Wana CCM tushikamane kipindi hiki KIGUMU, yatapita tu!

Chunguza ama9 mchumguze asiye ipemda ccm utangundua kitu.kama ni mzee ujue kafukuzwa kz kama ni kijana ujue ni mpiga debe na kama ni mtu wa makamo basi jua huyo ni mvivu balaaa cc ni jembe na nyundo hiyo ni falsafa yao wavivu sasa wanavyo ikokotoa eti nyundo nikuponda kichwa hadi ufe najembe kazi yake ni kuzika wavivu wOte.
 
bila shaka kabisa na hawana lolote usione wazee wetu wa ccm wametulia ukadhaniwanaogopa ila wanasuka mipango ccm oyeeee

tumekwishaaaaa ccm .hili liwe fundisho kwa vyama vinavyopenda kukatakata watu kwa kiburi.ukawa vivaaaa chukueni nchiiiiiii
 
Nawaomba kwa dhati wanachama wa CCM tushikamane kwa nguvu zote kipindi hiki kuelekea uchaguzi yatasemwa mengi sana kuhusu chama chetu na viongozi wetu tusiwape nafasi wabaya wetu wanaopanga kutuangamiza kwa maneno ya UONGO. Wale MAFISADI waacheni waende kwenye vyama dhaifu (vyama vya UKABILA na UDINI). CCM ndo chama dola na itaendelea kushika dola milele na milele

Kwa style hii kweli tutaupata mshikamano?

Naishauri CCM isome alama za nyakati. Katika matokeo ya uchaguzi wa ubunge wa viti maalum kupitia VIJANA yaani UVCCM inaonesha kuwa watoto wa wananchi wa kawaida hawana nafasi ya kupata fursa za uongozi kupitia UVCCM.

Kati ya majina 6 ya walioshinda nafasi hizo wote ni watoto wa viongozi wa CCM, Je hii ni coincidence kwamba watoto wa viongozi pekee ndio wenye uwezo?

Mimi nilikuwa nafuatilia kwa karibu mchakato mzima wa uchaguzi huu na ninachoweza kusema ni kwamba CCM imelewa na madaraka na wakati sasa umebadilika, CCM isiendelee kuendesha mambo yake kwa mazoea sasa ni mwaka 2015 mambo yanabadilika wananchi sasa wana upeo kulinganisha na zamani.

UKAWA inawekeza katika vijana ambao hawana ajira na hawana fursa za kufanikiwa ndani ya CCM kwa sababu CCM inapendelea watoto wa vigogo.

Kuna vijana wengi ambao waliingia katika mchakato huu wa kupitia UVCCM na wana uwezo wa uongozi lakini hawawezi kufanikiwa ndani ya chama kwa sababu ya kuna wengine wanabebwa kutokana na majina ya wazazi wao. Hebu angalia majina ya walioshinda uchaguzi huo na uhusiano na viongozi wa CCM.

Washindi wa ubunge viti maalumu UVCCM - Bara, 2015.

1.HALIMA BULEMBO - Mtoto wa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM (Taifa) Bw. Abdallah Bulembo.

2.ZAINAB KATIMBA - Mtoto wa Kada wa CCM, Bi Maimuna Tarishi pia amewahi kuwa Katibu Mkuu wa Wizara mbalimbali nchini.

3.JULIANA MASABURI - Mtoto wa Kada maarufu wa CCM na Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Dkt. Didas Masaburi

4.MARIUM DITOPILE - Mtoto wa Merehemu Ditopile Mzuzuri aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa CCM Wilaya za Sengerema, Mwanza, Tabora na Mbunge wa Ilala, DSM.

5.MARIA KANGOLE - Mtoto wa Mwenyekiti wa CCM Mkoani Arusha Bw. Onesmo Kangole.

6.SOPHIA KIZIGO - Mtoto wa Naibu Katibu Mkuu wa UVCCM (Taifa) Bw. Mfaume Kizigo.

7.JACQUELINE MZINDAKAYA - Mtoto wa Kada Maarufu wa CCM Dkt. Chrisant Mzindakaya ambaye aliwahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Kwela na Mkuu wa Wilaya ya Busega, Simiyu.

CCM ijiulize, Je watoto wa viongozi wa CCM wanawakilsha asilimia ngapi ya vijana wa nchi hii?.

Cha ajabu watoto hawa walianza kuzunguka mikoani na kuanza kampeni kwa wajumbe wa ngazi ya Taifa kabla ya mchujo wa ngazi mkoa haujafanyika.

Je, walipata wapi uhakika kwamba watapita ngazi za mikoa mpaka wakaanza kutoa rushwa ngazi ya Taifa bila ya kuwa na uhakika wa kubebwa?
 
Wanaondoka CCM wameondoka kwa uroho wa madaraka baada ya kutemwa na vikao halali vya chama wanahaha na kukimbilia chama dhaifu CHADEMA huu ni uroho wa madaraka tofauti na malengo na kanuni za CCM
 
Umoja ni nguvu wana ccm tusitetereke na mafisadi. MPINZANI WA KWELI NI MHE. DOVUTWA wengine ni mbwembwe tu hawana sera
 
Tunashikamana lakini mambo hayaendi huku mtaani aisee kila mtu ni UKAWA UKAWA mpaka inatutia hofu sisi wana CCM je tutashinda kweli mwaka huu?
 
Wana CCM tusijione wanyonge kwa ule umati wa pale Jangwani siku watani wetu wa jadi wanazindua kampeni zile zote ni hila za mafisadi katika kututisha. Sisi tumejipanga na tuna timu makini ikiwemo WASANII MAARUFU hasa Dada Wema na Mcekeshaji Steve Nyerere wao watapita kila nyumba kuhakikisha tunapata kura za kutosha. Ondoeni hofu ushindi kwetu ni lazima. Mgombea wetu anauzika sana. Asanteni.
 
Poleni ndugu zetu mmekuwa wavumilivu sana.ni kuwa na roho au ubongo wa kichaa ndio ubaki ugambani.mazishi ni 25/10/2015.
 
Nawaomba kwa dhati wanachama wa CCM tushikamane kwa nguvu zote kipindi hiki kuelekea uchaguzi yatasemwa mengi sana kuhusu chama chetu na viongozi wetu tusiwape nafasi wabaya wetu wanaopanga kutuangamiza kwa maneno ya UONGO. Wale MAFISADI waacheni waende kwenye vyama dhaifu (vyama vya UKABILA na UDINI). CCM ndo chama dola na itaendelea kushika dola milele na milele

Kila jambo lina mwanzo na mwisho wake kwa mtazamo wa sasa ccm imepoteza mvuto na watu hawana iman nayo tena,mabadiliko ndio mda wake kwa sasa hayayuiliki tukubari na tuyaunge mkono
 
Wana CCM tusijione wanyonge kwa ule umati wa pale Jangwani siku watani wetu wa jadi wanazindua kampeni zile zote ni hila za mafisadi katika kututisha. Sisi tumejipanga na tuna timu makini ikiwemo WASANII MAARUFU hasa Dada Wema na Mcekeshaji Steve Nyerere wao watapita kila nyumba kuhakikisha tunapata kura za kutosha. Ondoeni hofu ushindi kwetu ni lazima. Mgombea wetu anauzika sana. Asanteni.

Anauzika bei gani?Maana huku tumemkata,hivyo hata bure tumemwambia hatumtaki.
 
Wanaondoka CCM wameondoka kwa uroho wa madaraka baada ya kutemwa na vikao halali vya chama wanahaha na kukimbilia chama dhaifu CHADEMA huu ni uroho wa madaraka tofauti na malengo na kanuni za CCM

Kama CCM hakuna MROHO wa MADARAKA kwanini mnapigana hovyo kwenye kutafuta wagombea?Ili tujue nyie siyo waroho wa MADARAKA kwanini mmemsimamisha Magufuli?Kwanini msiiache hiyo nafasi wazi upinznai wakaichukua?

Kama CCM haina UROHO wa MADARAKA kwanini mnawanyima UKAWA nafasi za kufanya kampeni???

Kama hamna UROHO wa MADARAKA kwanini mtumie pesa nyingi kwenye uchaguzi.?????

Hakuna chama cha siasa kisichotaka MADARAKA,poleni sana kwa hoja mufilisi.
 
Nawaomba kwa dhati wanachama wa CCM tushikamane kwa nguvu zote kipindi hiki kuelekea uchaguzi yatasemwa mengi sana kuhusu chama chetu na viongozi wetu tusiwape nafasi wabaya wetu wanaopanga kutuangamiza kwa maneno ya UONGO. Wale MAFISADI waacheni waende kwenye vyama dhaifu (vyama vya UKABILA na UDINI). CCM ndo chama dola na itaendelea kushika dola milele na milele

Hayapiti mkiwa salama mpaka mfarakane...! Ata firauni alikuwa jeuri hivyohivyo akawambia wanajeshi wake washikamane watavuka mwisho wake waliangamia kwenye red sea.
 
Kwa style hii kweli tutaupata mshikamano?

Naishauri CCM isome alama za nyakati. Katika matokeo ya uchaguzi wa ubunge wa viti maalum kupitia VIJANA yaani UVCCM inaonesha kuwa watoto wa wananchi wa kawaida hawana nafasi ya kupata fursa za uongozi kupitia UVCCM.

Kati ya majina 6 ya walioshinda nafasi hizo wote ni watoto wa viongozi wa CCM, Je hii ni coincidence kwamba watoto wa viongozi pekee ndio wenye uwezo?

Mimi nilikuwa nafuatilia kwa karibu mchakato mzima wa uchaguzi huu na ninachoweza kusema ni kwamba CCM imelewa na madaraka na wakati sasa umebadilika, CCM isiendelee kuendesha mambo yake kwa mazoea sasa ni mwaka 2015 mambo yanabadilika wananchi sasa wana upeo kulinganisha na zamani.

UKAWA inawekeza katika vijana ambao hawana ajira na hawana fursa za kufanikiwa ndani ya CCM kwa sababu CCM inapendelea watoto wa vigogo.

Kuna vijana wengi ambao waliingia katika mchakato huu wa kupitia UVCCM na wana uwezo wa uongozi lakini hawawezi kufanikiwa ndani ya chama kwa sababu ya kuna wengine wanabebwa kutokana na majina ya wazazi wao. Hebu angalia majina ya walioshinda uchaguzi huo na uhusiano na viongozi wa CCM.

Washindi wa ubunge viti maalumu UVCCM - Bara, 2015.

1.HALIMA BULEMBO - Mtoto wa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM (Taifa) Bw. Abdallah Bulembo.

2.ZAINAB KATIMBA - Mtoto wa Kada wa CCM, Bi Maimuna Tarishi pia amewahi kuwa Katibu Mkuu wa Wizara mbalimbali nchini.

3.JULIANA MASABURI - Mtoto wa Kada maarufu wa CCM na Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Dkt. Didas Masaburi

4.MARIUM DITOPILE - Mtoto wa Merehemu Ditopile Mzuzuri aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa CCM Wilaya za Sengerema, Mwanza, Tabora na Mbunge wa Ilala, DSM.

5.MARIA KANGOLE - Mtoto wa Mwenyekiti wa CCM Mkoani Arusha Bw. Onesmo Kangole.

6.SOPHIA KIZIGO - Mtoto wa Naibu Katibu Mkuu wa UVCCM (Taifa) Bw. Mfaume Kizigo.

7.JACQUELINE MZINDAKAYA - Mtoto wa Kada Maarufu wa CCM Dkt. Chrisant Mzindakaya ambaye aliwahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Kwela na Mkuu wa Wilaya ya Busega, Simiyu.

CCM ijiulize, Je watoto wa viongozi wa CCM wanawakilsha asilimia ngapi ya vijana wa nchi hii?.

Cha ajabu watoto hawa walianza kuzunguka mikoani na kuanza kampeni kwa wajumbe wa ngazi ya Taifa kabla ya mchujo wa ngazi mkoa haujafanyika.

Je, walipata wapi uhakika kwamba watapita ngazi za mikoa mpaka wakaanza kutoa rushwa ngazi ya Taifa bila ya kuwa na uhakika wa kubebwa?

Baada ya muda mfupi chama hicho kitakuwa na wanachama wafuatao:

Watoto wa wakuu wilaya na familia zao
watoto wa wakuu wa mikoa na familia zao
watoto wa mawaziri na familia zao
watoto wa manaibu waziri na familia zao
watoto wa Makatibu wakuu na familia zao.

Yaani list ni ndefu,maana watoto wa Kayumba,mtoka jasho,kabwela,lofa hawatakuwepo.Maana hiyo list yako inasema kila kitu.Nashangaa mtu anakipigia debe chama cha mapinduzi
 
Nimewakuta ccm mahali wamevaa mashati yao yani wamechoka surazao zimekata tamaakabisa nitaweka picha zao hapa mzione.

Wanaonyesha kabisa wanatamani mabadiliko lakini wanakauogaflani hivi, ila kupitia Brody language zao naweza hatakubeti kwamba watampa kura Lowasa.

Make my word.
 
Back
Top Bottom