRY!!
 
Mwl JK Nyerere aliwahi kusema ili nchi iweze kuendelea inahitaji vitu vinne
[1]Siasa safi
[2]Uongozi bora
[3]Ardhi
[4]Watu,

hata leo nakubaliana kabisa na kauli ya Baba wa taifa.

Tanzania inashindwa kuendelea kwasababu imekosa siasa safi na uongozi bora,watu wapo na ardhi ya kutosha tena yenye rutuba ipo.

Mheshimiwa Slaa ajapinga fedha za EPA kupelekwa kwa wakulima kama magazeti ya serekali yanavyojaribu kuupotosha umma wa watanzania.Mheshimiwa Slaa alipinga rais Jakaya Kikwete kuzipeleka fedha za EPA TIB kwasababu si kazi yake bali ni kazi ya bunge.Kinachoendelea ni siasa chafu za chama cha mapinduzi za kujaribu kumchafua mheshimiwa Slaa.

Siasa chafu zinazalishwa na uongozi mbovu kama huu wa mheshimiwa Kikwete.

Wezi wa fedha za EPA walistahili kushtakiwa kwa makosa mawili makubwa 1.kugushi nyaraka 2 wizi .makosa yote haya mawili ukiyatazama kiundani nia makosa ya jinai lakini mheshimiwa rais anataka kuwaaminisha watanzania kwamba ni makosa ya madai.

Kichekesho kingine ni hayo maandamano,sijui wanaandamanaji walikuwa wanapongeza nini!!!!!!!!!!!!!!!!.

1 Hakuna fisadi hata mmoja aliyefikishwa mahakamani
2 Hakuna anayejua kama kweli fedha za EPA zimerejeshwa
3 Rais amenyakuwa kazi za bunge kwa kugawa fedha za EPA TIB [Kama kweli fedha zipo]
4 Rais kaingilia kazi za mahakama,kahukumu wezi warejeshe fedha.
5 Kitendo cha rais kuendelea kuwabeba wezi kitawapa moyo wezi wengi kuiba
 
Kuna mtu aliyewahi kusema kuwa Tanzania HATUKUSATAHILI KUPEWA UHURU MWAKA 1961.....Sasa kama mambo ni hayo......Then labda ni kweli wabongo bado hawastahili kuwa HURU.
 
Sikusikia au kusoma hotuba ya Dr. Slaa ila siamini kama angepinga hizo pesa kupelekwa kwenye bank ya wakulima. Huenda hapa tunaongelea technicalities tu na sio kupinga idea nzima.

Kwa nchi ambayo wananchi walio wengi hawana uelewo mkubwa sana na pia vyombo vya habari vilivyo vingi ni biased ni rahisi sana kupotosha nia njema ya mtu na kuifanya scandal ya kisiasa.

Naamini Dr. Slaa ni makini na hawezi kupinga hiyo idea kwasababu tu ya kupinga.
 
Kama yafuatayo ni ya kweli basi ninalo la kusema: -
- yaliyoandikwa na daily news yametoka kwa wananchi
- na hao wananchi walikuwa wanaongea ukweli wao
- kama kweli walikuwa wamemsikiliza Dr. Slaa
- kama idadi kubwa ya waTanzania wanaubongo kama wa hao jamaa
- Kama mwandishi wa habari imeridhika na alichokifanya (kuripoti pumba na kuziacha hewani. Kwa mwandishi makini, akitoa habari kama hiyo mwishoni atasema hata hivyo... (anaweka ufafanuzi ili kutowapotosha watu).

basi mapambano ya kifikra ni magumu na ushindi upo mbali sana. Huenda tunamatatizo ya ubongo, na ujinga umekuwa mkubwa mno hivyo tunastahili utawala mbovu, wacha tuendelee kuliwa tu.
 
Habari leo, deilenyuzi, tibisii na wachovu wengine kama Nyu habari korporesheni, uhuru na mzalendo ni virusi vya hatari katika jumuiya ya media Tanzania yenye dhamana ya nguzo ya nne ya dola.
Na ni aibu kubwa kwa wahariri wake na waandishi, kwani kwa kukubali kwao kutumika kupotosha Umma wa Watanzania walio wengi kwa vile hawana upeo mkubwa wa kuelewa mambo ili kuwapa mwanya Viongozi na matajiri waendelee kufanya watakavyo NI DHAMBI KUBWA NA USALITI kwa watanzania wenzao.
Usaliti wa aina yeyote (kama ule wa YUDA ISKARIOTE) ni AIBU AIBU AIBUambayo kwa kawaida binadamu asipotubu kwa wahusika ataingia nayo kaburini.
 
Mwl JK Nyerere aliwahi kusema ili nchi iweze kuendelea inahitaji vitu vinne [1]Siasa safi[2]Uongozi bora[3]Ardhi [4]Watu,hata leo nakubaliana kabisa na kauli ya Baba wa taifa.
Tanzania inashindwa kuendelea kwasababu imekosa siasa safi na uongozi bora,watu wapo na ardhi ya kutosha tena yenye rutuba ipo.
Mheshimiwa Slaa ajapinga fedha za EPA kupelekwa kwa wakulima kama magazeti ya serekali yanavyojaribu kuupotosha umma wa watanzania.Mheshimiwa Slaa alipinga rais Jakaya Kikwete kuzipeleka fedha za EPA TIB kwasababu si kazi yake bali ni kazi ya bunge.Kinachoendelea ni siasa chafu za chama cha mapinduzi za kujaribu kumchafua mheshimiwa Slaa.
Siasa chafu zinazalishwa na uongozi mbovu kama huu wa mheshimiwa Kikwete.
Wezi wa fedha za EPA walistahili kushtakiwa kwa makosa mawili makubwa 1.kugushi nyaraka 2 wizi .makosa yote haya mawili ukiyatazama kiundani nia makosa ya jinai lakini mheshimiwa rais anataka kuwaaminisha watanzania kwamba ni makosa ya madai.
Kichekesho kingine ni hayo maandamano,sijui wanaandamanaji walikuwa wanapongeza nini!!!!!!!!!!!!!!!!.
1 Hakuna fisadi hata mmoja aliyefikishwa mahakamani
2 Hakuna anayejua kama kweli fedha za EPA zimerejeshwa
3 Rais amenyakuwa kazi za bunge kwa kugawa fedha za EPA TIB [Kama kweli fedha zipo]
4 Rais kaingilia kazi za mahakama,kahukumu wezi warejeshe fedha.
5 Kitendo cha rais kuendelea kuwabeba wezi kitawapa moyo wezi wengi kuiba

Ndio style yao sasa CCM siku hizi, kumbuka Change na Lowasa walivyoandaa bash kwenye majimbo yao baada ya kashfa zao! Sioni tofauti yoyote na hili la JK. Inatia kinyaa sana kuona watu wasivyoweza kuchambua mambo kwa utashi na mantiki badala yake wanaangalia ushabiki wa vyama! Sasa kati ya hao waliopinga hoja ya Slaa kuna hata mmoja anaweza kuthibitisha kwamba hizo pesa walizoambiwa kweli zipo? Hili ni bao la kisigino mafisadi wanataka kutupiga, hakuna hata senti tano imerudishwa....DAMN, I'M SO SAD!!
 
mtu mwenye kichwa juu ya mabega yake hawezi kukubali upuuzi kama huu unaondelea nchini

christopher mtikila akihutubia chuo kikuu cha dsm 1992, kwenye ukumbi wa nkrumah
 
Nilikuwa na taarifas mapema tu kuwa viongozi wa CCM walikuwa wamepewa jukumu la kuandaa maandamano ya kuunga mkono hotuba ya rais aliyoitoa bungeni.
NIa ya maandamano haya ambayo yanaratibiwa na CCM ofisi ndogo ya Lumumba ni kupunguza kasi ya kushuka kwa umaarufu wa chama na eti kurudisha mshikamano baina ya wanachama.

Iliaminika pia kuwa maandamano haya yatatuliza kwa kiasi kikubwa hoja ya ufisadi na kuchelewesha kama si kuondolea mbali mpango wa wafanyakazi wa kugoma.
Vyombo vya habari vimepewa kazi ya kucover maandamano haya ya CCM kila siku.

Taarifa zilizonifikia mchana wa leo ni kuwa kule Moshi CCM wameagizwa wakusanye wanachama kutoka wilaya zote na kuwakusanya mjini kwani haiwezekani kukusanya wanachama wa CCM mjini Moshi watakaofikia 60. Maandamano ya Moshi sasa yatafanyika siku ya Jumamosi wiki hii.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom