Wamissionari wanakumbukwa Kwa kuuleta ukoloni Afrika

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,307
12,602
Kila nikiwaona watu wa dini wananikumbusha namna ukoloni ulivyofika Afrika ikiwemo Tanzania.

Hawa ni watu ambao walikuja Kwanza kabla ya wakoloni (wanyonyaji) kufika na kuua machifu wetu waliokataa kunyonywa na kutawaliwa. Jambo la kushangaa na kutisha hawa watu wa dini ( missionaries) walikaa, waliishi na kushirikiana vizuri sana na wakoloni wetu waliohamisha rasilimali na watu wetu kwenda kwao. Hawakuonyesha kukerwa na vitendo vya wakoloni hata kidogo, wakoloni walikuwa wanakwenda kusali kwenye makanisa na misikiti yao bila kukemewa vitendo vyao vya kupora mali za wanyonge kwenda ulaya na uarabuni.

Hii ilimaanisha kuwa kupora mali za wanyonge ilikuwa sawa na halali kwa watu wa dini. Hii inanifanya hadi leo niamini kuwa makanisa na misikiti ni lango kuu la uporaji wa mali za wanyonge hata leo, maana quran na Bible waliyokuwa wanaitumia wakati wa ukoloni ni hii hii wanayoitumia leo.

Kama tusiposhituka dini zitatufanya Afrika tuendee kuwatumikia wazungu na waarabu milele Kwa kufahamu au bila kufahamu. Sera zao hazichukii unyonyaji wa aina yoyote hata ikibidi utumwa. Sioni kama kuna tofauti ya mahubiri, vision na mission kati ya wamissionari wale na hawa wa leo. Sikumbuki ni wapi wamionaries walipowahi kuukemea, ukoloni na vitendo vyao vya kibaguzi na kinyonyaji Kwa watanzania.

Kama Rais Magufuli akitaka kuleta ukombozi wa kweli wa taifa hili atupie macho mara tano tano misikiti na makanisa, huu ndio mkono, macho na masikio wa mkoloni uliobakia Afrika, ukisaidiwa na World Bank, IMF na World Trade Organisation.

Kitulacho kiko nguoni mwetu, akili Yao yote iko ulaya, Marekani na Uarabuni. Ukiunganisha ardhi yooote wanayoikalia Afrika, vitagauchumi vyoote wanavyovimiliki Afrika na Kodi wanayotulipa waafrika utagundua kuwa kazi bado tunayo waafrika, ukoloni bado upo na ndyo maana aAfrika yote kusini mwa jangwa la Sahara Kwa pamoja haipigi hatua.
 
Angalia walitupatia Elimu na kutuachia mashule.
Shule zilitumika kama chombo cha kuendeleza mipango ya kikoloni. Angalia ni akina nani waliokuwa wanasoma kwenye shule hizo na nalengo ya kuwasomesha. Angalia ni aina gani ya elimu ilikuwa ikifundishwa kwenye hizo shule.

Shule/madrasa zilikuwa pia nyia ya kuwapa wa kujiunga na dini hizo.
 
binafs nawashukuru sana wakolon. na cjui kama c wao kuja huku tungekuwaje hiv leo. kama ya wakolon kuja kulikuwepo tawala za jadi zenye tabia mbaya mara kumi ya hizo za wakolon. haikuwekana uwe na nyumba su mke au utajir kuliko machifu wale. hawakuwa na mipango yoyote waliokuwa nayo zaid ya kutuswaga kama mbuz hawa machifu. wazungu wametufundisha ustaarabu japo walikuwa na malengo yao ambayo kawaida hata ingekuwa ni wewe huwez kumsaidia mtu yeyote bila malengo. tatizo kubwa mi ninaloliona Africa hawasemi ukweli na pia hawajui kula na kipofu. nchi zote zilizoendelea zilitawaliwa kipindi flan lakin wao hawakuwa na zile tabia za kuwaita waliowatawala mashetan halafu wakaachana nao moja kwa moja waliwatoa kwenye mamlaka then wakaendelea kuwa nao mdogomdogo mpaka walipojitosheleza kila idara na hata hivyo wameendelea kuwa nao. cc waafrica ni wabaguz wakubwa kila kitu tunakitizama katika hali ya mapungufu yake wanasahau kila pungufu kuna la kujifunza.
 
Kitali uko sahihi, lakini tusingetaifisha shule zile, ardhi na mashirika yale wewe leo usingesoma huenda. Au ungesoma Kwa gharama ya kuwa mkatoriki, mluteri, Anglican, au muislam tena wa Sunni au Sher.

Kosa tulililofanya na tunaloendelea kulifanya ni kusahau kuwa wamissionari ndio waliouleta ukoloni, nisehemu ya wakoloni na hawakuonyesha kukerwa na tabia za wakoloni hata kidogo. Hatukutaka kuchunguza uhusiano wa dini na wakoloni baada ya wakoloni kuondoka Africa. Tuliendelea kupokea masheikh, mapadre, maaskofu kutoka Kwa wakoloni bila kuwa na hofu kubwa. Tuliendelea kutoa misamaha ya kodi Kwa misikiti na makanisa bila kujiuliza maswali mengi, tuliendelea kuwamilikisha mapande makubwa ya ardhi bila kuhofia chochote.

Ushahidi upo mkubwa kuwa wakoloni Kwa kutumia dini hizi wanatuchagulia aina ya viongozi Kwa maslahi Yao. Ona kule DR Congo kanisa linasema nani anafaa na nani hafai kwaajili ya kulinda maslahi ya wakoloni wanaonufaika na mali za Congo.
Tumeshawahi kujiuliza % gani ya faida ya biashara za mashirika ya dini Afrika inavunjwa kwenda Kwa wakoloni? Makusanyo ya Ada za shule, hospital, viwanda, nyumba za kulala na mikutano, hotel, nk faida inakwenda wapi? Safari za kwenda kuhiji zinaingiza hela ngapi katika nchi hizo kila mwaka?
 
broda nimetangulia kusema kila binadam anajitahid kujiweka bora zaid. na hata kama wewe ndio ungekuwa ni hao wakolon ungefanya hayo hayo. leo afrika inamiaka hamsin na kitu lakin unaweza kuamin hata jengo la makao makuu ya afrika tumejengewa kwa msaada na wachina? kwan tulitafuta uhuru ili iweje? kwa mfano ukimwangalia jacob zuma kakaa msituni miaka zaid ya 40 kupigania uhur then anakuja kuwa rais kaz ni wiz na uzinz tu. bro ukolon ni mfumo ambao hata wewe unaweza kuutengeneza. ukiweza kutafuta hela na ukajijengea kataasisi kako imara kuna sehem ya watu utawatawala hiyo ni nature mzee. kuna watu kwa asili hawana future wao kila wanachowaza ni leo basi. so kama unafikir hao watu weupe wanatutawala kupitia din au vyovyote unafikir ninan anatutawala kwa matakwa yetu? yeyote anaekutawala ni kwa matakwa yake lakin yeyote anaetuongoza ni kwaajili yetu. so mimi napinga kabisa hii dhana ya ukolon kuitawala africa naweza kukubaliana na wewe kama utakiri ukweli huu kuwa africa ndio jamiii dhaifu zaid ya kibinadam inayoish na sio kuwasingizia watu wengine.
 
Walipokuja Sisi tulikuwa na ardhi na wao walikuja na biblia ba wakatufundisha biblia tulipoijua na kujua kusali ndip walipotuambia tufunge nacho tusali ba baada ya kumaliza sala tulupofungua macho tu, tukajiona sisi tuna biblia na wao wamechukua ardhi zote na ndio mpaka Leo tumebaki na mabibllia ba ardhi hatujajua tufanye nini???

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Walipokuja Sisi tulikuwa na ardhi na wao walikuja na biblia ba wakatufundisha biblia tulipoijua na kujua kusali ndip walipotuambia tufunge nacho tusali ba baada ya kumaliza sala tulupofungua macho tu, tukajiona sisi tuna biblia na wao wamechukua ardhi zote na ndio mpaka Leo tumebaki na mabibllia ba ardhi hatujajua tufanye nini???

Sent using Jamii Forums mobile app
hiyo ni stor tu kama za kwenye kanga.
 
Kaka yangu Kitali haiwezekani viongozi wooote kusini mwa jangwa la Sahara wawe wezi wasiopenda Maendeleo ya nchi zao na watu wao. Lazima ipo common factor inayowahujumu viongozi wetu Kwa pamoja ambayo inaapply katika nchi hizi zote.
Unapotaka kuitafuta hii factor inayowahujumu viongozi wetu Kwa pamoja kwa wakati mmoja lazima factor ambayo iko katika nchi zote hizi. Tunaona factor hizi ni uwepo wa misikiti na makanisa, uwepo wa madeni makubwa, uwepo wa IMF, WB, WTO.

Una mkopo wenye riba kubwa, una watu wanaokupangia bei ya mazao yako, una watu wanaoingiza bidhaa zao kwako Kwa bei waliyoipanga wao, una watu unaowapa misamaha mikubwa Kwa kisingizio cha dini, una watu waliochangia kumuingiza madarakani kiongozi wanaemtaka Kwa faida Yao, kuna watu wamehodhi mapande makubwa ya ardhi bila kuyalipia Kodi stahiki Kwa kisingizio cha dini, kuna watu waliosamehewa kulipa kodi kwenye shughuli za uzalishaji mali kama mashule, hospital, viwanda, majumba ya kulala wageni na mikutano, nk. Kiongozi anayeingizwa madarakani na dini fulani au watu fulani unategemea atafanya nini Kwa waliomsaidia kukamata madaraka?
Iko siku tujaribu kuchagua kiongozi mpagani asiyesali kokote ili tuone hali itakuwaje?

Kuna siku tulishghudia kiongozi anarudisha fadhira Kwa kuwarudishia watu wa dini mali zao zilizotaifishwa na Nyerere kama sehemu ya makubaliano.

Haiwezekani Marais wote wawe wajinga kiasi hiki, nina uhakika Rais atakayekataa nchi yake kunyonywa atakuwa kwenye misukosuko mingi inayohatarisha uwepo wake kwenye nafasi hiyo au hata kuuawa. Ukiona kiongozi wa nchi hizi za kusini mwa jangwa la Sahara anasalia madarakani milele bila kunyooshewa kidole na dini fulani au nchi za kikoloni ujuwe kuwa huyo ni mwenzao Kwa maslahi Yao.
 
Kaka yangu Kitali haiwezekani viongozi wooote kusini mwa jangwa la Sahara wawe wezi wasiopenda Maendeleo ya nchi zao na watu wao. Lazima ipo common factor inayowahujumu viongozi wetu Kwa pamoja ambayo inaapply katika nchi hizi zote.
Unapotaka kuitafuta hii factor inayowahujumu viongozi wetu Kwa pamoja kwa wakati mmoja lazima factor ambayo iko katika nchi zote hizi. Tunaona factor hizi ni uwepo wa misikiti na makanisa, uwepo wa madeni makubwa, uwepo wa IMF, WB, WTO.

Una mkopo wenye riba kubwa, una watu wanaokupangia bei ya mazao yako, una watu wanaoingiza bidhaa zao kwako Kwa bei waliyoipanga wao, una watu unaowapa misamaha mikubwa Kwa kisingizio cha dini, una watu waliochangia kumuingiza madarakani kiongozi wanaemtaka Kwa faida Yao, kuna watu wamehodhi mapande makubwa ya ardhi bila kuyalipia Kodi stahiki Kwa kisingizio cha dini, kuna watu waliosamehewa kulipa kodi kwenye shughuli za uzalishaji mali kama mashule, hospital, viwanda, majumba ya kulala wageni na mikutano, nk. Kiongozi anayeingizwa madarakani na dini fulani au watu fulani unategemea atafanya nini Kwa waliomsaidia kukamata madaraka?
Iko siku tujaribu kuchagua kiongozi mpagani asiyesali kokote ili tuone hali itakuwaje?

Kuna siku tulishghudia kiongozi anarudisha fadhira Kwa kuwarudishia watu wa dini mali zao zilizotaifishwa na Nyerere kama sehemu ya makubaliano.

Haiwezekani Marais wote wawe wajinga kiasi hiki, nina uhakika Rais atakayekataa nchi yake kunyonywa atakuwa kwenye misukosuko mingi inayohatarisha uwepo wake kwenye nafasi hiyo au hata kuuawa. Ukiona kiongozi wa nchi hizi za kusini mwa jangwa la Sahara anasalia madarakani milele bila kunyooshewa kidole na dini fulani au nchi za kikoloni ujuwe kuwa huyo ni mwenzao Kwa maslahi Yao.
hilo tatizo unaloliongelea viongoz wetu walishalijua tangu mwaka 1960 na bado hawajajipanga namna ya kulitatua walichobaki nacho ni kulia lia tu na kulaumu na kuachia matatizo yajitatue kimiujiza. we kubali tu waafrica ndio jamii dhaifu zaid.
 
hilo tatizo unaloliongelea viongoz wetu walishalijua tangu mwaka 1960 na bado hawajajipanga namna ya kulitatua walichobaki nacho ni kulia lia tu na kulaumu na kuachia matatizo yajitatue kimiujiza. we kubali tu waafrica ndio jamii dhaifu zaid.
Gadaff alitaka kuwasaidia kulitatua lakini wakamuua kabla ya kukamilisha mpango wake huo. Nyerere alijaribu kujikomboa lakini alishindwa, walimuwekea vikwazo vya kiuchumi vya kila aina hadi akambia mwenyewe baba wa watu kwa njia ya kung'atuka. Nyerere na akina Nkrumah walizunguukwa na Marais vibaraka ndani ya OAU hivyo kila wanalosema na kupanga halifanikiwa.
 
Kama Africa tunataka kumkamata mbaya wetu anayetuvuta chini tuanzie miguuni kwetu humu tunamosali, haiwezekani tumkabidhi maisha rafiki wa adui(mkoloni) yako ambaye amekuuza kama mtumwa, hamkemei anayekunyima fursa za biashara ya mazao yako, anayekuwekea vikwazo vya kiuchumi vya kila aina, anayehalalisha ushoga, anaebwaga mabomu Kwa watu wengine bila huruma. Rafiki ya adui yako ni adui yako pia.
 
Back
Top Bottom