Wamiliki wa magari mnajua hili?

RRONDO

JF-Expert Member
Jan 3, 2010
51,719
107,770
Leo nimesikia redio kuna taasisi hapa Tanzania itakuwa inakagua/inapima moshi wa magari kujua kama uko sawa kwa mazingira yetu, yaani vehicle emission standard.

Kwa nilivyosikia redioni hawa wapimaji wakiona gari lako halijafaulu viwango vyao wanatoa number plate na kukwambia ukarekebishe, gari halitaruhusiwa kutembea mpaka lirekebishwe.

Sasa nina maswali kwa wahusika natumaini masali yangu yatasaidia wengi.
1.What is the vehicle emission standard kwa Tanzania?

2.Huko tunakoagiza magari huwa mnawapa emission standard zetu ili magari yakija yakidhi hizo standard?

3.Emission standard zinatofautiana nchi na nchi na Tanzania tunanunua magari kutoka nchi mbalimbali je watawezaje kupambana na hio changamoto?

4.Magari mengi ya zamani (<2005 ) hayafikii emission standard za >2010 na wenzetu huko wana phase out taratibu hizo gari nyinyi hapa mtafanyaje na gari nyingi hapa Tanzania ni za miaka 10 au zaidi iliopita.
Mfano kuna magari yana catalytic converter na mengine hayana hasa hasa ya Japan kuanzia 2005 kushuka hili mnalichukulia vipi?

5.Gari zilizojaa 'showrooms' mmezipima kabla ya kuuziwa sisi ili tukinunua msije kuzikamata na kutoa number plate?

Wakaguzi wa haya magari naomba mjibu maswali haya natumaini mtatusaidia maanake tunakoelekea mtatoa number plates za magari mengi sana na yatabaki ya serikali yale mapya tu!

Emission standard - Wikipedia
 
Hawa ni wababaishaji kama wababaishaji wengine tu, walitakiwa wakamipe huo upuuzi wao kule ambapo gari zinatoka, haiwezekani ulipie TBS pre-shipment inspection fee karibu dola 300 au zaidi na ifike tanzania eti utoe plate namba ya gari..sasa ile pre-shipment ni ya nini??
 
Leo nimesikia redio kuna taasisi hapa Tanzania itakuwa inakagua/inapima moshi wa magari kujua kama uko sawa kwa mazingira yetu, yaani vehicle emission standard.

Kwa nilivyosikia redioni hawa wapimaji wakiona gari lako halijafaulu viwango vyao wanatoa number plate na kukwambia ukarekebishe, gari halitaruhusiwa kutembea mpaka lirekebishwe.

Sasa nina maswali kwa wahusika natumaini masali yangu yatasaidia wengi.
1.What is the vehicle emission standard kwa Tanzania?

2.Huko tunakoagiza magari huwa mnawapa emission standard zetu ili magari yakija yakidhi hizo standard?

3.Emission standard zinatofautiana nchi na nchi na Tanzania tunanunua magari kutoka nchi mbalimbali je watawezaje kupambana na hio changamoto?

4.Magari mengi ya zamani (<2005 ) hayafikii emission standard za >2010 na wenzetu huko wana phase out taratibu hizo gari nyinyi hapa mtafanyaje na gari nyingi hapa Tanzania ni za miaka 10 au zaidi iliopita.
Mfano kuna magari yana catalytic converter na mengine hayana hasa hasa ya Japan kuanzia 2005 kushuka hili mnalichukulia vipi?

5.Gari zilizojaa 'showrooms' mmezipima kabla ya kuuziwa sisi ili tukinunua msije kuzikamata na kutoa number plate?

Wakaguzi wa haya magari naomba mjibu maswali haya natumaini mtatusaidia maanake tunakoelekea mtatoa number plates za magari mengi sana na yatabaki ya serikali yale mapya tu!

Emission standard - Wikipedia
Sheria mpya Na utaratibu mpya unatakiwa kuanzia pale ulipoanzishwa nasi kurudi nyuma hiyo sio haki Na nikosa kisheria.Hata kwenye Showroom GARI ambazo azijauzwa lakini zilisha letwa nchini kabla ya utaratibu huu zinatakiwa ziuzwe au walipwe fidia wakaziuze kwingine.
 
Sheria mpya Na utaratibu mpya unatakiwa kuanzia pale ulipoanzishwa nasi kurudi nyuma hiyo sio haki Na nikosa kisheria.Hata kwenye Showroom GARI ambazo azijauzwa lakini zilisha letwa nchini kabla ya utaratibu huu zinatakiwa ziuzwe au walipwe fidia wakaziuze kwingine.
Watujulishe pia gari ikifeli garage gani tunaweza kurekebisha wenye vipimo vinavyoonesha standard zao zimefikiwa.
 
Hawa ni wababaishaji kama wababaishaji wengine tu, walitakiwa wakamipe huo upuuzi wao kule ambapo gari zinatoka, haiwezekani ulipie TBS pre-shipment inspection fee karibu dola 300 au zaidi na ifike tanzania eti utoe plate namba ya gari..sasa ile pre-shipment ni ya nini??
Hivi vipimo kwa nchi zilizoendela mfano EU countries unafanya kwa mwaka mara moja wakati unafanya MOT. Sasa hapa TZ tunafanyia wapi? Au ndio wanakaa barabarani kukamata watu na kulets usunbufu? Hii ndio ilitakiwa iwe kazi ya sticker za nenda kwa usalama. Gari ikipewa ile sticker ina maana imequalify kutembea kwa mwaka mzima.
 
Hawa wameanza tena kujitekenya.... Unamuhukumu mtu kwa kujamba Wakati kunde umemlisha wewe.?? Tunatuma watu TBS Huko tunaponunua magari, na wanatoa certificates kabisa, na wanalipwa kwa kodi zetu, leo mnakuja kusema upupu gani?? Tumekuwa tunalalamikia mafuta na vilainish vilivyopo madukani havina viwango nyie mnakagua moshi....

Naomba kujua taratibu za kupata hifadhi ya kikimbizi nje.
 
Hivi vipimo kwa nchi zilizoendela mfano EU countries unafanya kwa mwaka mara moja wakati unafanya MOT. Sasa hapa TZ tunafanyia wapi? Au ndio wanakaa barabarani kukamata watu na kulets usunbufu? Hii ndio ilitakiwa iwe kazi ya sticker za nenda kwa usalama. Gari ikipewa ile sticker ina maana imequalify kutembea kwa mwaka mzima.

Yaani very controversial, hawajui hata garama ya makodi makubwa tunayolipa kwenye hayo magari chakavu.
 
Hawa wameanza tena kujitekenya.... Unamuhukumu mtu kwa kujamba Wakati kunde umemlisha wewe.?? Tunatuma watu TBS Huko tunaponunua magari, na wanatoa certificates kabisa, na wanalipwa kwa kodi zetu, leo mnakuja kusema upupu gani?? Tumekuwa tunalalamikia mafuta na vilainish vilivyopo madukani havina viwango nyie mnakagua moshi....

Naomba kujua taratibu za kupata hifadhi ya kikimbizi nje.

Tena hao watu wa TBS wewe hiyo certificate hupati bure unalipia dola sawa au zaidi ya 300
 
wanatengeneza njia ya mapato kama zile kadi za nenda kwa usalama hakuna jipya porojo tu.... mtu nimeagiza gari chakavu ukanipiga makato ya kutosha kisa uchakavu na kuruhusu iingie halafu inafika unaleta story za gari zinachafua mazingira huu ni upunguani uliopitiliza
 
Hawa wameanza tena kujitekenya.... Unamuhukumu mtu kwa kujamba Wakati kunde umemlisha wewe.?? Tunatuma watu TBS Huko tunaponunua magari, na wanatoa certificates kabisa, na wanalipwa kwa kodi zetu, leo mnakuja kusema upupu gani?? Tumekuwa tunalalamikia mafuta na vilainish vilivyopo madukani havina viwango nyie mnakagua moshi....

Naomba kujua taratibu za kupata hifadhi ya kikimbizi nje.
Ukifanikiwa kupata hifadhi ya ukimbizi naomba na mimi tufatane, namba yangu ni 075348792-
 
Nchi hii haitakaa iishiwe vichekesho, baadaye watasema hata kujamba ni kosa
Hata hivyo ni kosa mkuu, ndio maana inatakiwe ujambe pole pole ili mtu au watu wasijue ni nani Kaachia ushuzi,

Pamoja na hayo napenda sana Kujamba, tena hasa tukiwa wengi (kikundi) Baada ya kuachia nafurahia watu wanapo ulizana kwa kumtafuta mtu Amie jamba, nasikia raha sana.
 
Itakuwa jambo jema ili kunusuru afya na mazingira yetu kwa ujumla.

Hydrocarbon ni hatari sana hatujui tu
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom