Wamo Au Hawamo?

Yona F. Maro

R I P
Nov 2, 2006
4,202
218
Fukuto la fukuta, moshi wafoka, mapovu yanamwagika, CCM imefika njia panda! Ama isuke au inyoe!

Hili vurugu la Richmond, likizingirwa na BOT EPA, BOT CIS, BOT Minara, Rada, Kiwira, Buzwagi na moto kutoka Upinzani, unafanya mambo kadhaa tujiandee kutokea.

1. Wabunge ambao si mtandao, wenye uchungu wa kweli wa CCM, kuendelea kusulubisha viongozi wao na Serikali yao iwe wazi. Hawa wabunge, mwokozi wao na nguzo yao ni Wastaafu Malecela, Kawawa, Mwinyi, Salim na Msuya. Huku wako hawa walioshupalia RDC;-Mwakyembe, Kilango-Malecela, Seleli, Kimaro, n.k.

2. Team Mkapa; huku ni wale wajanja wa Che-Nkapa ambao bado wanatibu majeruhi ya mchakato wa kugombea Urais 2005 na kunyang'anywa tonge la Hatamu za Chama. Hapa kuna Mang'ula, Ngwilizi, Kigoda, Kinana, Warioba na Ruhinda. Katika kundi hili, pia wapo wale waliotajirika na mradi wa Ujasirimali Ikulu; Yona, Mramba, Mgonja, Mkono n.k.

3. Mtandao; Kundi hili lina majeruhi wengi kutokana na kuvunjwa kwa baraza la mwazirina mwegemeo wa kashfa za ufisadi kuwa kwenye shingo zao. Kundi hili, limegawanyika katika sura mbili;

1. Team Kikwete ambayo wamebakia Makamba, Chiligati, Membe, Migiro, Karume

2. Team Rostwassa(Rostam/Lowassa); Karamagi, Msabaha, Nchimbi, Apson, Meghji, Kamala, Masha Diallo, Chenge,

4. Wasiofungamana lakini wana nguvu na ni tishio; Pinda, Mwandosya, Sumaye, Balali, Salmin, Magufuli, Msekwa na Sitta.

Serikali mpya na baraza lake la mawaziri bado ni ya Kikwete Lowasa na Rostam.

Masha-Mambo ya ndani, bila Lowasa Bw. Mdogo Masha asingekuwa hapo alipo, ni lowasa aliyemshika mkono na kumwingiza kwenye siasa, kwani yeye Masha na Business partner wake Magai walikuwa private lawyers wa mamvi, na hata Magai aliwahi kupatiwa ujumbe wa bodi ndani ya city water wakati huo Lowasa ni waziri wa maji. Je unategemea Masha atasahau alikotoka kama JK asivyomtupa Hussein Mwinyi???? Hao polisi, Manumba na Magereza vyote viko chini ya Masha. Sasa je, nani atamkoma Nyani giradi????

Ngeleja-Nishati na Madini- Huyu alikuwa mwanasheria mkuu wa Vodacom Tanzania LTD ambako Rostam na lowasa wana hisa japo mamvi ni silent share holder. Ni Rostam aliyemshika mkono Ngeleja akagombee Sengerema na kumpatia fungu la kutosha ashinde. Na ndio maana ameachwa madini ili aendelee kulinda migodi ya Rostam. Hivyo tusitarajie mabadiliko makubwa.

Mkullo-fedha- Huyu akiwa mkurugenzi wa NPF sasa NSSF alichota mapesa kibao kumuunga mkono JK mwaka 1995, hivyo ni senior mwanamtandao. Na ndio maana Mkapa alipoingia madarakani akamtema NSSF.

Chenge- Miundombinu, JK hana namna, hampendi Chenge lakini anakuwa forced na Lowasa na Rostam. Mikataba yote kuanzia IPTL n.k imesainiwa wakati wa Chenge na yeye anaelewa nani ni nani katika hayo makampuni yanayozidi kuutafuna utajri wa taifa hili na kutuacha watanzania tukilalia chips kavu. Eti JK atamtosa Chenge! THUBUTU! Atasema kila kitu ! Na ndio maana wakamuwahi Salome mbatia wakamuua ili asiendelee kutoa siri kwa wapinzani kuhusiana na pesa za BOT, kwani yeye ndo alikuwa Mweka hazina mkuu wa chama wakati wa uchaguzi

Kutokana na kuwepo makundi haya makubwa na utata unaotambaa angani hasa baada ya Lowassa kuangushwa na minong'ono kuwa naye Lowassa ana ushahidi wa kujikosha, linalobakia kwetu watazamaji ni kupima upepo na kuomba dua wapigane na wagawanyike ili tujue nani ni kwa manufaa ya Taifa na nani ni mnyonyaji.

CCM si salama, na hata kama wakitoka nje ya ukumbi wakiwa wamekumbatiana, tusiwaamini
 
Ama kweli, ukistaajabu ya Mussa, utayaona ya Firauni! Kama unadhani vigogo wa EPA ni mafisadi peke yao, basi ulikuwa hujamfahamu Spika wa Bunge SAMUEL JOHN TEGEZA SITTA ! Ukimsikiliza anapoongea unaweza kuamini kwamba kiongozi huyo wa Bunge ni msafi kutokana na umahiri wake wa kujivalisha sifa kemkem – Mr Misifa. Unakumbuka hivi karibuni alivyomtukana Naibu Spika eti hawezi kusimamia mambo nyeti mpaka awepo yeye mwenye Bunge? ! Kisa nini? Kupenda sifa na kumdhalilisha mwenzake mbele ya umma, halafu bado anaendelea kuliita Bunge eti ni chombo cha kidemokrasia!

Tumebaini kwamba Sitta amekuwa akijimiminia sifa nyingi ili kulinda ufisadi anaoufanya usigundulike katika jamii yetu. Ngoja nikupe tone tu la madhambi yake kwa umma ili uone ni hatua gani utachukua, na ili na yeye ajipime kwa nafasi yake. Angalia uchafu huu:-

- Anatumia vibaya fedha za umma. Amekuwa akitumia msaidizi wake kuchota mapesa kwa kisingizio kuwa ni masurufu ya safari za ndani na nje ya nchi. Kila safari ya siku moja ndani ya nchi huchukua shilingi Milioni tano (5,000,000/=), na kila safari ya siku moja nje ya nchi huchukua shilingi Milioni Kumi na Tano (15,000,0000/=). Ameshindwa kufanya marejesho ya masurufu (imprest) hayo, licha ya kupeleka risiti kadhaa za kughushi/za uongo kwa Mhasibu Mkuu wa Ofisi ya Bunge. Mpaka sasa anadaiwa jumla ya shilingi Milioni sitini (60,000,000/=) za masurufu.

- SITTA hupeleka risiti za uongo kwa Mhasibu Mkuu, zikionesha madai kutoka Oysterbay Pharmacy ya Shilingi Milioni Mbili ( 2,000,000/= ) aliyotumia kwa tiba kila wiki.

- Amekuwa akilazimisha hawara yake wa Hospitali ya Aga Khan naye alipwe posho kama wabunge anapokwenda naye Dodoma. Kwa mfano, hawara huyo alilipwa 'per diem' kuanzia tarehe 13/12/2007 hadi tarehe 31/01/2008 ( Siku 50). Huo ni Ufisadi mkubwa!

- Anaye kimada wake mwingine anayekwenda kwa jina la ASIA ambaye anaishi nyumba Na. 111 karibu na Mahakama ya Ardhi Upanga na amezaa naye. Huko mtaani kwao kimada huyo hujiita mama SITTA, na ni dada yake aliyekuwa Mwenyekiti Mtendaji wa iliyokuwa Tume ya Kurekebisha Mashirika ya Umma (PSRC). Mwanamke huyo muda wote hutumia gari la Ofisi ya Bunge STK 232 Toyota RAV 4.

- Pia anaye kimada mwingine (jina limehifadhiwa) ambaye anaishi kinondoni ( Livingstone), mtaa wa Honolulu katika nyumba ya kupanga inayomilikiwa na dada yake Kawawa. Nyumba hiyo inatazamana na Nyumba Na. KH.MK/No. 337 katika mtaa huo huo. Kimada huyo hutumia gari ya kiofisi ya Spika mwenyewe STK 3002.

- Vimada wote hao hupata huduma za maji na umeme kwa gharama za Ofisi ya Bunge. Kuna kipindi mke halali wa Spika, aliwahi kulalamikia hali hiyo. Kuna siku maji yalikatika nyumbani, mke wa Spika akaomba apelekewe ' bowser' la maji na Ofisi ya Bunge. Ohooo! Watekelezaji wakapeleka maji kimakosa kwa kimada. Mama Sitta akashtukia dili.

- Kuna taarifa kwamba mnamo Mwezi Oktoba 2007, Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) iligundua mapungufu makubwa katika matumizi ya fedha yaliyofanywa na Spika SITTA. nimedokezwa kuwa Spika aliwanyamazisha wajumbe wa kamati hiyo, ambapo aliwatishia kutowapatia posho na safari za nje kama wangeyafumua mapungufu yake hadharani! Hapo inaonesha kuwa wajumbe hao walipewa rushwa!!

- Kama JK anataka viongozi wa kisiasa na wa serikali watenganishe biashara na uongozi wa ku – 'sacrifice' kimojawapo, hilo litakuwa gumu kwa sababu Sitta alipokuwa Mwenyekiti Mtendaji wa Kituo cha cha Uwekezaji nchini (TIC) alitumia nafasi hiyo kuingia ubia na wafanyabiashara wengi wa Kigeni. Je, Wizara ya Maliasili na Utalii inatambua kuwa Spika ana hisa kwenye kampuni moja ya Kichina inayosafirisha nagogo licha ya marufuku yaliyowekwa?!

- Nililokupa hapo ni tone tu.
 
The leadership system we have in Tanzania is "USHOGALISM SYSTEM"kama si shoga wa JK madaraka utakua unayasikia redioni hata kama unazo sifa kibao.
 
Fukuto la fukuta, moshi wafoka, mapovu yanamwagika, CCM imefika njia panda! Ama isuke au inyoe!

Hili vurugu la Richmond, likizingirwa na BOT EPA, BOT CIS, BOT Minara, Rada, Kiwira, Buzwagi na moto kutoka Upinzani, unafanya mambo kadhaa tujiandee kutokea.

1. Wabunge ambao si mtandao, wenye uchungu wa kweli wa CCM, kuendelea kusulubisha viongozi wao na Serikali yao iwe wazi. Hawa wabunge, mwokozi wao na nguzo yao ni Wastaafu Malecela, Kawawa, Mwinyi, Salim na Msuya. Huku wako hawa walioshupalia RDC;-Mwakyembe, Kilango-Malecela, Seleli, Kimaro, n.k.

2. Team Mkapa; huku ni wale wajanja wa Che-Nkapa ambao bado wanatibu majeruhi ya mchakato wa kugombea Urais 2005 na kunyang'anywa tonge la Hatamu za Chama. Hapa kuna Mang'ula, Ngwilizi, Kigoda, Kinana, Warioba na Ruhinda. Katika kundi hili, pia wapo wale waliotajirika na mradi wa Ujasirimali Ikulu; Yona, Mramba, Mgonja, Mkono n.k.

3. Mtandao; Kundi hili lina majeruhi wengi kutokana na kuvunjwa kwa baraza la mwazirina mwegemeo wa kashfa za ufisadi kuwa kwenye shingo zao. Kundi hili, limegawanyika katika sura mbili;

1. Team Kikwete ambayo wamebakia Makamba, Chiligati, Membe, Migiro, Karume

2. Team Rostwassa(Rostam/Lowassa); Karamagi, Msabaha, Nchimbi, Apson, Meghji, Kamala, Masha Diallo, Chenge,

4. Wasiofungamana lakini wana nguvu na ni tishio; Pinda, Mwandosya, Sumaye, Balali, Salmin, Magufuli, Msekwa na Sitta.

Serikali mpya na baraza lake la mawaziri bado ni ya Kikwete Lowasa na Rostam.

Masha-Mambo ya ndani, bila Lowasa Bw. Mdogo Masha asingekuwa hapo alipo, ni lowasa aliyemshika mkono na kumwingiza kwenye siasa, kwani yeye Masha na Business partner wake Magai walikuwa private lawyers wa mamvi, na hata Magai aliwahi kupatiwa ujumbe wa bodi ndani ya city water wakati huo Lowasa ni waziri wa maji. Je unategemea Masha atasahau alikotoka kama JK asivyomtupa Hussein Mwinyi???? Hao polisi, Manumba na Magereza vyote viko chini ya Masha. Sasa je, nani atamkoma Nyani giradi????

Ngeleja-Nishati na Madini- Huyu alikuwa mwanasheria mkuu wa Vodacom Tanzania LTD ambako Rostam na lowasa wana hisa japo mamvi ni silent share holder. Ni Rostam aliyemshika mkono Ngeleja akagombee Sengerema na kumpatia fungu la kutosha ashinde. Na ndio maana ameachwa madini ili aendelee kulinda migodi ya Rostam. Hivyo tusitarajie mabadiliko makubwa.

Mkullo-fedha- Huyu akiwa mkurugenzi wa NPF sasa NSSF alichota mapesa kibao kumuunga mkono JK mwaka 1995, hivyo ni senior mwanamtandao. Na ndio maana Mkapa alipoingia madarakani akamtema NSSF.

Chenge- Miundombinu, JK hana namna, hampendi Chenge lakini anakuwa forced na Lowasa na Rostam. Mikataba yote kuanzia IPTL n.k imesainiwa wakati wa Chenge na yeye anaelewa nani ni nani katika hayo makampuni yanayozidi kuutafuna utajri wa taifa hili na kutuacha watanzania tukilalia chips kavu. Eti JK atamtosa Chenge! THUBUTU! Atasema kila kitu ! Na ndio maana wakamuwahi Salome mbatia wakamuua ili asiendelee kutoa siri kwa wapinzani kuhusiana na pesa za BOT, kwani yeye ndo alikuwa Mweka hazina mkuu wa chama wakati wa uchaguzi

Kutokana na kuwepo makundi haya makubwa na utata unaotambaa angani hasa baada ya Lowassa kuangushwa na minong'ono kuwa naye Lowassa ana ushahidi wa kujikosha, linalobakia kwetu watazamaji ni kupima upepo na kuomba dua wapigane na wagawanyike ili tujue nani ni kwa manufaa ya Taifa na nani ni mnyonyaji.

CCM si salama, na hata kama wakitoka nje ya ukumbi wakiwa wamekumbatiana, tusiwaamini
MAFIOSO (MAFIA) AND GAMBINO ERA
 
.................Ngeleja-Nishati na Madini- Huyu alikuwa mwanasheria mkuu wa Vodacom Tanzania LTD ambako Rostam na lowasa wana hisa japo mamvi ni silent share holder. Ni Rostam aliyemshika mkono Ngeleja akagombee Sengerema na kumpatia fungu la kutosha ashinde. Na ndio maana ameachwa madini ili aendelee kulinda migodi ya Rostam. Hivyo tusitarajie mabadiliko makubwa.................


....na keshaanza kutuletea miswada wake wa ajabu ajabu kuhus umeme ili ku-babysit HIS BROTHERS MAFISADI......SHAME ON YOU!!.... NGELEJA.....naona unafuata nyayo za kaka yako Karamagi......SHAME ON YOU!!
 
....na keshaanza kutuletea miswada wake wa ajabu ajabu kuhus umeme ili ku-babysit HIS BROTHERS MAFISADI......SHAME ON YOU!!.... NGELEJA.....naona unafuata nyayo za kaka yako Karamagi......SHAME ON YOU!!

kWA MAMBO HAYA KWELI NAAMINI KUWA JK LOVES RUBBISH....... TENA NADHANI VITU TUIHAMISHIE KWAKE ILI AONJE FUKUTO KAMA SII KUUNGUA NA TUANZE SASA KUPIGA KAMPENI KUBWA YA KUWAELIMISHA WATZ KUTO VOTE FOR HIM..
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom