'' Wamechapwa mbele ya wazai wao Je adhabu hiyo inafaa au ni udalilishaji?''

niibada

Member
Jul 6, 2012
40
6
Nimepita katika pita pita zangu nimekuta watoto wanaosadikiwa kuwa ni watahiniwa wa mwaka huu wakipata viboko katika shule moja iko maeneo ya Kihonda magorofani kama mchezo wa kuigiza Je kulikuwa na tatizo gani?
Nimekuta kuna halaiki ya watu na wanafunzi wakichapwa mwenye taarifa anijuze jamaani na je viboko bado vinaendelea mashuleni maana waalimu zaidi ya wawili walikuwa wakishughulika na kazi hiyo
Na je ni viboko vingapi mwanafunzi anatakiwa kuchapwa kwa mujibu wa sheria za wizara ya elimu?
Je ni kawaida kwa mkoa huu wa Morogoro? au kawaida kwa mikoa yote nchini? maana sikuona hata chombo chochote cha habari mfano wachukua video kwa ajili ya matukio na je Morogoro hakuna waandishi wa habari au wawakilishi wa vyombo vya habari vya nje ya mkoa?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom