Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,709
Nilimuambia bukoba boy kwamba kuna uwezekano mkubwa sana kwamba sisi Wabantu tukawa ndiyo wale Wasraeli halisi kwa maana ya wana wa Yakobo...Deuteronomy 28:15 na kuendelea ni mwiba.
Mkuu Eiyer unamaanisha maisha ya mtu mweusi ni matokeo ya kutotii maagizo ya Mwenyezi Mungu?.
Fafanua tafadhali.
Kwasababu hiyo,ukiangalia maandiko Wayahudi [Waisraeli walioishi kusini mwa Israeli baada ya mgawanyiko wa mwaka 670 b.c] na pia Waisraeli wa kaskazini mwa Israeli walimkataa masihi,na siyo hilo tu bali walikaidi maagizo ya Mungu....
Kwenye Kumbukumbu 28 kuna baraka na laana kama watafuata maagizo yake na kama watayakaidi.Sasa ukisoma hizo laana kwakuwa walikwenda kinyume na maagizo ya Mungu utaona kabisa utadhani mwandishi alikuwa anatuangalia sisi kwa yale yanayotupata....
Ndiyo nikasema kwamba hii inatuhusu kama nitakuwa sahihi kuhusu Wabantu kuwa Waisraeli halisi....