Mtu wa Pwani
JF-Expert Member
- Dec 26, 2006
- 4,191
- 677
Wana-apolo wateka gari lenye mchanga wa tanzanite
Na Neil Bwindiki, Simanjiro
KUNDI la Wana-Apolo 200 walioko katika eneo la Mgodi wa Madini ya Tanzanite One wa Mererani, wilayani Simanjiro, mkoani Manyara, wameliteka lori dogo lililokuwa likisafirisha mchanga wenye madini hayo mali ya Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) mkoani Arusha na kupora viroba vilivyosheheni mchanga huo.
Kamanda wa Polisi mkoani Manyara, Luther Mbutu, amethibitisha tukio hilo lililotokea juzi saa 11 jioni katika eneo la kijiji cha Naisinyai kilichopo katika barabara kuu inayotoka eneo la mgodi huo kuelekea uwanja wa ndege wa Kimatifa wa Kilimanjaro (KIA).
Alisema, lori hilo lenye mali ya Leonard Kavishe, mkazi wa Kaloleni, mkoani Arusha lilitumika kubeba mchanga huo kutoka kwa mwekezaji wa kampuni inayojishughulisha na uchimbaji wa madini hayo baada ya kuomba ili aweze kupata fedha za kuendesha mradi wao.
Kamanda Mbutu alisema baada ya kutoka katika eneo hilo la mgodini, lilipofika katika eneo hilo, dereva wa gari hilo, Davis Geoffrey (27) mkazi wa Arusha, aliwakuta baadhi ya wana-apolo wakiwa wamelala barabarani.
Alisema aliposimama, alivamiwa na kujeruhiwa mkononi na gari lake kushambuliwa kwa mawe kupora viroba hivyo ambavyo thamani yake bado haijajulikana.
Kamanda Mbutu alisema, baada ya kupora, wana-apolo hao walitoweka kusikojulikana na kuliacha gari hilo barabarani na kwamba, dereva huyo aliyejeruhiwa, alisaidiwa muda mchache baada ya askari polisi kufika eneo la tukio.
Alisema baada ya kutekwa, lori hilo liliharibiwa na kusababisha hasara ya zaidi ya Sh800,000 na limehifadhiwa katika kituo kidogo cha polisi kilichopo Mererani.
Kamanda Mbutu alisema polisi imefuatilia kujua mchanga huo ni mali ya nani baada ya kuwapo kwa uvumi kuwa ni mali ya Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka na kubaini kuwa ni mali ya UV-CCM wilayani humo kutokana na kibali kilichotolewa na kuidhinishwa na Katibu wa Vijana Mkoa wa Arusha, Mfaume Kizigo.
Naye Ole Sendeka akizungumza kwa njia ya simu kutoka jijini Dar es Salaam, alithibitisha tukio hilo na kukanusha uvumi kuwa mchanga huo kuwa ni mali yake na kusema kuwa baadhi ya wanasiasa wanatumia nafasi hiyo kulichafua jina lake.
mwananchi
kazi hiyo sio ndogo hapa panahitaji utfiti wa kutosha haya mambo yanaendaje?
Na Neil Bwindiki, Simanjiro
KUNDI la Wana-Apolo 200 walioko katika eneo la Mgodi wa Madini ya Tanzanite One wa Mererani, wilayani Simanjiro, mkoani Manyara, wameliteka lori dogo lililokuwa likisafirisha mchanga wenye madini hayo mali ya Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) mkoani Arusha na kupora viroba vilivyosheheni mchanga huo.
Kamanda wa Polisi mkoani Manyara, Luther Mbutu, amethibitisha tukio hilo lililotokea juzi saa 11 jioni katika eneo la kijiji cha Naisinyai kilichopo katika barabara kuu inayotoka eneo la mgodi huo kuelekea uwanja wa ndege wa Kimatifa wa Kilimanjaro (KIA).
Alisema, lori hilo lenye mali ya Leonard Kavishe, mkazi wa Kaloleni, mkoani Arusha lilitumika kubeba mchanga huo kutoka kwa mwekezaji wa kampuni inayojishughulisha na uchimbaji wa madini hayo baada ya kuomba ili aweze kupata fedha za kuendesha mradi wao.
Kamanda Mbutu alisema baada ya kutoka katika eneo hilo la mgodini, lilipofika katika eneo hilo, dereva wa gari hilo, Davis Geoffrey (27) mkazi wa Arusha, aliwakuta baadhi ya wana-apolo wakiwa wamelala barabarani.
Alisema aliposimama, alivamiwa na kujeruhiwa mkononi na gari lake kushambuliwa kwa mawe kupora viroba hivyo ambavyo thamani yake bado haijajulikana.
Kamanda Mbutu alisema, baada ya kupora, wana-apolo hao walitoweka kusikojulikana na kuliacha gari hilo barabarani na kwamba, dereva huyo aliyejeruhiwa, alisaidiwa muda mchache baada ya askari polisi kufika eneo la tukio.
Alisema baada ya kutekwa, lori hilo liliharibiwa na kusababisha hasara ya zaidi ya Sh800,000 na limehifadhiwa katika kituo kidogo cha polisi kilichopo Mererani.
Kamanda Mbutu alisema polisi imefuatilia kujua mchanga huo ni mali ya nani baada ya kuwapo kwa uvumi kuwa ni mali ya Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka na kubaini kuwa ni mali ya UV-CCM wilayani humo kutokana na kibali kilichotolewa na kuidhinishwa na Katibu wa Vijana Mkoa wa Arusha, Mfaume Kizigo.
Naye Ole Sendeka akizungumza kwa njia ya simu kutoka jijini Dar es Salaam, alithibitisha tukio hilo na kukanusha uvumi kuwa mchanga huo kuwa ni mali yake na kusema kuwa baadhi ya wanasiasa wanatumia nafasi hiyo kulichafua jina lake.
mwananchi
kazi hiyo sio ndogo hapa panahitaji utfiti wa kutosha haya mambo yanaendaje?