GUSSIE
JF-Expert Member
- Dec 2, 2014
- 3,866
- 11,099
Wanabodi, Wana CCM wa kuja au wavamizi wanaompinga Mama Samia Suluhu hawakutegemea mabadiliko ya ghafla ya kuondoa sera kandamizi.
Mimi ni mwana CCM. Kati ya mwaka 2017 mpaka 2020 Chama kilivamiwa na watu toka upinzani wakisema "Wanaunga juhudi za mwenyekiti wa CCM za kuleta Maendeleo".
Hawa wavamizi ndani ya CCM walimfuata mwenyekiti wa CCM tu bali hawakufuata itikadi na sera. Sasa Mwenyekiti hayupo.
Kundi la pili lilikuwa CCM maslahi au watafuta vyeo hawa kazi yao ilikuwa kusifu na kumpamba mwenyekiti wa CCM kwa kauli za "Aongezewe muda amefanya mambo makubwa toka tupate uhuru"
Hawa watu walijiona hii nchi ni ya kwao na hakuna mtu zaidi ya wao, Walitishia watu kwa mgongo wa mwenyekiti,
Hawa wavamizi waliamua kujitoa ufahamu na kupanga safu zao za uongozi ndani ya chama wakitegemea ataongezewa muda wa kutawala Mwenyekiti.
Unakumbuka kauli kama"Unaijua viete wewe?. Kama hamtaki kufuata sera zaCCM hameni nchi.
Makundi haya ndani ya CCM yameachwa yatima na wapweke sana, Sasa wamekaa kupinga sera za Mama Samia
Kila dakika wana CCM wavamizi wanahubiri Mama awabane wafanyabiashara, Mama aendeleze sera za chuki na kuligawa Taifa. Kitu ambacho kwa dini ya Mama Samia sio haki na hairuhusiwi.
Mimi ni mwana CCM. Kati ya mwaka 2017 mpaka 2020 Chama kilivamiwa na watu toka upinzani wakisema "Wanaunga juhudi za mwenyekiti wa CCM za kuleta Maendeleo".
Hawa wavamizi ndani ya CCM walimfuata mwenyekiti wa CCM tu bali hawakufuata itikadi na sera. Sasa Mwenyekiti hayupo.
Kundi la pili lilikuwa CCM maslahi au watafuta vyeo hawa kazi yao ilikuwa kusifu na kumpamba mwenyekiti wa CCM kwa kauli za "Aongezewe muda amefanya mambo makubwa toka tupate uhuru"
Hawa watu walijiona hii nchi ni ya kwao na hakuna mtu zaidi ya wao, Walitishia watu kwa mgongo wa mwenyekiti,
Hawa wavamizi waliamua kujitoa ufahamu na kupanga safu zao za uongozi ndani ya chama wakitegemea ataongezewa muda wa kutawala Mwenyekiti.
Unakumbuka kauli kama"Unaijua viete wewe?. Kama hamtaki kufuata sera zaCCM hameni nchi.
Makundi haya ndani ya CCM yameachwa yatima na wapweke sana, Sasa wamekaa kupinga sera za Mama Samia
Kila dakika wana CCM wavamizi wanahubiri Mama awabane wafanyabiashara, Mama aendeleze sera za chuki na kuligawa Taifa. Kitu ambacho kwa dini ya Mama Samia sio haki na hairuhusiwi.