Wamiliki wa Gazeti la MwanaHalisi watakiwa kujieleza kwa kukiuka maadili ya uandishi wa habari

Serikali kupitia Idara ya Habari Maelezo yataka wamiliki wa gazeti la MwanaHALISI wajieleze kwa kukiuka maadili ya uandishi habari.

This should have been done a long time ago! Kwanza nasikitika kuwa Serikali imeamua kuwafungia kwa miaka miwili tu. Nilitegemea kuwa lingefungiwa indefinately! Mwanahalisi waliandika gazetini kwenye kichwa cha habari kuwa "ufisadi ndani ya ofisi ya JPM" wakati kichwa cha habari hakina hata tone moja la habari inayohusu ufisadi! Actually mwandishi ameongelea Shirika la Elimu Kibahaaa!. Haya, Serikali ikavumilia na kumwonya tu. Badala ya kumtandika Nondo hapo hapo! Wahenga walisema ukicheza na Mbwa atakufuata hadi Msikitini.
Kwa vile Serikali haikupiga nondo, Mwanahalisi wakawa wanawashwawashwa. Wakaandika tena "Mwakyembe: Maisha yangu Hatarini". Wakajiandikia stori na kumquote Mwakyembe visivyo! Mwakyembe akafura akakemea uongo huo. Hapa serikali ikaendelea kumbeba beba Mwanahalisi kwa kumwambia aache kuandika habari za uongo. Kama hayo hayatoshi. Wakatumia kalamu yao kuandika tena kwa kona ya kiuchochezichochezi kuwa tumwombee Magufuli au Tundu Lissu" Article yenyewe imejaa sumu tu. Sijui lengo la MwanaHalisi nini tena? Mimi kwa maoni yangu Serikali nailaumu sana tena sana kufungia hilo gazeti kwa miaka miwili tu. Dr Abbas, umetuangusha hapa! Ungepiga Nondo ya nguvu.
 
Back
Top Bottom