Wamisri wa kale walikuwa weusi(Africans)

Pia ni nani aliyetoa jina Africa??? Ni nani aliyetuita Waafrika??? Hapa kuna conspiracy kuficha historia ya mtu mweusi. Binafsi naamini na nitaendelea kuamini kwamba Waisrael wa leo sio wale waliotajwa kwenye Biblia na kwamba Binadamu wa kwanza aliishi Afrika na kama ndivyo hivyo Adam na Hawa walikuwa watu weusi wakiishi pale Olduvai Gorge. Kuna kitu kilifichwa hapa, Mwaka 2015 aliyekuwa Waziri Mkuu wa Israel Ehud Baraka alifunga safari yeye na wayahudi wenzake kuja Tanzania kuona mahali alipoishi mtu wa kwanza. Halafu Mitanzania imekodoa macho badala ya kutafiti kujua ukweli yamekalia kuiba fedha za umma na kusahau tunu kama hizi.
Nahet kobet
 
"Misri ilikua ni Afrika kwa maandishi yake,utamaduni wake na namna yake ya kufikiri" .Hivi ndivyo anavyohitimisha mtaalamu wa masuala ya kale ya Misri(Egyptologist) raia wa Ufaransa Jean Vercoutter na mpinzani wa Cheikh Anta Diop katika mkutano wa Cairo juu ya utambulisho wa Wamisri wa kale.

Mkutano wa Cairo ulifanyika Mwaka 1974,UNESCO taasisi ya kimataifa yenye uwezo wa kuamua masuala kama hayo,ilikubali kua Cheikh Anta Diop na Theopile Obenga wako sahihi kua Misri ya kale ilikua ni ustaarabu(Civilazation) wa kiafrika katika nyanja zote,hii ilitokea baada ya malumbano makali kati ya Egyptologist wawili wa Kiafrika na wenzao wawili.

USHAHIDI

Tofauti na mtu atakavyoelekezwa kuamini,Misri ilikaliwa na watu waliokua wanahamia kutoka Kusini kwenda Kaskazini na watu weusi walioitwa Anu. Hawa ni watu waliotokea Kusini mwa Afrika na maeneo ya maziwa makuu ambao walilowea kwanza ilipo kwa sasa Sudan na Kusini mwa Misri.Ni Watu jamii ya Anu polepole ndio waliofuata bonde la mto Nile na kuitia Kaskazini yote mpaka Delta katika himaya yao.
Ustaarabu wa Misri una mizizi yake kutokea Kusini mwa Afrika na eneo la maziwa makuu sababu eneo hili ndio binadamu wa kwanza walizaliwa na ndio bakibaki(traces) za ustaarabu wote wa binadamu unaweza kuonekana( rejea mambo ya Oldupai Gorge) na hii ndio sababu kwa nini eneo hili Wamisri wa kale waliliita Ta Ntjer maana yake ardhi takatifu au ardhi ya Mungu.

Na kwa urithi huu uliopatikana katikati mwa Afrika kwa miaka 170,000 uliowezesha Anu kuijenga Misri kutokea kusini kwenda kaskazini.Hisabati, Kuandika, Kilimo, Usanifu Majengo, dini nakadhalika vyote vilianzia Afrika na Sudan na vilikuzwa zaidi na Wamisri.

Mafarao wa kwanza walitawala upande wa kusini kwa maelfu ya miaka,ilikua ni Msudani alieitwa Nare Mari ndie aliyemaliza kuiteka Delta ya mto Nile na Kuunda Falme ya Misri(Dynasty) iliyoungana mnamo mwaka 3300 BC.

Jina la Misri na Wamisri

Jina walilojipa na jina walilolipa bara lao pasi na shaka linaonyesha waziwazi asili(race) yao. walitumia jina(mzizi) Kam/Kem ikiwa na maana iliyopakwa makaa(coal coated) kwahiyo walikua ni weusi.Ambao ni sawa na Kemi/Kembou/Kheum/Kala ikimaanisha coal(makaa), iliyounguzwa , nyeusi katika Lugha nyingi za Kiafrika.

Michoro na Sanamu zote za Farao zinaonyesha waziwazi hawa ni watu weusi,kuanzia utawala wa kwanza(first dynasty) mpaka uvamizi wa Wagiriki.
Narmer-1st-Dynasty.jpg

Ingawa wamejaribu kuziharibu pua zao ila tazama walivyo na midomo mipana.
images


-Ushahidi mwingine ni kipimo cha vina saba na majaribio katika ngozi kwa kuangalia uwingi wa melanin.
-Familia sawa ya Lugha ,tamaduni sawa na dini sawa na waafrika wengine kwingineko.
Egyptologist wote wa Ulaya walishindwa kuonyesha uwiano kati ya Kimisri na lugha za Endo European ambazo ni ''semitic'' kama Arabic na Hebrew,Ni Cheikh Anta Diop katika miaka ya 50 aliyegundua usawa kati ya Wolof(Lugha yake) na Kimisri
-Mfumo wa familia ulioegemea upande wa mama(matriachy),jinsi mazishi yanavyofanywa na mpangilio wa ufalme,kila kitu katika tamaduni za Misri kinafanana na tamaduni za kusini mwa jangwa la Sahara. Dini ya Misri ambayo imeandikwa sana na inaendelea kuandikwa ni sawa na ile inayofanywa na watu weusi. Misri haikuamini katika Mungu zaidi ya mmoja(polytheistic) na wana sayansi wote wanajua hii na wakapandikiza propaganda kua Misri iliamini katika Miungu ili wainyime Afrika heshima yao kua wao ndio wa kwanza kuabudu katika Mungu mmoja.

Ushahidi mwingine ni kutoka kwa Wasomi wa Ulaya wenyewe mfano Wagiriki wa kale kabisa wanaoheshimika kuja Afrika wanasema Wamisri waliokutana nao ni weusi

Herodotus,anajulikana kama baba wa historia anaandika hakika kabisa Colchians(watu walioishi kando ya Black Sea) wana asili ya Misri(are of Egyptian race) kwa sababu walikua na ngozi nyeusi na nywele frizzy.

Aristotle,penginepo mwenye ushawishi mkuu katika ufikiri wa Kimagharibi anasema wale weusi sana ni waoga,hii ni kwa Wamisri na Waethiopia.

Aeschylus,mwana mashahiri akielezea meli ya Wamisri ikiondoka, i notice the crew with its black members bringing out the white tunics.

hata wakati wa utawwala wa Rumi,miaka 250 kabla ya uvamizi wa waarabu bila kujalisha uwepo wa ngozi nyeupe Misri kwa miaka 600 Ammian Marcellin, rafiki wa mtawala wa Rumi Julius anasema watu wa Misri kwa wingi wao ni wekundu(brown) au weusi.


Kama Wamisri walikua weusi,watu weupe wanatoka wapi?

Ustaarabu wa Misri ulianza miaka 27,000 iliyopita,miaka 19,000 kabla ya kuonekana kwa mtu mweupe.Uvamizi wa kwanza mkubwa wa weupe ulikua ni ule wa mwaka 663 BC wa Assyrians
Baada ya hapa Misri ikaanza kuyumba.ikavamiwa tena na Persia na Wagiriki waliomaliza tawala zote za Misri wakaja Warumi na Mwisho kabisa Waarabu walioingia Misri kama sehemu ya Uvamizi wa Kiislam karibia miaka 1000 baada ya utawala wa mwisho wa wazawa.
Waarabu walivyoingia Misri wazawa walikua wamekimbilia pande nyingine za Afrika kati yao wapo Sonike wa Mali,Akan wa Ghana,Yoruba wa Nigeria, Bassa wa Cameroon na hata Zulu na Xhosa wa Afrika Kusini. Weusi waliobakia Misri walizaliana na wavamizi ambao hiki kizazi kinaitwa Copt.
hii inaelezea kwa nini hawa Copts ni weupe lakini wanaongea BLACK TONGUE .Waarabu hawana lolote kuhusu ustaarabu wa Misri na wako makini kutosema ili wakusanye pesa ya utalii Misri.

Kama Misri ilikua ya weusi,kwa nini weusi hawana akili?

Hili ni swali maarufu sana linaloulizwa na Waafrika waliomeza propaganda ya kua mtu mweusi ni inferior.Lazima ufahamu kua baada ya uvamizi wa wageni Misri iliyumba sana, ila kutoa Misri,Afrika kwingineko ustaarabu ulizaliwa.
Mpaka mwanzo wa biashara ya utumwa ya wazungu,Afrika ilikua imetapakaa Falme nyingi maridadi na ilikua bara tajiri kuliko yote. Hujawahi kujiuliza kwa nini Mansa Musa ambae aliishi karne ya 14 ndie mtu tajiri kuliko wote kuwahi kutokea?(Meet Mansa Musa I of Mali – the richest human being in all history)Ni utumwa na ukoloni ndio umewafanya waafrika wajione wako nyuma. Na haieleweki kwanini tunaambiwa udhaifu wetu ni wa asili tumeweza kujenga ustaarabu ambao ulikuja kuambukiza dunia nzima.
Hii habari ni ngumu kumwingia mtu mweusi sababu haijasemwa na maneno takatifu ya wazungu.

Nimejaribu kutafsiri kutoka
The ancient Egyptians were Black
Nahesh sebet
 
Hapa hukuwa na Torati, Biblia, Koran wala imani za kuletwa ambazo kimsingi zote zinatu undermine (ukweli).
Japo ukweli unaouma ni kwa nini hao wengine walipata wazo la kuja kutuvamia na sio sisi kuwavamia wao!?
Inabidi Waafrika tujichukulie kama nguo zinazofuliwa kwamba muda huu tumelowekwa na baada ya muda fulani labda 'tutatakata' hivyo kurudia ubora wetu kama ilivyokuwa hapo awali!
Inauma akini myahudi Ni mwongo he can't be trusted
 
Ni kweli mkuu inafikirisha sana tena sana tu.....

Lakini kikubwa na kibaya zaidi ni kwamba kuna watu weusi hasa kutoka mashariki mwa Afrika walipelekwa utumwani kule India na kuna kijiji kukubwa sana eneo moja kule Inadia wanaishi huko na wanajua kuwa walitoka huku mashariki mwa afrika,nimesahau eneo husika nikikumbuka nitalitaja hapa....

Watu wale walitoka hasa Kenya na sehemu za pwani ya Afrika ya mashariki.Ni masikini wa hatari kabisa kule na serikali ya India ni kama imewatupa hivi.Mkuu,sisi huku tunaishi maisha ya kishenzi lakini wale ni kama wapo shimoni,inasikitisha sana aisee....

Kwanini historia hizi zinafichwa?

Suala la mtu mweusi na uwepo wake duniani imekuwa kama ni laana.Haya ndiyo maana ninasema yana sababu maalum kabisa na siku siyo nyingi tutafutwa machozi haya ya damu siku itakayoutisha ulimwengu kwa namna ya kutisha kabisa.....

Acha tu waendelee kudanganya....
Na pia kwenye historian inasemekana Australia ilikuwa inakaliwa na watu weusi ila wazungu wakawaua
 
Na pia kwenye historian inasemekana Australia ilikuwa inakaliwa na watu weusi ila wazungu wakawaua
Sio inasemekana,hilo ni jambo lililo wazi kabisa kila mtu conscious analijua.

Waingereza waliingia hapo nusu ya pili ya karne ya 18,watu wenye asili ya bara Afrika walikua tayaru wameshafika huko kitambooo.
 
Vigelele imeandikwa kwenye Biblia.Akina Mama walipiga vigelegele.Makanisani hadi hii leo hupiga vigelegele.Huo ni utamaduni wetu bila shaka yoyote.
 
Wazungu kwa fitina na wivu wamefanya kula jitihada kutudhoofisha sie superior black race the chosen one by God baada ya kugundua uwezo wetu na upendeleo aliotupa Mungu but hakuna kitu kitadumu milele ukweli utadhidi kuwekwa wazi ni suala la mda tu,ni kama kesi ya Yusufu na nduguze ndo inatuponza.Pili Mungu aturehemu sana wake kama babu zetu hawakufuata amri zake turejee kwenye enzi yetu ya ustawi kama kale
 
49 Reactions
Reply
Back
Top Bottom