Wamiliki wa mabasi ya safari ndefu watakiwa kuhakikisha yanakuwa na madereva wawili

Nyendo

JF-Expert Member
Jun 4, 2017
1,188
4,100
Wito umetolewa kwa wamiliki wa mabasi ya safiri safari ndefu ,kuhakikisha kwamba yanakuwa na madereva wawili ,lengo likiwa ni kupunguza ajali zinazoweza kuepukika, pale dereva anapochoka kutokana na kuendesha gari kwa umbali mrefu

Hayo yamesemwa na Kamanda wa Kikosi cha Usalama barabarani nchini Wilbroad Mutafungwa ,alipokuwa kikazi mkoani Arusha mwishoni wa juma kwamba, ameshatoa maelekezo kwa akwuu wa usalama barabarani kwa mikoa yote ,kuhakikisha wanafanya ufuatiliaji wa kina ,sambamba na suala zima la mashindano ya mabasi ya abiria barabarani

Amewataka madereva wote nchini kuacha mashindano barabarani ,ambayo hayana maana yeyote kwani mara nyingi wamekuwa wakisababisha ajali vifo ,majeruhi na ulemavu wa kudumu pamoja na kuleta hasara,jambo ambalo wangelifuata utaratibu na kuzingatia sheria za usalama barabarani yote hayo yasingelitokea.

‘’Wapo baadhi ya maajenti ambao sasa ndiyo vichocheo vikubwa, nikiwa na maana kwamba wanafanya ile michezo ya kubeti ,gari linalofika sehemu Fulani ikiwa ya kwanza wanabeti wanachangishana fedha.Alisema Mutafungwa.

Kamanda Mutafungwa amewaagiza wakuu wote wa usalama barabarani, wawakamate maajenti ambao ndoyo wanaochochea kubeti,kushangilia ,kuwachochea madereva ili waweze kukimbia mwendokasi, pamoja na dereva mwenyewe kwani ‘’Hatuwezi kubeti na Maisha ya watu’’

Vilevile Kamanda Mutafungwa alipata wasaa wa kuzungumza na abiria waliokuwa katika stendi ya mabasi Arusha :Ninyi ndiyo wadau muhimu katika suala la usafiri, hivyo mnalojukumu kubwa sana la kutusaidia,kuna mahala penine askari wetu wa usalama barabarani hawapo,mnapoona kuna uendeshaji wagari unaovunja sheria za usalama barabarani kwa makusudi na wakati mwingine katika kiwango ambacho kinaweza kuhararisha hata maisha yenu, nawaombeni ndugu zangu abiria ,toeni taarifa kwa jeshi la polisi ili tuweze kumchukulia hatua za kisheria.

Wapo abiria tunapotembea tunawaona wanashabikia sana spidi niwaombe kwasababu leo wewe ni abiria kesho siyo abiria kama Watanzania tujenge tabia ya kuona maovu na kuyakemea kwa pamoja .alisema

Mutafungwa amesema kuwa wapo baadhi ya madereva ambao hawajaacha tabia ambayo imepigwa marufuku ya uendeshaji wa magari kwa mwendo kasi huku wakiwa wamebeba abiria,Unakuta baadhi ya madereva sehemu ambayo anatakiwa kwenda spidi 80,bado anakwenda spidi kubwa zaidi ya hiyo,sehemu abayo ni makazi ya watu anapotakiwa kwenda spidi ya 50, bado baadhi ya madereva wanakwenda mwendo kasi n hata sehemu ya zebra crossing tunashuhudia hayohayo yakitendeka

Herman Malisa ni dereva wa marangu coach alikuwa na haya ya kusema: Ninachowaomba Madereva wenzangu tuzingatie kanuni na sheria za Usalama barabarani,kwani hiyo ndiyo ofisi yetu na wanatakiwa kuiheshimu kwa kutii Sheria bila shuruti

Amewataka kuwa makini sambamba na kuwajali abiria wao kwani wao ndiyo sababu ya wao kuwepo katika vyombo hivyo,sambamba na kuwataka kutokulaghaiwa na maajenti ambao hawana nia njema ,ambao wanawashawishi baadhi ya madereva kukimbiza magari na kutokuzingatia sheria za usalama barabarani

kwa upande wake Katibu wa mabalozi wa usalama barabarani mkoa wa Arusha Wilbald Ngambeki amesema kuwa wao kama RSA Kutoa elimu kwao ni ibada ,kwani elimu hiyo inawasaidia watu wengi ikiwemo abiria kutambua haki yake ya msingi awapo safarini ambayo inampa yeye nafasi ya kutoa taarifa pale anapoona dereva anakiuka sheria za usalama barabarani.

Ngambeki aliwataka abiria kutokuwa chanzo cha vichocheo vya kumshawishi dereva kutembea kwa mwendo kasi ,kwani tatizo litakapotokea majuto anakuwa mjukuu baadae na madhara yanakuwa makubwa.
 
Wakipinga agizo bc watajua n kwann ccm ilishinda kwa kishindo kikubwa
 
Pathetic...

watu wanabet kwenye maisha ya watu...roho za watu hazitawaacha salama

Kabetini kwenye mizuka mitatu sijui biko huko sio kwenye uhai wa raia
 
Back
Top Bottom