Wana-Apollo wateka gari lenye mchanga wa Tanzanite

Mtu wa Pwani

JF-Expert Member
Dec 26, 2006
4,184
671
Wana-apolo wateka gari lenye mchanga wa tanzanite
Na Neil Bwindiki, Simanjiro


KUNDI la Wana-Apolo 200 walioko katika eneo la Mgodi wa Madini ya Tanzanite One wa Mererani, wilayani Simanjiro, mkoani Manyara, wameliteka lori dogo lililokuwa likisafirisha mchanga wenye madini hayo mali ya Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) mkoani Arusha na kupora viroba vilivyosheheni mchanga huo.


Kamanda wa Polisi mkoani Manyara, Luther Mbutu, amethibitisha tukio hilo lililotokea juzi saa 11 jioni katika eneo la kijiji cha Naisinyai kilichopo katika barabara kuu inayotoka eneo la mgodi huo kuelekea uwanja wa ndege wa Kimatifa wa Kilimanjaro (KIA).


Alisema, lori hilo lenye mali ya Leonard Kavishe, mkazi wa Kaloleni, mkoani Arusha lilitumika kubeba mchanga huo kutoka kwa mwekezaji wa kampuni inayojishughulisha na uchimbaji wa madini hayo baada ya kuomba ili aweze kupata fedha za kuendesha mradi wao.


Kamanda Mbutu alisema baada ya kutoka katika eneo hilo la mgodini, lilipofika katika eneo hilo, dereva wa gari hilo, Davis Geoffrey (27) mkazi wa Arusha, aliwakuta baadhi ya wana-apolo wakiwa wamelala barabarani.


Alisema aliposimama, alivamiwa na kujeruhiwa mkononi na gari lake kushambuliwa kwa mawe kupora viroba hivyo ambavyo thamani yake bado haijajulikana.


Kamanda Mbutu alisema, baada ya kupora, wana-apolo hao walitoweka kusikojulikana na kuliacha gari hilo barabarani na kwamba, dereva huyo aliyejeruhiwa, alisaidiwa muda mchache baada ya askari polisi kufika eneo la tukio.


Alisema baada ya kutekwa, lori hilo liliharibiwa na kusababisha hasara ya zaidi ya Sh800,000 na limehifadhiwa katika kituo kidogo cha polisi kilichopo Mererani.


Kamanda Mbutu alisema polisi imefuatilia kujua mchanga huo ni mali ya nani baada ya kuwapo kwa uvumi kuwa ni mali ya Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka na kubaini kuwa ni mali ya UV-CCM wilayani humo kutokana na kibali kilichotolewa na kuidhinishwa na Katibu wa Vijana Mkoa wa Arusha, Mfaume Kizigo.


Naye Ole Sendeka akizungumza kwa njia ya simu kutoka jijini Dar es Salaam, alithibitisha tukio hilo na kukanusha uvumi kuwa mchanga huo kuwa ni mali yake na kusema kuwa baadhi ya wanasiasa wanatumia nafasi hiyo kulichafua jina lake.


mwananchi


kazi hiyo sio ndogo hapa panahitaji utfiti wa kutosha haya mambo yanaendaje?
 
swali kubwa hapa kwangu ni kuwa kunani hata kampuni hiyo iwape UVCCM mchanga wa Tanzanite? Siku UVCCM wanafanya biashara ya madini? Leaves a lot to be desired!
 
Hii inadhihirisha kuwa "WADANGANYIKA" wamechoka na blabla za maisha bora kwa kila mtanzania huku "Watu wanachukua Chao Mapema" Watu wakiwasema viongozi, jibu linakuwa leteni ushahidi. Sasa nao wameamua kutumia staili hiyo kwa sababu "Mnyonge Siku zote hana cha kupoteza"

Tanzania inaendelea kubadilika siku hadi siku; kuanzia kumrushia mawe Mkuu wa Wilaya , Zomea zomea na sasa kuchukua kile wanachokikosa kwa nguvu. Hii ni dalili mbaya kwa future ya nchi. Tusiendelee kujidanganya kuwa tuna AMANI wakati tumekalia BOMU kubwa ambalo ni suala la wakati tu. JK salam hizo zinatosha kuwafanya muangalie nyuma kabla hamjaiangamiza nchi.
 
Jamani hivi ni utaratibu gani unaotumika ili kuweza kupata huo mchanga wa Tanzanite/dhahabu? Nauliza ili Watanzania wengine wazijue taratibu hizo na wao waombe kama ni kupewa au kununua mchanga huo. Juzi juzi tulisikia baadhi ya mawaziri wana migodi yao, sasa tunasikia kwamba UVCCM walikuwa na machanga wa Tanzanet wakati huo huo Watanzania tulio wengi hatujui ni taratibu zipi zinazotumika kumiliki mgodi au mchanga.
 
Hii inadhihirisha kuwa "WADANGANYIKA" wamechoka na blabla za maisha bora kwa kila mtanzania huku "Watu wanachukua Chao Mapema" Watu wakiwasema viongozi, jibu linakuwa leteni ushahidi. Sasa nao wameamua kutumia staili hiyo kwa sababu "Mnyonge Siku zote hana cha kupoteza"

Tanzania inaendelea kubadilika siku hadi siku; kuanzia kumrushia mawe Mkuu wa Wilaya , Zomea zomea na sasa kuchukua kile wanachokikosa kwa nguvu. Hii ni dalili mbaya kwa future ya nchi. Tusiendelee kujidanganya kuwa tuna AMANI wakati tumekalia BOMU kubwa ambalo ni suala la wakati tu. JK salam hizo zinatosha kuwafanya muangalie nyuma kabla hamjaiangamiza nchi.

Magufuli kaja kusafusha uchafu.
 
swali kubwa hapa kwangu ni kuwa kunani hata kampuni hiyo iwape UVCCM mchanga wa Tanzanite? Siku UVCCM wanafanya biashara ya madini? Leaves a lot to be desired!
Huyu kabla hapa njaa hajaivalia koti ila hongeta mkuu unatumikia tumbo lako sasa hivi
 
Hii inadhihirisha kuwa "WADANGANYIKA" wamechoka na blabla za maisha bora kwa kila mtanzania huku "Watu wanachukua Chao Mapema" Watu wakiwasema viongozi, jibu linakuwa leteni ushahidi. Sasa nao wameamua kutumia staili hiyo kwa sababu "Mnyonge Siku zote hana cha kupoteza"

Tanzania inaendelea kubadilika siku hadi siku; kuanzia kumrushia mawe Mkuu wa Wilaya , Zomea zomea na sasa kuchukua kile wanachokikosa kwa nguvu. Hii ni dalili mbaya kwa future ya nchi. Tusiendelee kujidanganya kuwa tuna AMANI wakati tumekalia BOMU kubwa ambalo ni suala la wakati tu. JK salam hizo zinatosha kuwafanya muangalie nyuma kabla hamjaiangamiza nchi.
Maana yake nini kutuletea post hii?
 
Mh. Kitila Mkumbo hapa naona Kikubwa ni "uvamizi"
Inawezekana wana apollo wamekuwa inspired na serikali yao pale bandarini.
Just thinking big
=========update========
Tarehe ya kubandikwa thread hii inanielekeza kuiodoa post hii kwa maandishi.
 
Back
Top Bottom